Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Ebwana ndiyo,

siasa za mbeya kweli tamu saaana.

kama huu mwongozo ndiyo anautegemea kwa ajili ya kumng'oa Mwakyembe, atakuwa amechemsha vibaya mno.

Halafu huu mbona sio mwongozo! haya ni majungu tu mbona hakuna chochote cha maana!

Kama hii ndiyo hekima ya Mwakipesile basi Mbeya bado safari ndefu sana kupiga hatua za kimaendeleo, ndio maana hata miradi mikubwa na mizuri kama uwanja wa ndege wa Songwe upo upo tu kama kambi ya wakimbizi.

Halafu kusema kweli hata kama mwakalinga ni mwenzetu hapa JF na tunahitaji kumuunga mkono ili afanikiwe kuingia mjengoni, sharti ajiepushe na watu wachafu.

Hakuna namna yeyote ataweza kusimamia maslahi ya watu wa kyela na Tanzania kwa ujumla kama nyuma yake ana support ya mafisadi.

Kila siku hapa tunamnyoshea vidole JK ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi kwa kuwa ndio waliombeba hadi kuingia magogoni, kwahiyo hatuwezi kutegemea lolote jipya toka kwa Mwakalinga kama anabebwa na fisadiz.

Tatizo wabaya wake ndio wanamwandalia waraka na kuuza hapa jf harafu wanajifanya ndio waraka wake.

Kwanini kuchafuana lakini? wapigane kwa hoja kama kweli wanaona uchungu wananchi wanavyoteseka.
 
Kama huu ndio mpango wa kushindana kisiasa wa Mwakalinga, yaani kulinganisha watu na wanyama, kukashifu wenzake, basi wazee wa Kyela watabidi watafute pamba za kuziba masikio.

Mambo mengine nii too much kwa watu wengi wanaopenda ustaarabu kwenye masuala ya kisiasa. Katika hili, mnaenda low zaidi ya viwango vya kawaida vya siasa. Na huu pia ni ufisadi.

Suleiman Daudi,

Pole sana Mkuu kama una shida na uandishi huu.

Nimeamua nikijibu kwa kuona kuwa wee utakuwa mgeni bado na hapa JF kuna kitu kinaitwa KUSOMA NDANI YA MISTARI. Ntaomba sana tena sana uanze kuzoea uandishi wangu. Huwa mara nyingi ninachanganya mchele na Pumba. Mwakalinga ananifahamu kwa hilo na huwa hapati shida na huu mwendo wangu.

Mara nyingi nikiona mtu kaandika UPUPU, basi na mie huwa namjibu UPUPU. Hamna haja ya kumuelewesha mtu anayeanza kwa kusema NASIKIA na baadaye anaaanza kushutumu.

Haya maneno yako ya mwisho kuwa WAZEE wa Kyela watafute pamba, kwa leo nayaacha bila comment kwa sababu tu naona wee bado mgeni. Na ndiyo maana nakuandikia ujumbe wa heshima namna hii.

Kwa Taarifa yako mie naitwa Mwana Itimba wa Sikonge. Mwakalinga George yuko UK anakofanya kazi na ambaye nafikiri umesoma kuwa yuko safarini leo kwenda UK kutoka Tanzania kwa likizo. Ukifuatilia vizuri makala ya Mwakalinga kugombea UBUNGE na jinsi ilivyoshabikiwa hiyo makala, utagundua UMAARUFU na busara za jamaa. Vinginevyo, watu wasingekaliana kooni namna hiyo.

Kama ndiyo ningelikuwa mie hapa Mnyamwezi nataka kugombea na Mwakyembe jimbo la Kyela, hata kama mafisadi wangelikuwa wamenipa pesa, unafikiri Genge la wapinzani lingelikuwa kubwa namna hiyo? Kama kuna mtu kasababisha watu wajadili jumbe nyingi namna hiyo kwa siku moja, basi lazima ujuwe kuwa jamaa kajiandaa vizuri. Labda kwa taarifa yako lazima ujuwe kuwa wapambe fulani walikaa na kuamua kumtuma mtu aende hadi UK kwenda kumuomba jamaa asigombee ubunge. Kama angelikuwa mtu wa kaundika pumba kama zangu, basi asingeliwanyima jamaa usingizi.

Nafikiri umenielewa na utaendelea kufaidi hizi habari ambazo wengine milele tunaziandika nusu siriasi na nusu joki.
 
Tatizo wabaya wake ndio wanamwandalia waraka na kuuza hapa jf harafu wanajifanya ndio waraka wake.

Kwanini kuchafuana lakini? wapigane kwa hoja kama kweli wanaona uchungu wananchi wanavyoteseka.

ha ha h aha ha

Yaani sina mbavu, inafurahisha sana kuona MkamaP akilalamika kuwa watu wanachafuana.

jamani jamani jamani kwa nini kuchafuana? umeyaona haya leo?
 
Inakuwa ngumu kuchuja kama umeshalamba laptop na kuna ahadi ya kupata nyingine

Mfumwa nimempa leo asubuhi LAPUTOPU mbili. Yeye na jirani yake Mwafrika. Usione analia lia hapa maana hajajua kuwa nimem-PIMP his LAPUTOPU. kama wee Mpita njia hilo una shida nalo, matawi ya miti kibaooo, unaweza kwenda kujining'iniza. Ila uende mbali ili usituharibie hewa.
Pia wee kama hujapata LAPUTOPU basi ni-PM nikuandikishe kwenye listi ya masikini wa JF. Mafisadi wamenipa MIHELA hiyooo na hadi sijui niifanyie nini. Tanzania kweli Tambaraleeee....
 
Ebwana ndiyo,

siasa za mbeya kweli tamu saaana.

kama huu mwongozo ndiyo anautegemea kwa ajili ya kumng'oa Mwakyembe, atakuwa amechemsha vibaya mno.

Halafu huu mbona sio mwongozo! haya ni majungu tu mbona hakuna chochote cha maana!

Kama hii ndiyo hekima ya Mwakipesile basi Mbeya bado safari ndefu sana kupiga hatua za kimaendeleo, ndio maana hata miradi mikubwa na mizuri kama uwanja wa ndege wa Songwe upo upo tu kama kambi ya wakimbizi.

Halafu kusema kweli hata kama mwakalinga ni mwenzetu hapa JF na tunahitaji kumuunga mkono ili afanikiwe kuingia mjengoni, sharti ajiepushe na watu wachafu.

Hakuna namna yeyote ataweza kusimamia maslahi ya watu wa kyela na Tanzania kwa ujumla kama nyuma yake ana support ya mafisadi.

Kila siku hapa tunamnyoshea vidole JK ameshindwa kuwachukulia hatua mafisadi kwa kuwa ndio waliombeba hadi kuingia magogoni, kwahiyo hatuwezi kutegemea lolote jipya toka kwa Mwakalinga kama anabebwa na fisadiz.

Vipi Hapo!!!!

Mtu anajitolea kupeleka Radio ya jamii, chuo cha mawasiliano huria kwenye majengo yake, ajira, misaada mashuleni, kusaidia wafiwa n.k, kwa kutumia kipato chake baado tu anaoeneka hayupo.
Kumbe Mwakalinga ana nguvu sana na ni hatari 2010.

Kama vigogo wote wanaweza kuwa nyuma yake na kumfadhiri noti kibao kwa ajili ya kampeni zake basi anakubalika kweli, na atafanikiwa lengo lake.

Ni mapema mno kuufikia uchaguzi, lakini nikiangalia upepo wa mambo yanavyokwenda Kyela, nguvu ya Mwakalinga ni ya ajabu sana, maana amekubaliaka haraka sana. Leo uwezi mimi kunidanganya eti afahamiki Kyela wakati ana miradi kibao na amesaidia mambo mengi hata wadogo zetu wanafaidiaka na misaada yake, leo ndio unaleta porojo hizo, thubutu atapigiwa debe tu hata kama mtaongea wimbo uliozoeleka wa mafisadi.

Ni nani anayefahamika Kyela kati ya aliyejikita Kyela na anasiyekuwepo Kyela kwa maana kuwa hakuna chochote alichofanya Kyela.

Mtu asikudanganye, laiti kama Mwakalinga angekuwa mchafu, Mwakyembe ninaye mfahamu mimi angekuwa wa kwanza kwenda kwenye vyombo vya habari kutangaza, lakini imeonekana kuwa Mwakalinga ni safi na anafanya mambo yake kwa ajili ya watu wa Kyela.

Pesa ina nguvu yake, angalia kwenye chaguzi za jumuiya, watu ambao Mwakyembe alikuwa akiwapigia debe walianguka vibaya mno na akaishia kulalama kuwa Rostom Aziz kamwaga 20M kumwangusha, basi ategemee kwenye ubunge atamwaga 600M na kumpiga ngwala.

K. Gwamaka
 
kweli mwakyembe kiboko mpaka wameamua kumtafutia blogger kutoka ulaya aje kushindana nae
inaonekana jamaa aliposema yeye ni muanzilishi wa JF mafisadi wakaona huyu ndio anafaa kabisa kuchuana na mwakyembe

binafsi kama ningekuwa napiga kura ningempigia mwakyembe na ni kwa sababu moja tu, amesimama mbele ya hawa wanyanyanyasaji wawili EL na RA, yaani ukiwakosea hawa ndani ya ccm ni kama vile gharika....
yani hawa jamaa wawili (EL & RA) wamewachafua sana watu kwa mfano SAS, magufuli, mwandosya na kumnyanyasa nape na wengine wengi (na bado puppet kibao JF wanawashabikia kwa hela ya soda) du!

anyway kuna ma puppet wa kutosha kule bungeni and we dont need anymore
mwakalinga another puppet in the making
Mmmmm!!!!
Mwenzetu unatoka jimbo gani? Bahati nzuri hauna kura yako Kyela.
Siku hizi unaweza kugombea popote sio lazima Kyela, nakuomba mchukue mpeleke jimboni kwako ukampigie debe, maana kwetu Kyela hatutaki mtu ambaye hajui matatizo ya wana Kyela, hatutaki na nasema hatutaki.
kgwamaka
 
Jamani, hivi vyote si private investmements zake? Kwani anawagawia profit anayopata? Je, mnaingia bure kwenye huo ukumbi au kupewa special discounts kwa wana Kyela kwenye hiyo Supermarket yake kubwa? Vyote hivi amefanya kwanza kwa faida yake binafsi, period. The rest ni by-product ambayo inavyoonekana inaweza kulipa zaidi kuliko the main products kwa mawazo kama haya.
.

Chief.
Vipi kuhusu employment?.Au wewe haulewi hicho?.
Serikali inalia kila siku kuhusu ajira .sasa hizo investment utafanya kazi wewe? au wewe ni chief wa nini.Walio ajiliwa ni wana kyela bwana chief.
 
Duh, ndugu yangu. Kumiliki duka au redio ndo qualifications za Ubunge? Toka lini biashara ya mtu ikawa mali ya wote? Ama kweli, Wanyakyusa mmekwisha![/SIZE]
.

Fataki. Ajira kwa vijana.
Ndiyo maana yake
 
Yaani timu Mwakalinga imejipanga kweli kwenye message.

Kusoma na kuishi ulaya, kugawa laptop, kumiliki hotel na radio, kumiliki supermarket kubwa sana, na kubwa kwa yote ...... kutoa matusi kwa wale wapinzani wao.

Bahati nzuri (good luck) huko muendako. Nawaombea mfike salama.

Msg sent
 
Vipi Hapo!!!!
Mtu anajitolea kupeleka Radio ya jamii, chuo cha mawasiliano huria kwenye majengo yake, ajira, misaada mashuleni, kusaidia wafiwa n.k, kwa kutumia kipato chake baado tu anaoeneka hayupo.

Weka mambo kwenye pasipektivu yake. Hayo ya radio, hoteli, chuo cha mawasiliano na mengine yote yanayosemwa hapa ni biashara binafsi za Mwakalinga na wala sio msaada. Kutoa misaada mashuleni ni mapenzi yake binafsi na sio lazima yalipwe kwa ubunge - kinyume chake itakuwa takrima.

Kumbe Mwakalinga ana nguvu sana na ni hatari 2010.
Kama vigogo wote wanaweza kuwa nyuma yake na kumfadhiri noti kibao kwa ajili ya kampeni zake basi anakubalika kweli, na atafanikiwa lengo lake.
Ni mapema mno kuufikia uchaguzi, lakini nikiangalia upepo wa mambo yanavyokwenda Kyela, nguvu ya Mwakalinga ni ya ajabu sana, maana amekubaliaka haraka sana.

Mwenzako anajaribu kweli kuwakwepa hao vigogo - Lowasa, Rostam Azizi, Mwakipesile, Ridhiwani Kikwete na wengine kwa vile ni mafisadi lakini wewe unaona kama hii ni faida?!

Leo uwezi mimi kunidanganya eti afahamiki Kyela wakati ana miradi kibao na amesaidia mambo mengi hata wadogo zetu wanafaidiaka na misaada yake, leo ndio unaleta porojo hizo, thubutu atapigiwa debe tu hata kama mtaongea wimbo uliozoeleka wa mafisadi.
Ni nani anayefahamika Kyela kati ya aliyejikita Kyela na anasiyekuwepo Kyela kwa maana kuwa hakuna chochote alichofanya Kyela.

Kufahamika Kyela sio tija au sababu pekee ya kumfanya apewe kura.
Mtu asikudanganye, laiti kama Mwakalinga angekuwa mchafu, Mwakyembe ninaye mfahamu mimi angekuwa wa kwanza kwenda kwenye vyombo vya habari kutangaza, lakini imeonekana kuwa Mwakalinga ni safi na anafanya mambo yake kwa ajili ya watu wa Kyela.
Pesa ina nguvu yake, angalia kwenye chaguzi za jumuiya, watu ambao Mwakyembe alikuwa akiwapigia debe walianguka vibaya mno na akaishia kulalama kuwa Rostom Aziz kamwaga 20M kumwangusha, basi ategemee kwenye ubunge atamwaga 600M na kumpiga ngwala.
kgwamaka

Kwa maelezo ya pale juu kuwa Mwakalinga anafadhiliwa na vigogo yana pingana na haya ya kusema kuwa Mwakalinga ni msafi. Na kama Mwakalinga atapokea hizo milioni 600 toka kwa Rostam (ambazo ni za wizi) basi inabidi Kyela yote iambiwe vyanzo vya pesa za Mwakalinga.
 
.

Chief.
Vipi kuhusu employment?.Au wewe haulewi hicho?.
Serikali inalia kila siku kuhusu ajira .sasa hizo investment utafanya kazi wewe? au wewe ni chief wa nini.Walio ajiliwa ni wana kyela bwana chief.

Mwakalinga katoa ajira ngapi kwa wana Kyela?
 
Sisi inatusaidia nini kama huyo Mwakalinga wako anaondoka kwenda London,wangapi wanaenda london bwana wewe.
Acha ushamba wa kuwapaisha watu,bwana kama unampenda sana huyo Mwakalinga KAMPIKIE CHAI

Huyo sio kwamba ni mpenzi wa Mwakalinga,yeye ni lile kundi lingine,endelea kufatiliayeye kwa makini utajua yeye nani,ameanza kuleta siasa zake za uchawi toka YANGA, ameanza kupuliza kwanza baadaye atakuja na mbomu....Wamepoteza tayari mwelekeo
 
staili yako ya uandishi kwamba ,wewe mwandishi na blah blah kibao wengi tulijua ndo huko unaelekea.

Yani mbinu inayotumiwa sasa nikujaribu kumuunganisha Mwakalinga na kambi za watu waliopoteza dira halisi ili mpate kumchafua Mwakalinga.

Huyu lowasa kuhusu eti Mwakalinga yuko naye beneti ni uzushi tu amabo ulianza baada ya mtego wa kwanza kufeli kwamba Mwakalinga alikuwa tayari kelya akifanya kampeni na Invisible alipokuja na jibu la kwamba jamaa yuko Arusha basi wenye roho zao za korosho ndo wakadakia eti ameenda kwa lowasa tangu hapo ndio wavumishi wa mambo waliposhikilia.

Pigeni kampeni safi na siza kuchafuna ,mtu anayediriki kumchafua mwenzako ili ajipatie madaraka hakika hana nia njema kabisa na taifa ,mtu mwenye nia njema huwezi lazimisha uongozi ili uwaongoze. Kumchafua mwenzako ni dalili tosha ya dhamila ya mhusika husika.
mwak huu mpk mnadata.......sio invisible ni maxence aliesema.....huo mgao wa EL mtadata mwaka huu maana jama ni mbabe usipofanya kazi aliokutuma lazima akufaanyie..
 
Weka mambo kwenye pasipektivu yake. Hayo ya radio, hoteli, chuo cha mawasiliano na mengine yote yanayosemwa hapa ni biashara binafsi za Mwakalinga na wala sio msaada. Kutoa misaada mashuleni ni mapenzi yake binafsi na sio lazima yalipwe kwa ubunge - kinyume chake itakuwa takrima.



Mwenzako anajaribu kweli kuwakwepa hao vigogo - Lowasa, Rostam Azizi, Mwakipesile, Ridhiwani Kikwete na wengine kwa vile ni mafisadi lakini wewe unaona kama hii ni faida?!



Kufahamika Kyela sio tija au sababu pekee ya kumfanya apewe kura.


Kwa maelezo ya pale juu kuwa Mwakalinga anafadhiliwa na vigogo yana pingana na haya ya kusema kuwa Mwakalinga ni msafi. Na kama Mwakalinga atapokea hizo milioni 600 toka kwa Rostam (ambazo ni za wizi) basi inabidi Kyela yote iambiwe vyanzo vya pesa za Mwakalinga.
Hata zikiwa biashara za chura, provided ziko Kyela na zinatoa ajira kwa wanaKyela huyo ni mkombozi wa wanaKyela, kuliko kuwa na mpiga gita wa nyimbo zilizojaa pambio za mafuta.
Kgwamaka
 
mwak huu mpk mnadata.......sio invisible ni maxence aliesema.....huo mgao wa EL mtadata mwaka huu maana jama ni mbabe usipofanya kazi aliokutuma lazima akufaanyie..

Ha ha hahaha ... Yo Yo sikuwezi.

Nakwambia watapewa amri za kimorani hadi washangae. Cheki hii...

Lowasa - hifi kire kichamaa kipya kiko wapi, mbona sikioni aisee
Morani1 - unasema kipi posi -- kile cha porandi
Lowasa - ndiyo subayi, kire cha Porand
Morani1 - Nasikia kuwa kiripanda cheti ya moto na kurudi usunguni.
Lowasa ---- kireteni hapa mara moja subayi, lasima kipate mikuki kumi
Lowasa (huku akifyonza kwa hasira) -- pesa yangu yote karasi (kwisaaa)

.......
 
Ha ha hahaha ... Yo Yo sikuwezi.

Nakwambia watapewa amri za kimorani hadi washangae. Cheki hii...

Lowasa - hifi kire kichamaa kipya kiko wapi, mbona sikioni aisee
Morani1 - unasema kipi posi -- kile cha porandi
Lowasa - ndiyo subayi, kire cha Porand
Morani1 - Nasikia kuwa kiripanda cheti ya moto na kurudi usunguni.
Lowasa ---- kireteni hapa mara moja subayi, lasima kipate mikuki kumi
Lowasa (huku akifyonza kwa hasira) -- pesa yangu yote karasi (kwisaaa)

.......

Kumbe uchaguzi ujao ntashinda. Yaani Mpambe wa Mwakyembe anaandika UPUUZI wa namna hiyo? Sasa Morani nao wamekukosea nini?

Leo nimekuona nusura utolewe ngeo na Mnigeria? Unatumia LAPUTOPU yake na akija bibi yake pia unataka UMTUMIE? Mwafika bana, hofyoooo!!! Wee mtu MZIMA kabisa (jando halijatembea) unashindwa kununua laputopu yako hadi unadandia za watu? CAMAAN.

Lazima ujuwe mwakani kibaua kinaota Mbawa. Mwakyembe hakupi tena kazi. Utake usitake, mwakani mie ni mbunge ya KYELA. Kama hutapendezwa, kunywa maji ya mto wa Msimbazi.....
 
Mwongozo wa Mkuu wa Mkoa wa uendeshaji kampeni ya Mwakalinga, ambao kila mpambe wa Mwakipesile anao na sisi akina yakhe tunao, ni huu hapa:

"1. George ameanza kusaidia Kyela tokea alipokuwa mlimani kama mwanafunzi, wakati hakuwa na uwezo kabisa. Yeye na wenzake waliungana pamoja kuchangia walimu wanafunzi ili waje wafundishe shule za secondary Kyela wakati wa likizo. Wakati huo Mwakyembe alikuwa mlimani, alikuwa hana msaada, hata mikutano alikuwa hahudhurii na alikuwa anajulikana kama anatoka Rungwe.


2. Toka George aanze kazi kila mwaka hutumia mshahara wa mwezi mmoja kusaidia jamii mbalimbali Kyela zikiwemo shule, wanafunzi ambao wamekwama na matatizo mengine kama vile kuwasaidia walimu kudai mafao yao pamoja na wafiwa kufuatilia malipo ya waume zao wanao waliofariki.

3. Mpaka sasa George kishasaidia karibu kila kata na anaendelea kusaidia kadri mungu anavyompa uwezo.

4. George anapinga ugomvi na migawanyiko ya watu na anataka kuisaidia Kyela ili iweze kupiga hatua mbele kwenye maendeleo kuliko hata wilaya kama Rungwe ambayo haina utajiri kama Kyela. Baada ya uchaguzi anataka kuonana na watu wa makundi yote na kuwakutanisha pamoja kwa faida ya Kyela.

5. George amesoma, ametembea dunia, anajuana na watu wengi ambao watakuwa muhimu sana huko mbeleni wakati akitekeleza mipango yake ya kuiendeleza Kyela. Kwa mfano Kyela radio FM imetolewa na UN kupitia shirika la elimu, sayansi na utamaduni. Na sasa yuko mbioni kuanzisha tawi la Open University Kyela ili kila mwana Kyela anayetaka aweze kusoma mpaka uwezo wake utakapoishia.

6. Huko nyuma alipoona wana Kyela wanahangaika kwenye mikopo aliweza kuwashawishi PRIDE kutoka Tukuyu ili waje Kyela. Na mpaka leo PRIDE wanashukuru maana wamegundua soko la Kyela ni kubwa. Tunaamini wana Kyela wengi wamefaidika.Mpango wa baadaye ni kuungana na wana Kyela wengine kufungua bank ya wana Kyela ili wananchi waweze kujipatia mikopo na ushauri wa uhakika kwa faida yao .

7. George Ulaya ana kazi ya maana sana na ambayo kipato chake ni zaidi ya mara mbili ya ubunge.familia ilikuwa inataka aendelee kukaa huko na kuachana na siasa za majungu huku nyumbani. Lakini George ameamua kurudi baada ya usanii wa Mheshimiwa na amekubali pato lake litashuka sana lakini yuko tayari kuwatumikia wana Kyela kwa moyo wote kama ambavyo ameweza kuitumikia familia yake kwa muda mfupi na mpaka kufanikiwa kufungua kampuni kama KBC kwa kutumia pesa zake kwa miaka 10 tu ambayo amekuwa kazini.

8. George anataka kuzibadili shule na hospitali hasa ya Kyela ili ziwe za kisasa, kununua na kuomba vifaa kama magari ya wagonjwa na mashine za kutibia kutoka sehemu mbalimbali. Pia kuleta watu wa kujitolea kutoka nje kusaidia shule na hospitali ili ziwe na ubora na kupunguza vifo vya watoto na wanawake kama ilivyo sasa. George anataka kukomesha mambo ya kwenda Igogwe na Tukuyu kutibiwa, badala yake hospitali zetu zitakuwa bora hata zaidi.

9. George hataki ukubwa na muda wote anaishi maisha ya kawaida. Hahitaji
Shangingi na pesa za shangingi akipata anataka zitumike kununua magari ya wagonjwa kwa faidi ya jamii yote.

10.George amesaidia kuwaamsha vijana wa Kyela kwa kuwaletea ukumbi wa kisasa, kuona mipira kwenye TV kubwa na mpaka sasa vijana wa Kyela hawababaishwi tena na vijana wengine toka Dar. Huko mbele anataka kuimarisha huduma zingine mbalimbali kwa faida ya Kyela.

11. Kupitia KBC vijana wote wamekuwa wakipata vibarua KBC na kupata mahitaji yao muhimu. Lengo huko mbele ni kuimarisha ajira kwa vijana. Kwamba huko mbele anataka kusimamia mafunzo ya VETA na kuwapa vijana misaada ili wakajiajiri mijini, kuwasaidia vijana wanaotaka kujiunga na jeshi. Atakuwa wa kwamza kwenda kumpigia magoti Mwamunyange ili vijana zaidi waende jeshini, pia atasaidia vijana kujiunga na jeshi la polisi.

12.George anataka kurudi kwasababu ana uchungu na Kyela, anataka kusaidia Kyela akiwa bado kijana na nguvu zake badala ya kurudi uzeeni. Anataka wote waliosoma na kubaki Dar wawe na uhusiano na nyumbani, wajenge nyumbani, wasaidie nyumbani, matokeo yake vijana watapata kazi huku nyumbani. Waambie George anataka kuwasiliana na kila mwana Kyela ili kuwashawishi wafanye kitu chochote nyumbani ikiwemo kuwasaidia wazazi wao na wadogo zao.

13. Mheshimiwa hana uchungu na Kyela na alikuja Kyela baada ya kuwaogopa wale maprofesa kule Rungwe. Ndio maana muda wote anashinda Tukuyu.

14. Mheshimiwa anapoteza muda na Wachaga ambao wameendelea zamani huku kwake hakuna kitu, vijana wanahangaika bila ajira. Kwamba yeye Mwakyembe anachotaka ni uwaziri ndio maana kila sehemu anazunguka na waandishi wa habari ili wakuze jina lake.

15. Hata vita vya ufisadi na Richmond , data nyingi alipewa na akina George kutoka kwenye mitandao yao . mitandao ndio iliibua Richmond . Mwanzoni bunge walipuuza lakini watu wa mitandao wakazidisha nguvu na kutoa scandal zao mpaka bunge lilipokubali kuchunguza. Waambie George ni mdau mzuri kwenye mitandao ya Watanzania inayopinga ufisadi na viongozi wabaovu.

16. Mheshimiwa amekuwa mbunge miaka 9. ikiwa ni pamoja na bunge la East Afrika lakini hakuna alichofanya Kyela na badala yake kajenga jumba kubwa Dar ambali ni la anasa kuliko majumba ya mafisadi. Kwamba hata nyumba ya kwao Ikolo yeye hakai, ile alijenga ili tu kuwadanganya wana Kyela kwamba anatoka Kyela.


17. Mheshimiwa anakosana na kila mtu, hata George hakutaka kugombea sasa lakini Mheshimiwa anatumia ubunge wake kuikwamisha hata KBC. Alitumia akina Kifukwe kukwamisha CRDB kufungua branch KBC, alijaribu kuzuia radio isije Kyela na anapinga vijana wanaotaka kuendeleza Kyela.

18. Badala ya kuwapelekea wananchi maendeleo yeye anapeleka disco ili wacheze na kuambukizana ukimwi zaidi.

19. Anapenda makuu, daraja lililojengwa na jeshi tayari analiita daraja la kwake. Nyerere aliongoza miaka yote bila hata nyumba moja kuitwa jina lake. Angalau hilo daraja angeita daraja la Mwamunyanga.George hataki kabisa kutukuza jina lake na badala yake anatukuza Kyela, ndio maana kwenye kila kitu ameweka Kyela badala ya jina lake.

20. Mheshimiwa ameshindwa hata kushughulikia suala la maji na mabomba ya Wascandinavia badala ya kushughulikia ili yatoke maji, yeye ameyaacha na anashinda Dar, hajui hata Kyela kuna tatizo gani. Wapambe zake kazi kupeleka umbea tu."

Sasa wapi imeandikwa kuwa NIMENUNUA REDIO FM? Watu bana.

Wapi imeandikwa mie ni OWNER wa Jamiiforum, Watu bana,

Wapi imeandikwa kuwa nitagawa LAPUTOPU, watu bana.

Wapi imeandikwa ..... subirini nikakojoe........
 
Kumbe uchaguzi ujao ntashinda. Yaani Mpambe wa Mwakyembe anaandika UPUUZI wa namna hiyo? Sasa Morani nao wamekukosea nini?

Leo nimekuona nusura utolewe ngeo na Mnigeria? Unatumia LAPUTOPU yake na akija bibi yake pia unataka UMTUMIE? Mwafika bana, hofyoooo!!! Wee mtu MZIMA kabisa (jando halijatembea) unashindwa kununua laputopu yako hadi unadandia za watu? CAMAAN.

Lazima ujuwe mwakani kibaua kinaota Mbawa. Mwakyembe hakupi tena kazi. Utake usitake, mwakani mie ni mbunge ya KYELA. Kama hutapendezwa, kunywa maji ya mto wa Msimbazi.....

Ha ha ha ha nilijua hiyo itakugusa. Ha ha ha ha mbavu zangu!

Zilianza story kibao hapa - Ulaya miaka 18, laptop, garagasa, nk. Sasa hivi kimya- fyyyyyuuuu mmefyata.

Mlijiandaaa na story kibao -- ohh Mwakalinga kaanzisha JF -- Invisible kawaaibisha. Mara ohh yeye ndiye mfadhili wa JF --- imevutwa thread ya Sikonge (hana uhusiano wowote na Mwakalinga) akiomba watu wachangie JF na ikaonyesha kuwa Mwakalinga hata hakaribii asilimia kiduchu ya michango yote.

Mtoto wa Kikwete kaona kampeni imebuma katoka ndukiiiiiii --- yule sasa hivi anaganga makovu.

Masikini kambi ya Mwakalinga. Mlidhani mtapata njia rahisi hapa JF. Mlikuja mmejiandaa kumbe si vya kutosha. Ushauri rahisi. Rudini mjipange upya kwa maana safari si rahisi kama mlivyokadiria.

*****back kwenye mazungumzo ya Lowasa na Morani wenzake**

Lowasa - tufanye sasa nini subayi.
Morani2 - tutafute mwingine posi kwani huyu wa porandi hawesi kasi

-----

Lowasa (baaada ya kimyaa kizito) ---- horrrrooooo horrrrrooooooo

itaendelea
 
Ha ha ha ha nilijua hiyo itakugusa. Ha ha ha ha mbavu zangu!

Zilianza story kibao hapa - Ulaya miaka 18, laptop, garagasa, nk. Sasa hivi kimya- fyyyyyuuuu mmefyata.

Mlijiandaaa na story kibao -- ohh Mwakalinga kaanzisha JF -- Invisible kawaaibisha. Mara ohh yeye ndiye mfadhili wa JF --- imevutwa thread ya Sikonge (hana uhusiano wowote na Mwakalinga) akiomba watu wachangie JF na ikaonyesha kuwa Mwakalinga hata hakaribii asilimia kiduchu ya michango yote.

Mtoto wa Kikwete kaona kampeni imebuma katoka ndukiiiiiii --- yule sasa hivi anaganga makovu.

Masikini kambi ya Mwakalinga. Mlidhani mtapata njia rahisi hapa JF. Mlikuja mmejiandaa kumbe si vya kutosha. Ushauri rahisi. Rudini mjipange upya kwa maana safari si rahisi kama mlivyokadiria.

*****back kwenye mazungumzo ya Lowasa na Morani wenzake**

Lowasa - tufanye sasa nini subayi.
Morani2 - tutafute mwingine posi kwani huyu wa porandi hawesi kasi

-----

Lowasa (baaada ya kimyaa kizito) ---- horrrrooooo horrrrrooooooo

itaendelea

Hahahaaa Mnigeria alikukunja shati akakunyenyua juu hadi ukawa unasimamia vidole utadhani Michael Jackson anacheza wimbo wa Thriller.

Nikaona Mkuu macho yamekutoka kaa mjusi kabanwa na Mlango. Ilibidi Ngosha nitumie ubabe wangu kukuokoa na Kipigo cha Mboboo huyo.

Next time you must be careful na vya watu. Anza kujitegemea na usikalie visenti vya Mwakyembe, maana utakufa masikini, Mwafika weee!!!!
 
Back
Top Bottom