Nilichojifunza kwenye hii thread ni kua kundi la wafanyakazi au wanetumwa na PSPF wameamua kuanzisha uzi ili kuwaponda LAPF inawezekana wamekutana kwenye uzi kwa kupanga au bahati mbaya maana kwenye uhalisia ni mwendawazimu tu anaeweza kuamini uongo kama huu na hii inatokana na ujio wa ajira mpya za waalimu ivyo sishangai hii mifuko inavyonyukana kwa kugeuza uongo kua ukweli na mbaya zaidi wa-Tanzania hatuna ABC za mifuko ya hifadhi ya jamii na wengi wakipata ajira ndio wanakutana na jambo hili akishtuka ashaingizwa mjini.
-PSPF wana mapungufu mengi sana na hata wanachotangaza pia kuna uongo na mengine hayawezi kufanyika kwa kada fulani.
-LAPF nao wana mapungufu mengi ingawa kwenye huu uzi yale ya msingi hayajazungumzwa.
-NSSF nao wana mapungufu yao ila kwenye ajira za serikali(Elimu,afya,kilimo nk)wao ni toothless dog.
Mifuko mingine haina afya ya kugombana na hao giants hapo juu ndio maana hawana hata muda wa kuja kwenye social networks kuleta uongo.
Angalizo ndugu zangu mnaotarajia kuingia kwenye ajira mpya anzeni kutafuta taarifa sahihi kuhusu mifuko ya hifadhi ya jamii kuna propaganda nyingi sana kwa sasa hasa baada ya serikali kubadili mfumo mzima na kuruhusu mifuko hii inyang'anyane wateja kupitia ubora wao.