Je, haya ya huyu Diwani wa Kyela 2020 yanaweza kumkuta "mama" 2025?

mtwa mkulu

JF-Expert Member
Sep 11, 2013
8,098
9,994
Alikuwepo diwani maarufu kwa jina la Kanyanyila aliyeingia madarakani mwaka 2015 kuongoza kata yake ya Lusungo. Ilikuwa ni jambo la kushangaza kwa mwanamke kushikilia madaraka makubwa ya kisiasa namna hiyo hapo Lusungo na ukanda wa Ndamba kwa ujumla.

Utawala wake ulikuwa wenye kuudhi watu. Alikuwa mbabe sana na hakuwa msikivu. Hakuweza kuwapa huduma wananchi wake. Alijijengea utiisho sana kwa madaraka aliyopewa na mwishoni mwa madaraka yake alikumbwa na tuhuma za mauaji ya mtu asiye na hatia.

Muda wote wa utawala wake alizungukwa na chawa ambao muda wote walimwambia kuwa wako pamoja nae maana anaupiga mwingi. Chawa hawa walimwambia mama kanyanyila kuwa atapita miaka mitano mingine kwani anakubalika sana kwa yote anayo yafanya pale lusungo.

Ulifika muda wa kura za maoni ndani ya chama 2020, wajumbe ndani ya chama kwa umoja wao walipiga kura za hasira dhidi ya mama kanyanyila... aliangushwa akashika nafasi ya tatu.
Kamati ya siasa ya chama ngazi za juu ilitumia turufu yake kumpitisha mama huyu kuwa mgombea udiwani kupitia chama Tawala chenye mizizi yake kwa miaka mingi pale lusungo.

Wananchi walighafilishwa sana na jambo hilo.. ghadhabu hii ilikuwa kubwa kuliko kura za maoni.

Siku ya uchaguzi mkuu wote walipiga kura za udiwani kwa upande wa CDM huku wakimpa kura Raisi magufuli kwa upande wa uraisi. Kama Kanyanyila aliokota kura basi ni za familia yake tu.

Wilaya nzima ya Kyela kata moja tuu ya Lusungo ilipotelea upinzani.

Je, Watanzania wanaweza kufanya maamuzi magumu juu ya utawala huu mwaka 2025?
 
Siku ya uchaguzi mkuu wote walipiga kura za udiwani kwa upande wa CDM huku wakimpa kura Raisi magufuli kwa upande wa uraisi. Kama Kanyanyila aliokota kura basi ni za familia yake tu.

Wilaya nzima ya Kyela kata moja tuu ya Lusungo ilipotelea upinzani.
Yaani Pamoja na Wizi wa Magu bado hii Kata ilirudi kwa Mpinzani ili Mungu kumkomesha Kanyanyila?
 
Kwa rais Samia Hilo halitatokea kwasabb Tume MTU (siyo tume huru) itamtangaza hata kama hajashinda.
 
Alikuwepo diwani maarufu kwa jina la Kanyanyila aliyeingia madarakani mwaka 2015 kuongoza kata yake ya Lusungo. Ilikuwa ni jambo la kushangaza kwa mwanamke kushikilia madaraka makubwa ya kisiasa namna hiyo hapo Lusungo na ukanda wa Ndamba kwa ujumla.

Utawala wake ulikuwa wenye kuudhi watu. Alikuwa mbabe sana na hakuwa msikivu. Hakuweza kuwapa huduma wananchi wake. Alijijengea utiisho sana kwa madaraka aliyopewa na mwishoni mwa madaraka yake alikumbwa na tuhuma za mauaji ya mtu asiye na hatia.

Muda wote wa utawala wake alizungukwa na chawa ambao muda wote walimwambia kuwa wako pamoja nae maana anaupiga mwingi. Chawa hawa walimwambia mama kanyanyila kuwa atapita miaka mitano mingine kwani anakubalika sana kwa yote anayo yafanya pale lusungo.

Ulifika muda wa kura za maoni ndani ya chama 2020, wajumbe ndani ya chama kwa umoja wao walipiga kura za hasira dhidi ya mama kanyanyila... aliangushwa akashika nafasi ya tatu.
Kamati ya siasa ya chama ngazi za juu ilitumia turufu yake kumpitisha mama huyu kuwa mgombea udiwani kupitia chama Tawala chenye mizizi yake kwa miaka mingi pale lusungo.

Wananchi walighafilishwa sana na jambo hilo.. ghadhabu hii ilikuwa kubwa kuliko kura za maoni.

Siku ya uchaguzi mkuu wote walipiga kura za udiwani kwa upande wa CDM huku wakimpa kura Raisi magufuli kwa upande wa uraisi. Kama Kanyanyila aliokota kura basi ni za familia yake tu.

Wilaya nzima ya Kyela kata moja tuu ya Lusungo ilipotelea upinzani.

Je, Watanzania wanaweza kufanya maamuzi magumu juu ya utawala huu mwaka 2025?
hata kama si 2025 ipo siku ambayo sio mbali sana kutoka sasa itakuwa kama hivyo.
 
Alikuwepo diwani maarufu kwa jina la Kanyanyila aliyeingia madarakani mwaka 2015 kuongoza kata yake ya Lusungo. Ilikuwa ni jambo la kushangaza kwa mwanamke kushikilia madaraka makubwa ya kisiasa namna hiyo hapo Lusungo na ukanda wa Ndamba kwa ujumla.

Utawala wake ulikuwa wenye kuudhi watu. Alikuwa mbabe sana na hakuwa msikivu. Hakuweza kuwapa huduma wananchi wake. Alijijengea utiisho sana kwa madaraka aliyopewa na mwishoni mwa madaraka yake alikumbwa na tuhuma za mauaji ya mtu asiye na hatia.

Muda wote wa utawala wake alizungukwa na chawa ambao muda wote walimwambia kuwa wako pamoja nae maana anaupiga mwingi. Chawa hawa walimwambia mama kanyanyila kuwa atapita miaka mitano mingine kwani anakubalika sana kwa yote anayo yafanya pale lusungo.

Ulifika muda wa kura za maoni ndani ya chama 2020, wajumbe ndani ya chama kwa umoja wao walipiga kura za hasira dhidi ya mama kanyanyila... aliangushwa akashika nafasi ya tatu.
Kamati ya siasa ya chama ngazi za juu ilitumia turufu yake kumpitisha mama huyu kuwa mgombea udiwani kupitia chama Tawala chenye mizizi yake kwa miaka mingi pale lusungo.

Wananchi walighafilishwa sana na jambo hilo.. ghadhabu hii ilikuwa kubwa kuliko kura za maoni.

Siku ya uchaguzi mkuu wote walipiga kura za udiwani kwa upande wa CDM huku wakimpa kura Raisi magufuli kwa upande wa uraisi. Kama Kanyanyila aliokota kura basi ni za familia yake tu.

Wilaya nzima ya Kyela kata moja tuu ya Lusungo ilipotelea upinzani.

Je, Watanzania wanaweza kufanya maamuzi magumu juu ya utawala huu mwaka 2025?
Ikitokea kura za rais Tanzania nzima zikapungua sana upande wa Chanzo Cha Matatizo, kuna hatari mawakala wakalishwa sumu ili kura ziibwe
 
I suggest, kama ni hivyo CCM Zanzibar ingalikua ishang'oka since 1995.

Na Middle East viongozi wote wangelikua jela.
CCM zanzibar ina exist kwasababu ya udhaifu uliopo bara... ukitaka kujua nguvu ya watu kumbuka Arab Spring 2011
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom