Kwenu akina kaka wenye kutaka mapenzi ya kweli

Sidhani kama kuna mapenzi ya kweli kwenye zama hizi. Sijui watu wote humu wako pande gani za dunia lakini huku niliko mimi hii dhana ya mapenzi ya kweli inazidi kudhihirika jinsi ilivyo potofu.

Mambo ninayoyashuhudia makazini-maofisini na kwenye ma warehouse kwa wabeba maboksi yanazidi kuniaminisha kuwa hakuna kitu kinachoitwa mapenzi ya kweli. Labda sielewi kwa ujumla dhana nzima ya mapenzi ya kweli ni nini lakini kwa kile kidogo ninachokielewa hakuna mapenzi ya kweli.

Jaribuni kupitia hapa www.ashleymadison.com. Mwenye muda anaweza kujiandikisha tu kwa ajili ya kautafiti kadogo na aone jinsi watu walivyo wahakikishiwapo faragha yao.

Huku kwetu Bongo angalau bado yapo,mimi nakuhakikishia.Labda huko dunia ya kwanza.Kila kitu mnakuwa wa kwanza
 
Hakuna ukweli katika dhana hii ya mapenzi ya kweli. kama NN aavyosema. Mimi nilijaribu kuamini yapo, niligonga mwamba. Nikabadili uelekeo nikaona yamemea mahali ambapo sikuawa na mpango nako kabisa. Nimetulia kwa muda, nabarizi life goes on. Kitu cha msingi nadhani si mapenzi ila ni ubinadamu na utu. Ukishakuwa na dhana hizi inakuwia rahisi kupunguza msongo mawazo
 
Hakuna ukweli katika dhana hii ya mapenzi ya kweli. kama NN aavyosema. Mimi nilijaribu kuamini yapo, niligonga mwamba. Nikabadili uelekeo nikaona yamemea mahali ambapo sikuawa na mpango nako kabisa. Nimetulia kwa muda, nabarizi life goes on. Kitu cha msingi nadhani si mapenzi ila ni ubinadamu na utu. Ukishakuwa na dhana hizi inakuwia rahisi kupunguza msongo mawazo

Ndio matatizo haya ya kuwa na negative thinking kila wakati,be positive man! kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi.Tulia utapata wako mwaminifu
 
Hakuna ukweli katika dhana hii ya mapenzi ya kweli. kama NN aavyosema. Mimi nilijaribu kuamini yapo, niligonga mwamba. Nikabadili uelekeo nikaona yamemea mahali ambapo sikuawa na mpango nako kabisa. Nimetulia kwa muda, nabarizi life goes on. Kitu cha msingi nadhani si mapenzi ila ni ubinadamu na utu. Ukishakuwa na dhana hizi inakuwia rahisi kupunguza msongo mawazo

Ewaaaa. Hapo umenena la maana sana MZ. Utu na ubinadamu ndicho kiwe paramount. Ukiwekeza hisia zako zote katika mapenzi ya kweli basi una hatari ya kujilengesha kuvunjwa na kuvunjika moyo baadae. Mimi nilishaachana na hiyo dhana zamani na sasa hivi najiona niko huru, mwenye amani na furaha muda mwingi. Sina cha kuhofia eti nitaibiwa au nitamvunja mtu moyo wake. Hilo halipo kabisa katika maisha yangu ya sasa.
 
Ndio matatizo haya ya kuwa na negative thinking kila wakati,be positive man! kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi.Tulia utapata wako mwaminifu

Si negative thinking ZD, ni namna ya kuangalia maisha katika uhalisia wake. Ndio maana nikasema msingi wangu wa mapenzi umejikita katika utu na ubinadamu. Mengine yanaanzia hapo. Kila wakati najikumbusha dhana hizi mbili na nimegundua, mambo yanakwenda safi tu. Kama mapenzi ya kweli yanapatikana ndani ya utu na ubinadamu, twende kazi. Kimsingi sina special category ya mapenzi ya kweli na ya uongo
 
mapenzi ya kweli yanakuja kwa watu wanaopendana kwa tabia zaidi kuliko kwa maumbo au vitu.

wapo wanawake (wachache) na wanaume (wachache zaidi) wenye kutfuta wenza kwa kutizama tabia na kuzipenda, na kutojli kitu chengine
 
Huku kwetu Bongo angalau bado yapo,mimi nakuhakikishia.Labda huko dunia ya kwanza.Kila kitu mnakuwa wa kwanza


bongo ninayoijua mie mhh, na ukipata mwenye mapenzi ya kweli cku hizi unashukuru mungu, mie cjui mambo yamekuwaje, kutendana mtindo mmoja.
 
MZ ....mwanamke kama hakupendi kweli, utu wake na ubinaadamu kwako unakua mdogo sana hivyo akikuonyesha vitu hivyo kwa viwango vya juu, jua anakupenda
 
Yako wapi bana. Kila siku watu wanaibiana. Usiwe naive kiasi hicho.
Sio suala la kuwa naive,tatizo upo mbali,ungekuwa hapa bongo ningekupeleka kwa kapo wenye mapenzi ya kweli na ningekupa muda wa kuchunguza vilevile.Usibishe tu kwa kuwa watu wengi hawana mapenzi ya kweli au kwa vile ushatendwa.Mimi nimesema kuwa yapo kwa wachache,
 
tatizo la wanaosema hamna mapenzi ya kweli sasa hivi ni kuwa: waoga wa kuwa heart broken.. wasiwasi wenu umekaa zaidi kwenye mwenzi wako kuiba/kuibiwa. usipokuwa na imani first kwenye mapenzi, sio rahisi mengine kufanikishwa..penda mtu, mengine yakitokea ni baadae, sio kwa kuwa umedinyiwa mwenzi wako once basi ndo mwisho wa maisha..
 
Sio suala la kuwa naive,tatizo upo mbali,ungekuwa hapa bongo ningekupeleka kwa kapo wenye mapenzi ya kweli na ningekupa muda wa kuchunguza vilevile.Usibishe tu kwa kuwa watu wengi hawana mapenzi ya kweli au kwa vile ushatendwa.Mimi nimesema kuwa yapo kwa wachache,

Hebu tuanzie mwanzo, mapenzi ya kweli wewe unaya define vipi? Maana tusije tukawa tunaongelea vitu viwili tofauti hapa.
 
Sidhani kama kuna mapenzi ya kweli kwenye zama hizi. Sijui watu wote humu wako pande gani za dunia lakini huku niliko mimi hii dhana ya mapenzi ya kweli inazidi kudhihirika jinsi ilivyo potofu.

Mambo ninayoyashuhudia makazini-maofisini na kwenye ma warehouse kwa wabeba maboksi yanazidi kuniaminisha kuwa hakuna kitu kinachoitwa mapenzi ya kweli. Labda sielewi kwa ujumla dhana nzima ya mapenzi ya kweli ni nini lakini kwa kile kidogo ninachokielewa hakuna mapenzi ya kweli.

Jaribuni kupitia hapa www.ashleymadison.com. Mwenye muda anaweza kujiandikisha tu kwa ajili ya kautafiti kadogo na aone jinsi watu walivyo wahakikishiwapo faragha yao.
julius mwanakwetu hee kwa style hii utaoa bro?
 
julius mwanakwetu hee kwa style hii utaoa bro?

Hapana....sitaki kuoa na sitaoa. Kwa jinsi nilivyoumbwa niko mwepesi sana wa kukinai na niko mchaguzi (picky/choosy) mno. Ni uamuzi binafsi tu na haina maana wengine wasioe au kuolewa. Kila mtu na maisha yake.
 
Hebu tuanzie mwanzo, mapenzi ya kweli wewe unaya define vipi? Maana tusije tukawa tunaongelea vitu viwili tofauti hapa.
NN oops sorry,Julius.
mbona Vera ameelezea vizuri sana hapo juu.Kwa kifupi mimi naweza kusema ni upendo ambao ndani yake kuna uaminifu,ukweli na kujali.Yani mtu asiwe material type labda kuangalia elimu yako,kabila pesa,uzuri na vitu kama hivyo.Sijui umenipata?
 
Hapana....sitaki kuoa na sitaoa. Kwa jinsi nilivyoumbwa niko mwepesi sana wa kukinai na niko mchaguzi (picky/choosy) mno. Ni uamuzi binafsi tu na haina maana wengine wasioe au kuolewa. Kila mtu na maisha yake.

Ndio maana,you are over protective pamoja na MZ.Basi nyie mnatakiwa mpate watu wa type yenu hiyihiyo
 
NN oops sorry,Julius.
mbona Vera ameelezea vizuri sana hapo juu.Kwa kifupi mimi naweza kusema ni upendo ambao ndani yake kuna uaminifu,ukweli na kujali.Yani mtu asiwe material type labda kuangalia elimu yako,kabila pesa,uzuri na vitu kama hivyo.Sijui umenipata?

You can call me NN or Julius...no need to be sorry.

Na nimekupata vyema kabisa.
 
Ndio maana,you are over protective pamoja na MZ.Basi nyie mnatakiwa mpate watu wa type yenu hiyihiyo

You are damn right and slightly wrong. Ukimapata aliye aina yako uhusiano utaboa. Utaboa kwa sababu wote mko hivyo hivyo. Hamna kipya atakachokileta katika uhusiano. Mimi nataka mtu ambaye ata complement mapungufu yangu na vice versa.

This relationship business is too complicated. Let me stop before I put my own foot in my mouth.
 
You are damn right and slightly wrong. Ukimapata aliye aina yako uhusiano utaboa. Utaboa kwa sababu wote mko hivyo hivyo. Hamna kipya atakachokileta katika uhusiano. Mimi nataka mtu ambaye ata complement mapungufu yangu na vice versa.

This relationship business is too complicated. Let me stop before I put my own foot in my mouth.

Poa & gudluck kaka.
 
Ndio maana,you are over protective pamoja na MZ.Basi nyie mnatakiwa mpate watu wa type yenu hiyihiyo

ZD
Kama alivyosema NN, ukiangalia maisha katika uhalisia wake - weka kando misaafu (maana kuna wengine hawaijui) - utagundua tunajichosha kwa kuishi maisha yakufikirika. Uzoefu wangu ni kuwa unapojaribu kuishi 'mapenzi ya kweli', utakwaa kisiki maana hayana definition. Mfano utakutana na mwanamke/mwanaume anakuheshimu kuliko wazazi wake, hayo ndio mapenzi ya kweli? Unakutana na binti/mkaka ni mkarimu kupita kiasi hayo ndio mapenzi ya kweli? Haya utakutana na mwongo/mnafiki utasema hana mapenzi ya kweli? Hapo kuna dhana mbili tu, kuwa na/au kukosa utu na ubinadamu. Wizi, uongo, majivuno, dharau, ukatili ni kukosa utu na ubinadamu na wala si kukosa mapenzi ya kweli
 
Back
Top Bottom