LAPF na Clouds FM mbona mnadanganya umma?

LAPF na Clouds FM mbona mnadanganya umma?

Dr.Mbura

Senior Member
Joined
Jun 30, 2009
Posts
196
Reaction score
128
Kwa muda mrefu sasa katika kipindi cha Jahazi cha Clouds FM, Mfuko wa LAPF wanatoa tangazo linaloelezea kwamba wanatoa fao la kujikimu jambo ambalo sio kweli kabisa kwa maana wasimamizi wa Mifuko hawajatoa ruksa kwa LAPF kutoa fao hilo, huu ni uhuni wa hali ya juu kwa LAPF kudanganya umma na pia ni hatari kwa kituo makini kama Clouds FM chini ya Kamanda Ruge kutoa matangazo yanayopotosha kama hayo. Kama wameruhusiwa kutoa fao waoneshe barua kutoka kwa msimamizi wa Mifuko hiyo.

Pia kuna jamaa zangu huku Ipinda, huku Mbeya wamenieleza kuwa LAPF wamefulia kwa maana hivi sasa hawana tangazo katika TV yoyote ile, sasa hii maana yake wamejitoa katika ushindani au wameishiwa fedha. LAPF ni tatizo kubwa kwani wakiwa wananadi sera zao huwa wanatumia muda mwingi kuponda mifuko mingine, ushahidi ni hivi karibuni wakati wa usajili wa wafanyakazi wapya wa TRA, jamaa walipewa onyo na mdhibiti na mtumishi wao mmoja kafungiwa kujihusisha na masuala ya usajili.
 
Sasa hapa Ruge anakosa gani? Kaletewa tangazo anatangaze na hao LAPF kwa nini asitangaze? Kama unasema hilo sio tangazo la LAPF sasa nani analipia hilo tangazo?Mfano, mbona TV kibao zinatangaza Jay milion anatoa milion 100 kila siku wakati sio kweli, mbona huko husemi?,au umewaona LAPF pekee?
 
jephta
Mkuu, Ruge na Clouds hawana tatizo, ila inabidi wawe makini na ukweli wa matangazo, hilo la Jay million ni kama bahati nasibu fulani, lakini hili la LAPF ni jambo la maisha ya mtu.

Mtu anaweze kwenda huko kwa kuamini kinachotabgazwa kuwa ni kweli, ndio maana nasema kama LAPF wameruhusiwa kutoa Fao la kujikimu waweke hadharani barua kutoka kwa mdhibiti inayowaruhusu.

Hoja kubwa hapa ni kuwasaidia vijana wapya wanaoingia katika ajira sasa. Wewe nenda ofisi yoyote ya LAPF ukaulize kama wameruhusiwa kutoa mkopo huo.
 
Last edited by a moderator:
Nina brother angu alikuwa chuo cha kodi kwenye training ya TRA siku hiyo ni kweli huyo afisa wa LAPF kapigwa marufuku na SSRA kujihusisha na semina za wanachama. Alkuwa anasema full uongo. Huitaji kwenda ofisi ya LAPF kuthibitisha, wewe Google na kama humwamini Google angalia website yao hakuna hicho kitu. Hii mifuko midogo midogo imejaa uongo.
 
Nina brother angu alikuwa chuo cha kodi kwenye training ya TRA siku hiyo ni kweli huyo afisa wa LAPF kapigwa marufuku na SSRA kujihusisha na semina za wanachama. Alkuwa anasema full uongo. Huitaji kwenda ofisi ya LAPF kuthibitisha, wewe Google na kama humwamini Google angalia website yao hakuna hicho kitu. Hii mifuko midogo midogo imejaa uongo.

Mkuu tujulishe kirefu cha SSRA
 
Inaonekana huyu jamaa aliyeanzisha uzi huu anajua mambo ya katika hii Mifuko, sasa Ruge na team nzima ya Clouds, The Peoples station, kuweni makini na ikibidi hao jamaa wa Mifuko wawe wanawaonesha barua kutoka kwa msimamizi wao, au msimamizi ajitokeza na aseme ukweli juu ya LAPF na pia GEPF nao wanafanya kosa kama hilo la kutangaza vitu ambavyo hawajapatiwa ruksa na msimamizi wao. Clouds ni redio makini na wengi tunaikubali hivyo tusaidieni kwa kurusha matangazo ya ukweli.

Mtoto wangu alikwenda Makao Makuu ya LAPF baada ya kusajiunga nao na alipoulizia mkopo wa kujikimu maafisa wa LAPF hawakumpatia jawabu la maana na waliishia kusema na wao wanasikia tangazo redioni na hawajui kwanini wakubwa wao wanatoa tangazo hilo.
 
Clouds wako tayari kutangaza chochote ( isipokuwa habari za cdm ) wao wanaangalia hela tu , tena wala hawajali ilipotoka .
 
Kweli kabisa mtoa post,mi mwenyewe nimewasiliana nao lakn kuna ubabaishaji mkubwa, mara oh mpaka uthibitishwe kazini, nikawauliza nini maana ya fao la kujimu wakawa kimya!
 
Inaonekana huyu jamaa aliyeanzisha uzi huu anajua mambo ya katika hii Mifuko, sasa Ruge na team nzima ya Clouds The Peoples station kuweni makini na ikibidi hao jamaa jwa Mifuko wawe wanawaonesha barua kutoka kwa msimamizi wao, au msimamizi ajitokeza na aseme ukweli juu ya LAPF na pia GEPF nao wanafanya kosa kama hilo la kutangaza vitu ambavyo hawajapatiwa ruksa na msimamizi wao. Clouds ni redio makini na wengi tunaikubali hivyo tusaidieni kwa kurusha matangazo ya ukweli.

Mtoto wangu alikwenda Makao Makuu ya LAPF baada ya kusajiunga nao na alipoulizia mkopo wa kujikimu maafisa wa LAPF hawakumpatia jawabu la maana na waliishia kusema na wao wanasikia tangazo redioni na hawajui kwanini wakubwa wao wanatoa utangazo hilo.
unaweza kuchangia bila kuweka sifa za uongo na ukaelewela tu mkuu , unaposema clouds ni redio makini una maana gani ?
 
Mkuu tujulishe kirefu cha SSRA

Kirefu chake ni Social Security Regulatory Authority yaani Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini.

Nimeamua nikupe kwanza jibu ndo nikunange, inamaana umeshindwa hata ku-google upate kirefu chake na kazi zake?????!!!!!!!!!!!!!
Ndio maana sasa hata matangazo yanatolewa ili kuupotosha umma kwa kuwa hao jamaa wa LAPF walishajua watanzania walio wengi huwa hawajishughulishi kuutafuta ukweli hata kuwabana ili waache ku-uhadaa umma. kwani wanasema vitu vya uongo na kwenye website yao hakuna kitu kwani hata kwenye maandiko yao hakuna hicho wanachotangaza redioni.

Mimi binafsi niliposikia tangazo lao, nilijaribu kupita kwenye website yao hakukuwa na kitu, nikajaribu kuangalia kwenye facebook page yao hakuna kitu nikajaribu kuwauliza bado sikupata majibu...!!! Wale jamaa ukiwasikia wanavyojinadi unaweza kujikuta unavutiwa nao ila ni watupu balaa.
Ukitaka kuthibitisha utupu wao, angalia mambo yafuatayo:-
  1. Kwenye website yao hakuna Annual Reports ( taarifa za mwaka); ambazo kiuhalisia huonyesha utendaji wa Taasisi husika.
  2. Ukiangalia kwenye Annual reports za SSRA (Taarifa za mwaka za Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii) hawa jamaa wako mbali sana ya washindani wao, ila makelele wanayoyapiga utadhani wao ndo ma-giants. Mbona NSSF hawana kelele kama hawa jamaa??? Maana wanajua wanachofanya. Ila debe tupu ndo linapiga kelele balaa. Hata hivyo acha wadanganye maana wasipofanya hivyo hawatapata mtu, kwa kudanganya wanawapata wale ambao wanashikwa na huo uongo.
GNMhAtc4AIXuMAFLnCBC1yQ5X8APPGvmAmqiicAAAAASUVORK5CYII=



  1. source: SSRA Annual Report 2012/13
 
Hawa LAPF mwaka jana walikuwa wanaadhimisha miaka 70 toka kuanzishwa kwake. ukiangalia ukongwe wake na position yao kisekta hawakupaswa kudanganya umma, maana miaka 70 si haba ni umri wa mtu anayesubiri siku zake za mwisho wa uhai wake :lol::lol::lol::lol:
 
Hawa jamaa wa LAPF mwaka jana wakati tumeitwa kazini walirobby kwa Dada mmoja wa masjala hapa ofisini wakamkatia kidogodogo akawapa namba zetu za simu wakaanza kutupigia simu twende pale makao makuu kwao tukajisajili Jumamosi ambayo hata si siku ya kazi kwa serikali. HR mkuu akaidaka hiyo ishu akatupigia simu siku hiyohiyo kutwambia ni kinyume cha sheria walichotaka kutulaghai kwamba mifuko yote itatusajili siku moja tukiwa pale ofisini. Siku ya kusajiliwa walikuja wakaambulia mtu mmoja tu kati ya 48 tuliokuwa tumeitwa National Audit. Muwe makini na hawa jamaa nyie mnaotaka kujiunga na mifuko kwa kutegemea maneno ya kuambiwa na maafisa wao
 
LAPF ni genge la wahuni..nimebahatika kuhudhuria semina zao wao ni kuponda mifuko mingine hasa PSPF ukiwauliza kuhusu products zao ni usanii tu kama tangazo la John kupata 6 billioni hapo hapo na nyumba na gari(mkopo wa elimu)..mfuko bora ni PSPF kwa huduma na mafao bora..ingekuwa uwezo wangu ningejitoa huku ni lipo nijiunge na hawa jamaa (PSPF)
 
Ninyi PSPF Compliance Officers and Co. hamjielewi to the maximum. Yaani kuchafuana kote huku ni kwa sababu ya upcoming new teachers' registrations. Hizo tactics za kitoto sana. Jaribuni style nyingine coz kwa hii mmefeli. Sina interest na upande wowote ila muanzisha thread na wenzako mmeonesha ni jinsi gani hamjui kudeal na current market situation na badala yake mmeleta SIASA. Jipangeni tena!
 
Mifuko yotee tz haina umaana ila basi tu ssheria ya ajira inatubana. Mifuko yote m.a.v.i tu.....
 
LAPF ni genge la wahuni..nimebahatika kuhudhuria semina zao wao ni kuponda mifuko mingine hasa PSPF ukiwauliza kuhusu products zao ni usanii tu kama tangazo la John kupata 6 billioni hapo hapo na nyumba na gari(mkopo wa elimu)..mfuko bora ni PSPF kwa huduma na mafao bora..ingekuwa uwezo wangu ningejitoa huku ni lipo nijiunge na hawa jamaa (PSPF)

Hapo umesema ukweli mkuu.
Nilifanya uchunguzi kupitia SSRA pdf documents (available online) nika gundua nilifanya kosa kubwa mno!

Na nimewahi kuwa tumia email SSRA kutaka kuhama mfuko ndio wakanipa ufafanuzi kuwa haiwezekani!

Wakibadili tu sheria , Kesho nahamia PSPF.
Mm najuta kujiunga PPF.

Mfuko bora kuliko zote ni PSPF basiiiii!
 
Nina brother angu alikuwa chuo cha kodi kwenye training ya TRA siku hiyo ni kweli huyo afisa wa LAPF kapigwa marufuku na SSRA kujihusisha na semina za wanachama. Alkuwa anasema full uongo. Huitaji kwenda ofisi ya LAPF kuthibitisha, wewe Google na kama humwamini Google angalia website yao hakuna hicho kitu. Hii mifuko midogo midogo imejaa uongo.
hahaha!! huyo jamaa sintokaa nimsahau, ni muongo kinoma! enzi naajiriwa alikula sana vichwa. yani hawezi kufundisha bila kuiponda PSPF. anaitwa kagaruki, ana maneno utadhani mzaramo!
 
Back
Top Bottom