Pfizer
JF-Expert Member
- Mar 25, 2021
- 726
- 953
Timu ya Wawakilishi kutoka Taasisi ya Keep A Child Alive ya Msanii maarufu wa Marekani, Alicia Keys, imewasili nchini Tanzania kupitia uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl.Julius K. Nyerere tayari kwa ajili ya kwenda Wilayani Kwimba Mkoani kwenye uzinduzi wa jengo la kisasa la kuhudumia Watoto njiti lililojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba.
Timu hiyo baada ya kuwasili Airport imeelekea hadi Hospitali ya Amana na kuwajulia hali Wagonjwa kisha kuwapa zawadi pamoja na kujionea mazingira ya huduma kwa Watoto njiti ambapo wameahidi kuendelea kutoa misaada mbalimbali ikiwemo ya miundombinu na vifaa tiba.
Kiongozi wa Wawakilishi hao, Antonio Ruiz-Gimenez, ameelezea historia yake fupi ya namna alivyopata Mtoto njiti na hivyo anaguswa kuwasaidia Watoto njiti nchini Tanzania akishirikiana na Serikali na Wadau mbalimbali wakiwemo Doris Mollel Foundation (DMF).
Jengo la kuhudumia Watoto njiti lenye viwango vya Kimataifa limejengwa Kwimba na Taasisi ya Doris Mollel (@dorismollelfoundation) chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Doris Mollel (@dorismollel) na linatarajiwa kuzinduliwa leo February 28,2026.
Timu hiyo baada ya kuwasili Airport imeelekea hadi Hospitali ya Amana na kuwajulia hali Wagonjwa kisha kuwapa zawadi pamoja na kujionea mazingira ya huduma kwa Watoto njiti ambapo wameahidi kuendelea kutoa misaada mbalimbali ikiwemo ya miundombinu na vifaa tiba.
Kiongozi wa Wawakilishi hao, Antonio Ruiz-Gimenez, ameelezea historia yake fupi ya namna alivyopata Mtoto njiti na hivyo anaguswa kuwasaidia Watoto njiti nchini Tanzania akishirikiana na Serikali na Wadau mbalimbali wakiwemo Doris Mollel Foundation (DMF).
Jengo la kuhudumia Watoto njiti lenye viwango vya Kimataifa limejengwa Kwimba na Taasisi ya Doris Mollel (@dorismollelfoundation) chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Doris Mollel (@dorismollel) na linatarajiwa kuzinduliwa leo February 28,2026.