Kwenu Sektetarieti ya ajira (PSRS), je, uwajibikaji na uwazi ni changamoto kwenu? Sio kipaumbele kwenu?

Orosso

JF-Expert Member
Aug 3, 2022
931
2,262
Habari zenu wana jamvi.
Nimeshuka jamvini na swali kama linavojieleza katika kichwa cha habari.

Lengo kuu ni kuona namna gani michango ya wanajamvi inaweza saidia kufikisha ujumbe kwa wahusika na kufanya marekebisho katika dosari zinazojitokeza kila siku katika kutimiza majukum yao.

Tunafaham kuwa moja ya majukumu ya msingi ya sekretarieti ya ajira (PSRS) ni kusimamia na kuratibu mchakato mzima wa upatikanaji wa ajira kwa sekta ya umma. Kutimiza lengo hili, uwajibikaji na uwazi vinahitajika kwa kiwango cha juu mnoo kuhakikisha kunakuwepo na usawa kwa washindani katika kupigania fursa hizo.

Kwa muda mrefu kumekuwepo na malalamiko yanayoashiria kupungua kwa kiwango cha uwajibikaji na uwazi hasa linapokuja swala la watu kuitwa kazini. Malalamiko haya yanazidi kushika kasi hasa kipindi hiki ambacho kunashuhudiwa msululu wa saili zinazoendelea kujaza nafasi zilizo wazi serikalini.

Tumeshuhudia pia, matangazo ya waliofanikiwa kuitwa kuhudhuria sahili hizo kwa maana, sahili za mchujo na mahojiano yakitoka kupitia tovuti ya utumishi.

Changamoto inakuja panapohitajika uwazi zaidi namna inayofaa kutangaza majina ya walioshinda sahili hizo na hivyo kuitwa kazini. Hapa pamekua na changamoto hasa kwa siku hizi za karibuni.

Kwa siku hizi za karibuni tumeshuhudia taasisi za kiserikali kupitia tovuti zao, zikiwa za kwanza kutangaza majina ya watu walioshinda sahili na kuitwa kazini, je, kwanini katika hatua hii ya tatu ndo taasisi hizi ziwe zinatangulia kutangaza washindi na kuita watu kazinin? Ipi nafasi ya sekretarieti ya ajira katika kuwajibika na uwazi katika hatua hii muhimu katika mchakato wa kutoa ajira sekta ya umma nchini?

Kuthibitisha hili, Chuo kikuu huria kilitangulia kutoa majina ya walioshinda sahili na kuita watu kazini katika tovuti yake ya chuo, ndipo baadae sekretarieti ya ajira ikafuatia. Hali kama hiyo ikajirudia katika tovuti ya chuo kikuu Mzumbe, walitoa majina ya walioshinda sahili na kuitwa kazini, ilhali mpaka muda huu hakuna tangazo katika tovuti ya sekretarieti ya ajira. Nini chanzo cha mkanganyiko huu na nini itakua hatma ya tabia hii kwa sahili zote zinazoendelea hasa katika hatua ya mwisho, hatua ya "placement"?

Ni wazi tunahitaji kuona uwajibikaji na uwazi wa hali ya juu katika hatua zote za mchakato wa upatikanaji wa ajira, kwa maana kama ambavyo tangazo la kazi linavotolewa katika tovuti ya sekretarieti, kuita watu watu kwa usahili, pia, tunaomba majina ya sahili hizi zitolewe kupitia tovuti ya sekretariati.

Tunahimiza uwajibikaji na uwazi ili kuweza kuweka usawa na kuondoa malalamiko dhidi ya namna mchakato wa upatikanaji ajira unavohitimishwa.
Ahsanteni.
 
Hao jamaa kila kazi nikiomba naambiwa cheti cha kidato cha sita sija attach wakati kipo mara zote na nimewatumia feedback hawajajibu, nimeamua kupambana kutafuta private sector,kama nimeandikiwa kufanikiwa nitafanikiwa tu
 
Hao jamaa kila kazi nikiomba naambiwa cheti cha kidato cha sita sija attach wakati kipo mara zote na nimewatumia feedback hawajajibu, nimeamua kupambana kutafuta private sector,kama nimeandikiwa kufanikiwa nitafanikiwa tu
Ukisikia lini wanajibu feedback issue.. we weka feedback yako wao wanaweza kucrosscheck na kukusaidia
 
Me naona Kawaida kwa vyuo vikuu kutangaza placements wenyewe then wakiamua wanaweza kuwatumia pdf PSRS nao wakatangaza.. Maana hata Jana SUA wametangaza placements Yao na kama unakumbuka saili zake shortlisted ilitangazwa na PSRS mwezi wa nane,, Tar 25 saili zikaanza na Jana watu wameitwa kazini.. yaan hata mwezi hujafika..
PSRS kazi Yao ni kushortlist tu
 
Me naona Kawaida kwa vyuo vikuu kutangaza placements wenyewe then wakiamua wanaweza kuwatumia pdf PSRS nao wakatangaza.. Maana hata Jana SUA wametangaza placements Yao na kama unakumbuka saili zake shortlisted ilitangazwa na PSRS mwezi wa nane,, Tar 25 saili zikaanza na Jana watu wameitwa kazini.. yaan hata mwezi hujafika..
PSRS kazi Yao ni kushortlist tu
Asante kwa mchango ndg. Yakunle
Tukiangalia kwa undani kabisa mpaka kupelekea kuundwa kwa sekretariati ya ajira ilikua kuondoa "urasimu" hasa katika katika mchakato mzima wa upatikanaji wa ajira serikalini ikiwemo kusimamia na kutangaza washindi wa sahili hizo.
Kuna dosari inajitokeza na kuota mizizi katika utekelezaji wa majukumu hayo, ni wazi na ni haki ya sahili hizi hata kama zinaendeshwa na taasisi husika, ni lazima ziratibiwe na kusimamiwa kikamilifu na sekretariati za ajira katika hatua zote zinazohusika katika upatikanaji wa ajira.
 
Me naona Kawaida kwa vyuo vikuu kutangaza placements wenyewe then wakiamua wanaweza kuwatumia pdf PSRS nao wakatangaza.. Maana hata Jana SUA wametangaza placements Yao na kama unakumbuka saili zake shortlisted ilitangazwa na PSRS mwezi wa nane,, Tar 25 saili zikaanza na Jana watu wameitwa kazini.. yaan hata mwezi hujafika..
PSRS kazi Yao ni kushortlist tu
Mimi nijuavyo PSRS ni kuchakata na kusimamia ajira zote za utumishi wa umma na kuwapelekea watu taasisi mbali mbali kwani baada ya muda taasisi inapeleka taarifa za mtumishi aliyepitia psrs kujua uwajibikaji
 
Mimi nijuavyo PSRS ni kuchakata na kusimamia ajira zote za utumishi wa umma na kuwapelekea watu taasisi mbali mbali kwani baada ya muda taasisi inapeleka taarifa za mtumishi aliyepitia psrs kujua uwajibikaji
Yeah,. Kwa lugha rahisi,. Sekretarieti ya ajira ni wakala wa ajira katika utumishi wa umma.
 
Yeah,. Kwa lugha rahisi,. Sekretarieti ya ajira ni wakala wa ajira katika utumishi wa umma.
Sahihi kabisa pia kuna taasisi flani iliita watu kazini kipindi cha nyuma walioitwa kazini wakawa hawakufika wote zile nafasi ilirudi utumishi na kutangazwa tena hivyo PSRS imeundwa rasmi kusimamia hilo ili kuondoa urasimu wa kubebana katika taasisi nyeti na kufanya watoto wa maskini wasilambe asali ya taasisi hizo
 
Sahihi kabisa pia kuna taasisi flani iliita watu kazini kipindi cha nyuma walioitwa kazini wakawa hawakufika wote zile nafasi ilirudi utumishi na kutangazwa tena hivyo PSRS imeundwa rasmi kusimamia hilo ili kuondoa urasimu wa kubebana katika taasisi nyeti na kufanya watoto wa maskini wasilambe asali ya taasisi hizo
Duuhh
 
Habari zenu wana jamvi.
Nimeshuka jamvini na swali kama linavojieleza katika kichwa cha habari.

Lengo kuu ni kuona namna gani michango ya wanajamvi inaweza saidia kufikisha ujumbe kwa wahusika na kufanya marekebisho katika dosari zinazojitokeza kila siku katika kutimiza majukum yao.

Tunafaham kuwa moja ya majukumu ya msingi ya sekretarieti ya ajira (PSRS) ni kusimamia na kuratibu mchakato mzima wa upatikanaji wa ajira kwa sekta ya umma. Kutimiza lengo hili, uwajibikaji na uwazi vinahitajika kwa kiwango cha juu mnoo kuhakikisha kunakuwepo na usawa kwa washindani katika kupigania fursa hizo.

Kwa muda mrefu kumekuwepo na malalamiko yanayoashiria kupungua kwa kiwango cha uwajibikaji na uwazi hasa linapokuja swala la watu kuitwa kazini. Malalamiko haya yanazidi kushika kasi hasa kipindi hiki ambacho kunashuhudiwa msululu wa saili zinazoendelea kujaza nafasi zilizo wazi serikalini.

Tumeshuhudia pia, matangazo ya waliofanikiwa kuitwa kuhudhuria sahili hizo kwa maana, sahili za mchujo na mahojiano yakitoka kupitia tovuti ya utumishi.

Changamoto inakuja panapohitajika uwazi zaidi namna inayofaa kutangaza majina ya walioshinda sahili hizo na hivyo kuitwa kazini. Hapa pamekua na changamoto hasa kwa siku hizi za karibuni.

Kwa siku hizi za karibuni tumeshuhudia taasisi za kiserikali kupitia tovuti zao, zikiwa za kwanza kutangaza majina ya watu walioshinda sahili na kuitwa kazini, je, kwanini katika hatua hii ya tatu ndo taasisi hizi ziwe zinatangulia kutangaza washindi na kuita watu kazinin? Ipi nafasi ya sekretarieti ya ajira katika kuwajibika na uwazi katika hatua hii muhimu katika mchakato wa kutoa ajira sekta ya umma nchini?

Kuthibitisha hili, Chuo kikuu huria kilitangulia kutoa majina ya walioshinda sahili na kuita watu kazini katika tovuti yake ya chuo, ndipo baadae sekretarieti ya ajira ikafuatia. Hali kama hiyo ikajirudia katika tovuti ya chuo kikuu Mzumbe, walitoa majina ya walioshinda sahili na kuitwa kazini, ilhali mpaka muda huu hakuna tangazo katika tovuti ya sekretarieti ya ajira. Nini chanzo cha mkanganyiko huu na nini itakua hatma ya tabia hii kwa sahili zote zinazoendelea hasa katika hatua ya mwisho, hatua ya "placement"?

Ni wazi tunahitaji kuona uwajibikaji na uwazi wa hali ya juu katika hatua zote za mchakato wa upatikanaji wa ajira, kwa maana kama ambavyo tangazo la kazi linavotolewa katika tovuti ya sekretarieti, kuita watu watu kwa usahili, pia, tunaomba majina ya sahili hizi zitolewe kupitia tovuti ya sekretariati.

Tunahimiza uwajibikaji na uwazi ili kuweza kuweka usawa na kuondoa malalamiko dhidi ya namna mchakato wa upatikanaji ajira unavohitimishwa.
Ahsanteni.

Sektetarieti ya ajira (PSRS) ni janga la kitaifa mkuu.​

Serikali isipoangali kuna siku utakuta serikslini kuna watoto wa Lowassa na JK tu.​

 
Back
Top Bottom