LAT nipe Msaada please


mkuu ..... hichi kifaa kinaitwa Badizzo mimi nilinunua TFA Arusha by the time kiligharimu Tsh 40,000/= nadhani pia unaweza kukipata kwenye Vet iliyopo pale ubungo

ningekushauri uweke na Kondoo ..... kondoo ni wazuri sana na hata nyama yao ni tamu tena ni laini sana ...... advantage ya kondoo ni kwamba mzao wao ni mara tatu kwa mwaka pia wana ability kubwa sana ya ku sustain magonjwa ..... kiimani pia kondoo ni mifugo inayosadikika kuleta baraka katika maisha .... haa haaaaa haaaa naomba msini quote hapa

kuna majani yanaitwa luceni na aina fulani ya miti midogo ambayo ni fodders nzuri sana za kuboresha mbuzi ..... nikirudi dar nitakupa mbegu ya miti hii lakini luceni ni mpaka Arusha au labda shirika la elimu kibaha

mkuu .... tafuta vet mmoja akuonyeshe jinsi ya kutibu mbuzi wako rather search kwenye internet utajua, dawa ya minyoo zipo aina mbili, moja wanachoma kwenye misuli (intermascular) especially sehemu ya paja na ni 10mls kwa mbuzi ambaye yupo about 10-20kg under 10kg unachoma 5mls, nyingine inachomwa katikati ya ngozi na myama especialy kwenye shingo dawa hii inauzwa Tsh 4000/= , ipo nyingine ya minyoo ya kunywesha mdomoni..... na antibiotics ni Tsha 4500/= antibiotics huchomwa kwenye misuli tu
 
LAT umekuwa afisa mifugo pia. ha ha ha ha. thanks very much for your valuable information!!
 
Reactions: LAT

Nikushukuru tena kwa ushauri wako,
Tayari nimempata Bi mifugo mmoja, na nitampa kazi ya kuhudumia mifugo yangu kama ulivyoshauri. Kondoo tayari nimepata jibu wapi nitawanunua, wapo Mkamba na bei wameniambia hamsini elfu tu. Badizzo lazima ninunue mwezi huu ili vile vibeberu vichache vilambe castration faster.

Tafadhali naomba kama unavyotarajia kunisaidia hizo mbegu, jitahidi uje nazo,utakuwa umenisaidia pakubwa, gharama zake nitalipa. Be blessed.
 
@kanyagio ,,,,, haha haaaaa ..... a vet by nature


@Malila .... mbegu ya fodders za miti tayari ninayo dar nitakupatia

also think about m'gombe wachache kwa ajili ya biogas ... jamaa wa CARMATEC wanataleta generators zitakazofua umeme kwa kutumia biogas .... hivyo utanufaika na hili
 
 

LAT, nimefanikiwa kutengeneza mtungi wa biogas,kupitia youtube videos,sasa nilikuwa ktk mchakato wa kutengeneza generator ya kutumia hiyo biogas,uliposema kuwa kuna carmatec wanayo na wanauza hizo generators umenistua kidogo na kujenga matumaini kuwa kazi yangu itakuwa rahisi,
je wanauza bei gani hzo generators ,pia wapo wapi ili niende kuona DEMO.

nimefanya google ya carmatec nimeona linki hizi tu
http://www.biogas-tanzania.org/index.php/tdbp/about/category/biogas_basics/

[URL="http://www.tanzania.go.tz/carmatec.htm"]http://www.tanzania.go.tz/carmatec.htm

[/URL]
 

NM
sijajua CARMATEC watauza kiasi gani pale watakapofanikisha lengo lao
 


Mkuu , mtambo wako unauwezo gani wa kuzalisha gesi kwa siku ?, unaweza kupata Kg ngapi per day based on the volume of the plant
 
Not more than 3.6 Milion hadi sasa zikiwa zimebaki kama 3 weeks kuvuna
Karibu uje tuvune mkuu!!!!
hivi vitunguu huchukua mda gani hadi kuvunwa??
garama za kukodi shamba zipoje??
kulima? kupanda?palizi? ulinzi? usafiri?bei kwa gunia moja?
nisaidie mkubwa. hii inaweza kua ajira mbadala.
 
Mkuu , mtambo wako unauwezo gani wa kuzalisha gesi kwa siku ?, unaweza kupata Kg ngapi per day based on the volume of the plant

mtungi wangu ni kama mapipa 3 so around lita 600 ujazo wa maji,sijaweza kujua unazalisha gas kiasi gani.bado nipo ktk majaribio
 
Mkuu , mtambo wako unauwezo gani wa kuzalisha gesi kwa siku ?, unaweza kupata Kg ngapi per day based on the volume of the plant

mkuu .... asante

nilikwenda kwa rafiki yangu anatumia bio gas kwa matumizi ya kupikia aliniambia moto wake ni mkali sana na unahitaji masufuria ambayo yana uzito mzuri au yale ambayo kitako chake ni shaba ...... optional niliona anatumia vyungu vya udongo mfinyanzi na vyakula vigumu kama maharage huiva fasta

congratulations NM
 

Nimefuatilia pale Ubungo kama ulivyo nielekeza, lile duka waliniambia wameishiwa, narudi mjini Dar week ijayo, nitajitahidi niku-pm ili kama kuna namna ya kuonana ili nipate zile mbegu nifanye hivyo. Bado natafuta Badizzo, ukiiona mahali inauzwa nijulishe. Kufanya kienyeji sitaki.
 
Mmenifurahisha nikitoka jikoni kupika ntarudi hapa ili mnipe nyepesi tufanye mambo.
 

Mkuu malila..
Nilipita Singida miezi kadhaaa.. Nimeona kama Mkuu wa Kaya anadumisha itikadi ya chama kwa kujenga barabara kwenda mbeya.. ila sijajua iko katika kiwa ngo kipi...ila kunapitika.

Mpakani mwa Moro na iringa(kabla ya Great Ruaha river).. kuna njia ya kwenda mpwapwa(unachepuka ukiwa watokea moro)... kuna kijiji kinaitwa Mgogozi.. kuna bonde pale Mjapani kalaza miundombinu ya umwagiliaji... kitunguu kinatoka pale si machezo... maadam u mwenyeji pande hizo pita huko si mbali sana toka njia kuu ya lami...

Kutokea mpwapwa(kupitia kijiji cha pwaga ) kuingia Kilosa kuna pahala panaitwa Lumuma(ni centre kubwa tu)...kutokea kilosa njia si mbaya ila makalavati yalikuwa yamechokachoka na sijui kama wamkarabati... kuna kitunguu kingi huku... waweza cheki ..
 

Nikushukuru sana kwa hili,
Mwaka huu nikijaliwa afya ya mwili na muda nitapita njia ya Singida/Mby. Safari ya kanda ya kati ni kwa ajili ya shamba la nyuki kubwa. Nikitoka Tbr nitapita Singida kuelekea Mby. Ratiba imejaa mpaka mwakani march,hii ya kanda ya kati imo ndani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…