ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,589
Nawapa hay wanajf kwa siku ingine tena ya leo, imenibidi niseme yaliyojaa moyoni mwangu kwani kuna kitu kinakera sana acha na leo nikitapike hapa katika kolamu hii nilikuwa sitaki kukisema ila acha nikiseme kwani tunamaliza mwaka nakuwa na kitu kinachokukera usivuke nacho kwa mwaka mwinngine.
Ni hii tabia ya wanadamu hasa WANAUME wanaanzisha mahusiano kisha wanasepa, hii tabia yao imenikera sana na ndo maana nimeona niandike hapa, si wanaume wote bali ni baadhi wanatabia za kitoto na zisizoeleweka kabisa, yaani mtu anaanzisha uhusiano kama akiona amedumu na wewe mwezi mmoja au zaidi basi kile alichotafuta kwako kama amekipata utaona analeta chokochoko za hapa na pale na kisha kusepa si ameshatimiza lile kusudio alolitaka kwani abaki na wewe kwa madhumuni gani tena, wengine wanasema maneno ya kashfa kwa marafiki azao kwamba angalie dude lile pale nimelichuna kisha nimeliacha solemba. Jamani makaka zetu tabia hiyo sio mbaya kwani mnawaumiza wadada wetu bure. Ili jambo imebidi niliandike hapa kwani limenikera sana ingawaje halijanitokea mimi ila kuna mtu limemtokea na ni rafiki wa moyoni. Sipendi tabia yenu wanaume hasa wale wanaonzia na herufi hizi: J, G, I, M, A, na K sio busara kumtenda mwenzio kiasi hicho na Mungu hapendi tabia za ajabu namna hiyo. Nawaomba makaka , mababu, mababa zetu muache tabia hiyo ni mbaya sana.
Ni hii tabia ya wanadamu hasa WANAUME wanaanzisha mahusiano kisha wanasepa, hii tabia yao imenikera sana na ndo maana nimeona niandike hapa, si wanaume wote bali ni baadhi wanatabia za kitoto na zisizoeleweka kabisa, yaani mtu anaanzisha uhusiano kama akiona amedumu na wewe mwezi mmoja au zaidi basi kile alichotafuta kwako kama amekipata utaona analeta chokochoko za hapa na pale na kisha kusepa si ameshatimiza lile kusudio alolitaka kwani abaki na wewe kwa madhumuni gani tena, wengine wanasema maneno ya kashfa kwa marafiki azao kwamba angalie dude lile pale nimelichuna kisha nimeliacha solemba. Jamani makaka zetu tabia hiyo sio mbaya kwani mnawaumiza wadada wetu bure. Ili jambo imebidi niliandike hapa kwani limenikera sana ingawaje halijanitokea mimi ila kuna mtu limemtokea na ni rafiki wa moyoni. Sipendi tabia yenu wanaume hasa wale wanaonzia na herufi hizi: J, G, I, M, A, na K sio busara kumtenda mwenzio kiasi hicho na Mungu hapendi tabia za ajabu namna hiyo. Nawaomba makaka , mababu, mababa zetu muache tabia hiyo ni mbaya sana.