Mleta mada, mimi siamini kuwa machozi yake(yao) yatanipa laana, kwa sababu;
1. Mbele za M/Mungu tulifanya dhambi ya uzinzi, ngono na uchafu ambao Mungu hapendi.
2. Tulitenda dhambi ya uongo wote (mimi nilimdanganya, nae kadanganya kwa Mungu)
Hayo yaliyokupata ni sehemu ya maisha tu (ups and downs) na wala haihusiani na kumdanganya au kuchezea mwili na hisia zake. Mwanamke wa kweli hachezewi mwili coz anaitambua thamani ya mwili wake, the worst you can do ni kuchezea hisia. Mwanamke/mwanaume anayechezewa mwili ni mjinga mjinga tu..
Katika masuala ya mahusiano mwanaume ndio muanzilishi....ni agharabu sana kwa mwanamke kumtongoza mwanaume ingawa hutokea....
Katika kushawishi huko unaweza ukamtoa mwanamke katika hali fulani hivi ya kutokukuamini na hatimaye akakuamini na hatimaye mkawa kwenye mahusiano.....
Wakati mwingine huyo mwanamke anaweza kuwa alikuwa kwenye mahusiano na mtu mwingine wenye mipango ya muda mrefu lakini kuringana na sera zako za kuvutia hatimaye ukambadilisha maamuzi na kuingia kwenye imaya yako.....kumbuka hata hapo kwenye kumtoa mwanamke kwenye imaya ya mtu mwingine tayari umeshaumiza nafsi ya mtu mwingine.....
Hadi kufikia hapo mwanamke huyu atakuwa na matumaini makubwa sana kwako....mapenzi yake na yote atayahamishia kwako akiamini kuwa wewe ndiye yule aliyeletewa na Bwana.....wakati mwingine huwa anakuulizia masuala ya kuona na wewe unamuambia kuwa dear mbona mapema sana....
Kwa kuwa lengo lako ni kumvua tu nguo na kumuacha unaanza harakati za kuomba ngono kwa kushawishi kwa aina mbali mbali na yeye lazima atakupa akiamini kuwa ni moja wapo ya njia ya kudumisha penzi lenu ili mfike mbali.....mtoto wa kike anajiachia kwako kwa raha zote hakuna sehemu ya mwili wake usiyoijua kwa jinsi alivyojiachia kwako akiamini kabisa kuwa wewe ndiye mumewe.....
Siku zinavyoende kwa kuwa umeshapata ulichokuwa unakitaka mapenzi yanapungua....unaanza kumuona kama kero fulani hivi....yaani kama anajipendekeza fulani hivi kwako.....hali hiyo inaendelea mpaka mwanamke anaanza kuwa na wasi wasi kuhusu hali ya uhusiano wenu....unaamzungusha na hatimaye unaamua kumuambia live kuwa huna mpango nae....
Hebu jiweke katika nafasi ya mwanamke je ungejisikiaje...
Hakika ni jambo lenye kukera na kusononeka maaana katika muda huo labda alipuuzia mahitaji ya watu wenye upendo wa kweli huku akiishi katika uongo wako....
Ni jambo ambalo kwa mwanadamu mwenye akili ya kawiada hangependa limtokee kwani ni jambo kuumiza moyo kama sio kuuchoma moyo....
Yale manung'uniko, masononeko na machozi yasiyokauka muda wote kila akifikiria jinsi ulivyozikatisha ndoto zake nyingi tu kwa ajili ya uongo wako ndivyo vinavyokuletea mikosi kwenye maisha yako.....
Ndio maana hata nyakati hizi utafutaji ridhiki umekuwa ni mgumu sana kwa vijana wa kiume kwa sababu ya madhambi makubwa sana waliyowatendea mabinti wa watu.....maana kuna mabinti wengine walijitunza sana lakini wakashawishika kwa ulaghai wao.....
Na mambo ambayo ni ngumu kuyathibitisha kama ambavyo ilivyo kwa nguvu za giza lakini yapo na watu wanateseka kwa ajili ya hayo....
Hujawahi kuona anakuwa kama kachanganyikiwa baaada ya kuachika na mtu ampendaye....wengine huenda mbali mpaka kunywa sumu na kuutoa uhai wako mtukufu kwa ajili ya ulaghai wako tu......sasa hapo kuna baraka gani kwenye maisha yako ikiwa wewe ndiyo chanzo cha mahangaiko na vifo vya mabinti wengi sana mtaani......??