Landmarks za Tanzania na Majina ya Viongozi

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,544
19,404
Wakati Nyerere akiwa hai alikuwa hapendi jina lake kutumika katika landmarks mbalimbali. Uwanja wa Nelson Mandela kule Sumbawanga ulikuwa umejengwa kama uwanja wa Nyerere lakini alipokwenda kuufungua akaubadilisha jina na kuuita Nelson Mandela. Siku za hivi karibuni kumekuwa na landmarks nyingi sana zilizopewa majina ya Nyerere lakini naona kama kuna viongozi wanaosahauliwa kabisa.

Karume (Muasisi wa Zanzibar ya leo) zaidi ya kuwa na ule uwanja wa Karume ambao zamani ulikuwa uwanja wa Ilala, na mitaa midogomidogo na shule za msingi huko mikoani, sidhani kama kuna landamark kubwa ya kumuenzi. Kwa vile huyu alikuwa baharia, ningeshauri mojawapo ya bandari zetu iitwe Bandari ya Karume

Aboud Jumbe (huyu alikuwa makamu wa rais effective sana ila alikosea kidogo tu) hana landamark yoyote ya kumkumbuka. kwa vile yeye alitumia sehemu kubwa sana ya maisha yake Kigamboni, ningeshauri lile jimbo la kigamboni liitwe Kwa Jumbe

Mwinyi (Rais wa ruksa) amewekwa kwenye barabara ile iliyokuwa ikiitwa Bagamoyo road, na labda uwanja wa mpira wa mkoa wa Tabora tu. Hizo landmarks siyo kubwa sana kwa hadhi yake, na hivyo ningeshauri aongezewe kwenye list. Kwa vile yeye alihimiza sana biashara kwa kutumia falsafa ya Ruksa, ningeshauri jengo la wizara inayohusika na biashara hapo Dodoma liitwe Mwinyi House.

Angalu jina la Mkapa liko kwenye landamark kubwa mbili- daraja kubwa sana la Rufiji na stadium kubwa sana Tanzania; hakuna ulazima wa kuongeza landmark nyingine kwa jina la Mkapa.

Kikwete anaenziwa labda na taasisi ya Moyo ya Kikwete hapo Muhimbili, lakini nadhani anastahili kueziwa zaidi hasa katika jithada zake za kusambaza elimu nchini chini ya sera za sekondari za kata na UDOM. Ningeshauri kile chuo Kikuu cha Dodoma alichokiasisi yeye kiitwe Kikwete University of Dodoma (KUDOM).

Halafu tuwe na sheria inayoweka limit ya kutumia jina moja kwenye major landmarks; yaani jina moja lisitumike katika landmarks kubwa zaidi ya tatu au nne hivi. Mitaa midogo midogo pamoja majina ya vitongoji na shule za msingi siyo landmarks kubwa; hivyo havitaguswa na sheria hiyo.

Mengine yataongezewa kadri muda na matukio yanavyoruhusu
 
Ushauri mzuri katika Muktadha usiofaa ni dharau kufuta jina la mwanzo na kuweka jipya bora wasubirie Vijengwe vipya kisha wataandikwa majina yao hapo inavutia na kupendeza mfano Aboud Jumbe Stadium, Dodoma au Jakaya Kikwete International Airport, Msalato.
 
Ushauri mzuri katika Muktadha usiofaa ni dharau kufuta jina la mwanzo na kuweka jipya bora wasubirie Vijengwe vipya kisha wataandikwa majina yao hapo inavutia na kupendeza mfano Aboud Jumbe Stadium, Dodoma au Jakaya Kikwete International Airport, Msalato.
Nimekuelewa, ila sasa majina ambayo hayana historia yoyote kama University of Dodoma, au Kigamboni, au jengo jipya la wizara ya biashara si hiyo itakuwa ni fair game?
 
Nimekuelewa, ila sasa majina ambayo hayana historia yoyote kama University of Dodoma, au Kigamboni, au jengo jipya la wizara ya biashara si hiyo itakuwa ni fair game?
Hapo inaleta mashiko hata mimi naona Nyerere anatishwa zigo kila kitu ni yeye tuuuuuuuuu! utadhani hakuna wengine!
 
Hivi Magufuli akiita Ikulu ya chamwino kama Magufuli White house utafurahi. Maana ndio mjenzi na muendelezaji wa hizo unazozita Major landmarks.
 
Hapo inaleta mashiko hata mimi naona Nyerere anatishwa zigo kila kitu ni yeye tuuuuuuuuu! utadhani hakuna wengine!
Nyerere kawekwa kwenye landmarks kubwa zenye impact kubwa nyingi kupita kiasi na ndiyo maana nikafikiri kuwa tuwe na sheria inayoweka limit ya matumizi ya jina kwenye landmarks za kitaifa.

Halafu majina hayo yasibadilishwe kiholela; kwa mfano wa Uwanja wa ndege wa Houston ulikuwa unaitwa Kennedy Intentional Airport (kwa heshima ya JFK), lakini baadaye kwa sababu za kisiasa kwa madai ya kujiweka tofauti na JFK International Airport ya New York, ulibadilishwa kinyeji tu kwa kufuta jina la Kennedy hadi baadaye wakauita George HW Bush International Airport.

Kuwa na sheria nzuri inayosimamia majina ya landmarks kutazuia mitarafuku ya aina hiyo.
 
Kwahiyo hizo landmarks zitasaidia nini bibi yako kule kijijini.

Landmarks kubwa ya kiongozi yeyote wa Tanzania ni kufuata misingi ya uongozi na katiba. Hapo hatasahaulika miongoni mwa wananchi hata kizazi cha 12.
Hujachangia chochote kwenye mada bali umeleta hasira na hisia za kisisasa tu. Ni kama hujui kusoma mada na kuzielewa kabla ya kuzijibu; hii ni kwa post zako zote mbili ingawa nimekopi moja tu.
 
Hivi Magufuli akiita Ikulu ya chamwino kama Magufuli White house utafurahi. Maana ndio mjenzi na muendelezaji wa hizo unazozita Major landmarks.
Yeah iitwe Ikulu ya Magufuli
Itapendeza zaidi (sick)
 
sio lazima kuwaiga ingawaje kwa mtazamo wangu ni vizuri
Mali zimejengwa na umma sio vyema kuzipersonalize in names
Huyu mwamba aliona mbali sana
Hata mimi sioni umuhimu wala faida yoyote ya kuweka majina ya wanasiasa kwenye hizi mali za umma. Hivi ni wanasiasa peke yao waliochangia katika maendeleo tunayoyaona? Mbona wengine hatuoni wakienziwa? Angalao Magufuli alikumbuka kumuenzi mhandisi Mfugale kwa ile flyover ya Tazara, lakini je, hakuna wengine?
 
Sio lazima kuwaiga ingawaje kwa mtazamo wangu ni vizuri

Mali zimejengwa na umma sio vyema kuzipersonalize in names

Huyu mwamba aliona mbali sana
Ni vizuri umebainisha "kwa mtazamo wako" na ukakiri "sio lazima kuwaiga".

Kama "mali zimejengwa na umma" huoni kuwa ni umma huo huo unayo maamuzi ya kuwaenzi viongozi wao kama waliwafanyia mema?

Maoni yangu ni kwamba sio kila kiongozi anastahili kuenziwa. Ni muhimu pawepo na utaratibu unaofahamika utakaokuwa unafuatwa katika kuyafanya haya mambo, isiwe ni holela tu. Kushika ngazi ya uongozi pekee hata kama hukufanya jambo linalotambulika kuwa la muhimu kwa nchi haitoshi kuenziwa. Ni lazima pawepo na vigezo maalum vinavyotazamwa ili kukidhi matakwa ya heshima hiyo.

Kuhusu watu wanaopewa heshima hiyo, sio lazima wawe viongozi wa kisiasa peke yao. Kama kuna mTanzania amefanya jambo la kuiletea nchi heshima, ni wajibu hata yeye atambuliwe kwa mchango wake bila kujali yupo kwenye siasa au la. Kama ni mwanasayansi aliyebuni njia nzuri za kuwasaidia wakulima wasipoteze zaidi ya asilimia arobaini ya mazao yao, basi mtu huyo au kundi hilo linafaa kuenziwa kwa kupewa heshima hiyo.

Sikubaliani na wazo, kwa mfano kubadili jina la Cho Kikuu cha Dar es Salaam au Dodoma kwa sababu tu za kubandika jina la mtu. Hivi vilivyopo tayari visibadilishwe majina. Majina yapewe kwa hivyo vipya vitakavyojengwa. Ni sababu za kipekee kabisa zinazoweza kubadili jina muhimu na kwa taasisi muhimu kama Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mtu huyo kama kavumbua njia za haraka za kuyabadilisha maisha ya waTanzania na kuwa yenye neema, huyu pengine atastahili kufikiriwa kwa heshima kama hiyo. Na hili haliji kwa mtu mmoja tu, tena mwanasiasa kuamka asubuhi na kutangaza. Inatakiwa ajengewe hoja ili kuonyesha sifa zinazomfanya aenziwe kiasi cha kutaka kubadili jina muhimu lililozoeleka kwa jamii nzima na kimataifa.

Kuhusu "kupokonywa/kubadilishwa" - kama kiongozi atabainika kuwa alifanya maovu, kwa nini jina lake lisiondolewe, mradi tu usiwe msukumo wa kisiasa tu unaofanya hilo lifanyike?
 
Wakati Nyerere akiwa hai alikuwa hapendi jina lake kutumika katika landamarks mbalimbali. Uwanja Nelson Mandela kule Mpanda ulikuwa umejengwa kama uwanja wa Nyerere lakini alipokwenda kuufungua akaubadilisha jina na kuuita Nelson Mandela. Siku za hivi karibuni kumekuwa na landmarks nyingi sana zilizopewa majina ya Nyerere lakini naona kama kuna viongozi wanaosahauliwa kabisa.

Karume (Muasisi wa Zanzibar ya leo) zaidi ya kuwa na ule uwanja wa Karume ambao zamani ulikuwa uwanja wa Ilala, na mitaa midogomidogo na shule za msingi huko mikoani, sidhani kama kuna landamark kubwa ya kumuenzi. Kwa vile huyu alikuwa baharia, ningeshauri mojawapo ya bandari zetu iitwe Bandari ya Karume

Aboud Jumbe (huyu alikuwa makamu wa rais effective sana ila alikosea kidogo tu) hana landamark yoyote ya kumkumbuka. kwa vile yeye alitumia sehemu kubwa sana ya maisha yake Kigamboni, ningeshauri lile jimbo la kigamboni liitwe Kwa Jumbe

Mwinyi (Rais wa ruksa) amewekwa kwenye barabara ile iliyokuwa ikiitwa Bagamoyo road, na labda uwanja wa mpira wa mkoa wa Tabora tu. Hizo landmarks siyo kubwa sana kwa hadhi yake, na hivyo ningeshauri aongezewe kwenye list. Kwa vile yeye alihimiza sana biashara kwa kutumia falsafa ya Ruksa, ningeshauri jengo la wizara inayohusika na biashara hapo Dodoma liitwe Mwinyi House.

Angalu jina la Mkapa liko kwenye landamark kubwa mbili- daraja kubwa sana la Rufiji na stadium kubwa sana Tanzania; hakuna ulazima wa kuongeza landmark nyingine kwa jina la Mkapa.

Kikwete anaenziwa labda na taasisi ya Moyo ya Kikwete hapo Muhimbili, lakini nadhani anastahili kueziwa zaidi hasa katika jithada zake za kusambaza elimu nchini chini ya sera za sekondari za kata na UDOM. Ningeshauri kile chuo Kikuu cha Dodoma alichokiasisi yeye kiitwe Kikwete University of Dodoma (KUDOM).

Halafu tuwe na sheria inayoweka limit ya kutumia jina moja kwenye major landmarks; yaani jina moja lisitumike katika landmarks kubwa zaidi ya tatu au nne hivi. Mitaa midogo midogo pamoja majina ya vitongoji na shule za msingi siyo landmarks kubwa; hivyo havitaguswa na sheria hiyo.

Mengine yataongezewa kadri muda na matukio yanavyoruhusu
Well said Kichuguu, siku hizi watu wakiraka kujustify white elephants projects wanazipa jina la Nyerere

Tuna wazee wetu wa kale kabisa akina Mkwawa, Kinjekitile, Machifu wengi tu akiba Rumanyika, Songea, Marealle, Abushiri na wengineo wengi huoni wakienziwa, kila kitu kizuri kinaitwa jinala Nyerere.

1. uwanja wa ndege wa JKN
2. Bwawa la umeme la JKN
3.Ukumbi wa mikutano wa JKN
4. Uwanja wa Kambarage
5. Chuo cha Nyerere (Kivukoni)
6. Daraja la Nyerere (Kigamboni)
7. Barabara ya Nyerere(Pugu road)
8. Campus ya Mwalimu Nyerere (UDSM)
...
..
Na mengine mengi

Ina maana sisi kama Taifa tuna uhaba wa heroes wa kuenzi majina yao?
 
Sikubaliani na wazo, kwa mfano kubadili jina la Cho Kikuu cha Dar es Salaam au Dodoma kwa sababu tu za kubandika jina la mtu. Hivi vilivyopo tayari visibadilishwe majina. Majina yapewe kwa hivyo vipya vitakavyojengwa. Ni sababu za kipekee kabisa zinazoweza kubadili jina muhimu na kwa taasisi muhimu kama Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Mtu huyo kama kavumbua njia za haraka za kuyabadilisha maisha ya waTanzania na kuwa yenye neema, huyu pengine atastahili kufikiriwa kwa heshima kama hiyo. Na hili haliji kwa mtu mmoja tu, tena mwanasiasa kuamka asubuhi na kutangaza. Inatakiwa ajengewe hoja ili kuonyesha sifa zinazomfanya aenziwe kiasi cha kutaka kubadili jina muhimu lililozoeleka kwa jamii nzima na kimataifa.

Chuo Kikuu cha Dr es Salaam siyo vizuri kukibadilisha jina kwa kuwa hilo limeshatambuliwa kwa zaidi ya miaka 50 sasa, lakini sioni ubaya kubadilisha jina la Chuo cha Dodoma ambacho bado ni kipya tu. Chuo cha Sokoine Morogoro kilipohamishwa kutoka Kitivo cha Kilimo cha Chuo Kikuu cha Dar es salaam, kilikuwa kinaitwa Chuo Kikuu cha Kilimo Mororogoro, baada ya kifo cha Sokoine kikabadilishwa jina na kupewa jina hili la Sokoine. Juzi juzi tu hata huko Ujerumani wambedilisha jina la mtaaa kutoka Von Wismann kuwa Lucy Lameck, kwa hiyo kubadilisha majina siyo jambo la ajabu, mradi kuwe na utaratibu mzuri wa kufanya hivyo bila kuathiri historia.
 
Huyu wa sasa landmark yake ni Hapa Kazi na Tanzania ya Maendeleo ya Miundombinu. Kwa dunia ya sasa na ijayo Rais JPM anatupeleka Kuzuri tu.
 
Well said Kichuguu, siku hizi watu wakiraka kujustify white elephants projects wanazipa jina la Nyerere

Tuna wazee wetu wa kale kabisa akina Mkwawa, Kinjekitile, Machifu wengi tu akiba Rumanyika, Songea, Marealle, Abushiri na wengineo wengi huoni wakienziwa, kila kitu kizuri kinaitwa jinala Nyerere.

1. uwanja wa ndege wa JKN
2. Bwawa la umeme la JKN
3.Ukumbi wa mikutano wa JKN
4. Uwanja wa Kambarage
5. Chuo cha Nyerere (Kivukoni)
6. Daraja la Nyerere (Kigamboni)
7. Barabara ya Nyerere(Pugu road)
8. Campus ya Mwalimu Nyerere (UDSM)
...
..
Na mengine mengi

Ina maana sisi kama Taifa tuna uhaba wa heroes wa kuenzi majina yao?
Hiyo ni kufuru ya wanasiasa kuenziana kwa kodi zetu ili wakati ukifika na yeye aenziwe ingawa atakuwa hajafanyia jamii chochote cha maana. Ulaya wanaenziwa watu walioifanyia jamii kwa uwezo wao au gharama zao kama vile waandishi, wanasayansi, wavumbuzi, wagunduzi hata wanajeshi waliochangia ushindi muhimu wa nchi yao, wasanii kama composers kama Beethoven ambao nyimbo zao mpaka leo bado zinapendwa karne mbili baadaye. Ulaya ya Mashariki walienzi sana wanasiasa hasa wa Urusi kama akina Lenin, Stalin ingawa wakati wa uongozi wao watu wengi sana waliuawa na mali zao kutaifishwa lakini leo masanamu yao yameporomoshwa, majina kwenye mitaa au majengo yamefutwa. Reginald Mengi amefanya mengi sana kwa jamii kwa gharama zake ikiwa ni pamoja na IPP Media Ingawa baada ya kifo inaunga mkono juhudi, kwa hiyo anasitahili kuenziwa kuliko mwanasiasa yeyote nchini ambaye kwa gharama zetu hakuweza kusaidia wananchi. Mengi anasitahili kuenziwa kuliko Magufuli na watangulizi!
 
Back
Top Bottom