Kweli nimepatikana siamini

Kweli nimepatikana siamini

Kama yupo JF fanya mpango ausome uzi wako, na kama hayupo
Mwambie ajiunge JF akiuwona huu uzi wako itakua umemfikishia ujumbe wako kwa urahisi sana
 
unamuonea wivu mpaka anajua duuuu
jiongeze mwanamke tengua kitengo
 
Hivi kumbe bado kuna watu wanateswaaga na mahaba mpaka kipindi hii ya makinikia????
 
Fanya hivi, mualike kwako kama unajitegemea, muandalie chakula na vinywaji vizuri vya asili kama juice fresh. Kuwa huru mfano unakaa nae kwenye kochi moja, ukiwa unacheka mmefurahi unamuegemea kama kawaida. Usilazimishe kwenda kwake inaweza kuwa ana mwanamke wake ndio maana alikuwa haangaiki ni nyie hapo kazini. With time atakuelewa tu au atajikuta kakupenda. Na inawezekana huo unaoita ni msimamo sio udhaniavyo inaweza kuwa domo zege tu. Kwa kutumia njia ya kujiweka karibu sana na huru itampunguzia woga wa kukutongoza. Ukishindwa yote jilipue mwambie sasa umekuwa mpweke sababu upo single kwa muda mrefu akupe ushauri, hapo atakuelewa tu. Akikuuliza au kukushauri utafute mtu ndipo umjibu hauwezi tafuta sababu ni mwanamke inabidi utafutwe wewe. Uzuri wa njia hii ya kuomba ushauri ni kwamba akionesha kukukwepa au kukujibu kwamba yeye hayupo tayari au ana mtu basi na wewe unageuka unatabasamu una mwambia alikuelewa vibaya hauku mlenga yeye.
Uko vizuri Titicomb
 
Uko vizuri Titicomb
Hahaaa. Mkuu mimi nilijikuta namtokea msichana kwa sababu ya hizi mbinu zake za medani japo yeye tulikuwa tunaheshimiana sana kiasi cha kuniita kaka flani, alikuwa hawezi kukaa na mimi kochi moja na kuniegemea bali alikuwa ananialika kwao kwa lunch(alikuwa anaishi na dada yake). Alikuwa anakuja gheto kwangu. Mimi nikasoma ishara ndio ikatokea vile tena.... malizia stori mwenyewe. Mimi sikuwa domo zege lakini nilikuwa na demu mwingine ambae alikuwa hatupo vizuri kimahusiano na sikutaka demu maeneo jirani na ninapoishi ndio nikaamua kuwa serious sana hadi majirani wa kike wananiogopa.
 
SIMBA MWENDA POLE NDO MLA NYAMA, SI AJABU HATAKI MAZOEA NA WADADA OFISINI HAPO KWA SABABU ANAHOFIA ATAHARIBU KAZI, ILA JE, UMEMCHUNGUZA HUKO MTAANI HALI IKOJE. TAKWIMU ZINAONESHA KUWA WANAWAKE/WANAUME WAKIMYA NDO WANAONGOZA KWA TABIA MBAYA NYUMA YA PAZIA... REJEA WIMBO WA ALIKUFA KWA NGOMA WA MWANA FA

ANYWAY, KAMA UMEJIRIDHISHA KUWA UNAMPENDA NA ANAKUMFAA, MWELEZE UKWELI, SI AJABU NA YEYE ANAKUELEWA ILA NI DOMO ZEGE (ULIMI MZITO).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom