Asubuhi hii nilikuwa nasoma gazeti la Tanzania Daima toleo la leo tarehe 15 Juni, 2011, ambalo limeripoti kwamba Lowassa anarejea leo kutoka Nigeria ambako gazeti hili limeripoti kwamba alikwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa kwa Nabii Joshua. Taarifa hiyo ilitoa pia sifa za Nabii huyo kuhusiana na uponyaji wake, utajiri wake na ukubwa na umaarufu wa kanisa lake duniani kote.
Habari hii kwa kiasi kikubwa ilikuwa na nia ya ku-pre-empty habari iliyochapishwa katika toleo la leo la Mwanahalisi ambalo limechambua kwa kiasi kikubwa kile kinachofikiriwa kuwa ni madhumuni ya msafara wa Lowassa na nukuu kutoka kwa watu wake wa karibu. Lilirejea pia mawasiliano kati ya Beatrice Shellukindo na Pindi Chana kuhusu nguvu na dhamira ya Lowassa na maoni ya nabii Joshua kuhusu uwezekano wa Lowassa kuwa rais wa nchi hii 2015.
Kwa muelekeo huu, Tanzania Daima limeendelea kuthibitisha kwamba sasa hivi gazeti hili lnatumika kama maliwato ya kuwatakasa mafisadi na hasa mapacha hawa watatu na wakati huo huo kuwa ni mdomo wao katika masuala mbali mbali yanayohusiana na tuhuma na dhamira zao kisiasa. Sina shaka huu ni utekelezaji wa mpango wa Kibanda kuwa mpagazi wa mafisadi kuelekea uchaguzi wa 2015.
Habari hii kwa kiasi kikubwa ilikuwa na nia ya ku-pre-empty habari iliyochapishwa katika toleo la leo la Mwanahalisi ambalo limechambua kwa kiasi kikubwa kile kinachofikiriwa kuwa ni madhumuni ya msafara wa Lowassa na nukuu kutoka kwa watu wake wa karibu. Lilirejea pia mawasiliano kati ya Beatrice Shellukindo na Pindi Chana kuhusu nguvu na dhamira ya Lowassa na maoni ya nabii Joshua kuhusu uwezekano wa Lowassa kuwa rais wa nchi hii 2015.
Kwa muelekeo huu, Tanzania Daima limeendelea kuthibitisha kwamba sasa hivi gazeti hili lnatumika kama maliwato ya kuwatakasa mafisadi na hasa mapacha hawa watatu na wakati huo huo kuwa ni mdomo wao katika masuala mbali mbali yanayohusiana na tuhuma na dhamira zao kisiasa. Sina shaka huu ni utekelezaji wa mpango wa Kibanda kuwa mpagazi wa mafisadi kuelekea uchaguzi wa 2015.