Laana ya mwanamke

Laana ya mwanamke

Laana wanawake tu?,mbona sie wanaume tukitoa laana haifiki,tutaachwa sana
Hata sisi huwa tuna laana....ila hapa nimeongelea wanawake kwa kuwa ndio wahanga wakubwa sana kwenye mahusiano kwa kuwa vijana wanatumia muda mwingi kumuaminisha mwanamke kuwa yeye ni wake wa milele ili hali kwenye nafsi yake haipo hivyo.....ndipo laana zinapoanzia hapo....
 
Habari za wakati huu ndugu na marafiki wapendwa wa Jamii Forums....
Ni siku nyingine tena tulivu ikiambatana na manyunyu ya hapa na hapa pale kwa sisi wakazi wa Dar......

Leo ningependa kuwashirikisha katika jambo muhimu sana ndugu zangu ambalo hata mimi binafsi ninaweza kuwa shahidi kabisa....

Kuna kipindi nyakati za nyuma kidogo nilitokea kumtamani binti fulani hivi ambaye tulikuwa tukiishi nae karibu na nilipokuwa nikiishi mimi...kusema ukweli huyu mimi sikumpenda isipokuww nilikuwa namuhitaji kwa ajili ya kukidhi matakwa yangu ya kimwili, kutokana na ushawishi mkubwa nilifanikiwa kumnasa yule binti na tukaanza kushiriki ngono huku yeye akijua kuwa mimi ndiye mumewe mtarajiwa.....yule binti alikuwa ni binti mwenye kujitegemea maana alikuwa anafanya kazi kwenye kampuni fulani kubwa hivi ya kigeni kwa hiyo suala kipato alikuwa tatizo kwake....alichokuwa anakihataji ni mapenzi au mume ambaye aliamini kuwa ameshampata.....

Baada ya kukidhi haja zangu nikaanza kumkwepa kwa maana nilimuona kama ni kero vile kwangu.....yule dada nilimpa wakati mgumu sana kwa mabadiliko yale....na alikuwa akilia mbele yangu mara kwa mara akinisihi nisimuache lakini mimi sikuelewa lolote lile....yule mwanamke akakata tamaa na akaamua kuachana na mimi lakini alinitamkia maneno mazito sana kuhusu maisha yangu....ambayo nilianza kuyaelewa maana yake baada ya mwezi kupita tangu kukata mawasiliano naye.......

Niliona ghafla mambo yangu yanabadilika na kuwa mabaya kabisa....biashara zangu nyingi sana zilikwama mpaka nikawa nakosa hata hela ya kula......ile hali ikanishtua sana maana haikuwa kawaida ikabidi kuahangaika katika mambo ya kiswahili ndipo wataalamu waliponifunulia kuwa kuna mtu ana kinyongo na wewe kwa hiyo unatakiwa ukamiombe msamaha maana ndio njia pekee ya wewe kuondokana na mikosi hiyo maana hakuna aliyeniroga.....

Ikanibidi kwa unyonge kabisa nijipendekeze kwa yule binti na kuanza kujenga naye ukaribu upya na kuomba misamaha mingi sana....

Baada ya muda nikaona mambo yanaanza kubadilika na kuwa kama kawaida.....

N:B Dhumuni la mimi kushare kisa hiki ni kuwaasa vijana kuwa kama mwanamke huna mipango naye ya muda mrefu basi usimpotezee muda wake bure maana utamuacha na sononeko ambalo litakuletea mikosi kwenye maisha yako.....wapo vijana wasomi wanaohangaika kutafuta kazi takribani miaka kumi....wapo vijana wanaojaribu kuanzisha biashara zao lakini huwa zinakufa.....wapo vijana wanaofukuzwa kazi katika mazingira ambayo hata yeye hawayaelewi...hizi ni moja ya athari za watu waliokuwa na vinyongo na wewe.....

Stuka kijana
Very true . I'm a witness on this.. Thanks..
 
dah! you remind me of something ujue.... ila karma has everybody's address believe or not its just a matter time.. we better keep our circles positive!
Ni vitu ambavyo vinaumiza sana mioyo na baadhi yao walishajitoa uhai....na waliobahatika kuyavumilia ndio wanaoweka vinyongo nafsini mwao.....
 
Hakuna kitu kinauma kama kupotezewa Muda, Ex wangu hadi leo pamoja na kuwa na kazi nzuri maisha yake hayaeleweki, kwenye mahusiano ndo usiseme, nabado napiga goti kwa Mungu siku atakayorudi kuomba msamaha kwakunikosea ndo amwachilie.

I can feel you on this.. It hurts so much... But let him go so God can use you more ..Thanks..
 
Ni kweli usemayo,hakuna kitu kinauma kama kupotezewa muda jamani, umejitunza na kuwakataa wengine wenye nia afu mtu anakuacha hewani gafla,uwiii.... Mungu niepushie isinitokee tena
Yalishakukuta mpwa.....????
 
This Shit Applies To Both.
Ndio kiongozi....wapo wanawake wanaokumbana na mikosi kwa kuwakimbia au kuwasaliti wenzi wao.....lakini wahanga wengi wa matukio haya ni wanawake....kwa kuwa sisi wanaume ndio tunawajenga kuwa hivyo....na mwishowe tunakwenda kinyume na matarajio yao....
 
Pole kwa yaliyokukuta.....i hope ulisamehe....
Trust me dear it wasnt easy thing to do.. Until God said something to me .. But I still could not do it on my own , so I had to surrender complete unto God so He could fix me all over again...So I thank God through Jesus Christ ... Amen... But that person, Ooh Boy, alikutana na Moto WA Yesu until today anajuta .. I feel so sorry kwake but well you reap for what you sowed.. I'm surprise some people don't take it this serious .. The time its coming for them too... Wait and watch ... Thanks..
 
Trust me dear it wasnt easy thing to do.. Until God said something to me .. But I still could not do it on my own , so I had to surrender complete unto God so He could fix me all over again...So I thank God through Jesus Christ ... Amen... But that person, Ooh Boy, alikutana na Moto WA Yesu until today anajuta .. I feel so sorry kwake but well you reap for what you sowed.. I'm surprise some people don't take it this serious .. The time its coming for them too... Wait and watch ... Thanks..
Am feel sorry for you....dear....it really hurt....
Thanks god you have made it.....
 
Hii inatokea sana tu jiepushe na udanganyifu na kufanya hila kwa binadamu mwenzako. Ufanyapo hila unajifungia Baraka zako mwenyewe. Utaenda kwa waganga wa kienyeji na kukesha makanisani lakini husipoiondoa hila uliyoifanya awali hutakaa ufanikiwe. Jichunguze wengi source ya matatizo tuliyonayo tumejiletea wenyewe. Una mtoto nje unamwacha binti wa watu unaenda kuoa, mbaya hukumbuki hata kulea mtoto, kuna mawili hata ukizaa tena hao watoto mafanikio yao ni shida au unaweza husipate mtoto tena. Pia waweza husifanikiwe katika maisha yako yote. Mikosi itakuandama tu. Lazima ulie Zaidi ya yule uliyemliza. Utachangua mwenyewe kujitafakari upya uendavyo. Kama ulishajichanganya kaombe msamaha na beba jukumu uliloacha awali.
 
Yalishakukuta mpwa.....????
Hayo yalinikuta 2013 mpwa.... Hii mambo ishia tu kusikia kwa jirani lakini kwako usiombe.

Kupitia hilo nimejifunza ukiamua kumsahau aliekuumiza na kufurahia maisha inawezekana kabisa.

Nilimpenda mno na sikutegemea kama ningeweza kumsahau ila yote hayo kwasasa yamebaki historia tu... Jamaa bado hajaoa na alivokua nyuma ni tofauti na sasa,na hapo ndipo ninakubaliana na Uzi wako huu....
 
Ni kweli usemayo,hakuna kitu kinauma kama kupotezewa muda jamani, umejitunza na kuwakataa wengine wenye nia afu mtu anakuacha hewani gafla,uwiii.... Mungu niepushie isinitokee tena
akiamungu vale; sitakuacha hewani!!
 
Ni kweli usemayo,hakuna kitu kinauma kama kupotezewa muda jamani, umejitunza na kuwakataa wengine wenye nia afu mtu anakuacha hewani gafla,uwiii.... Mungu niepushie isinitokee tena

Very true.. There is nothing I hate very hate kama my time to be wasted ... Its better for that person to come clean Early .. It doesn't matter how much it hurts to tell the Truth but its better than pretend .. And then nakataa wenye nia njema.. Haki inauma sana .. So dear tuko wengi tuliotoka huko ... Acha nao wakutane na moto WA dhuluma on what they did to us... Thanks..
 
Hakuna kitu cha namna hiyo. Ni uoga wenu ukipatwa na tatizo unatafuta majibu mepesi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom