Tuna uwezo sawa kiakili, tatizo ni maumbile na resources tu wao ni wavivu sana na resource haziwatoshi ndo maana walikua wanatumia mda mwingi kufikiria njia rahisi ya kurahisisha kazi zao na ku-maximize matumizi ya resources zao. Wakati wao wanatakiwa kula matunda na mboga zikitokea kwenye friji kwasababu hazipatikani kirahisi, sisi tulikua tunakula matunda kutoka mitini moja kwa moja na kila msimu ukiwa na aina yake ya matunda na ukihitaji mboga za majani unaenda mabondeni kuchuma zilizojiotea zenyewe. Wakati wao wanahitaji na wanafikiria vifaa vya ku-purify maji yaliyochafuliwa na shughuli zao za kiuchumi, sisi tulikua tunajinywea maji kutoka kwenye chemi chemi za asiri zilizokua kibao na mpaka sasa bado zipo baadhi zinatoa maji safi na salama. wakati sisi tumezoea kila kitu kinawezekana kwa kutumia msuri kwa mfano ukitaka kushusha bei ya sukari unaagiza bei iwe shingapi na unavielekeza vyombo vya dola visimamie hilo, wao wanaanza kujiuliza nadhalia za Demand and supply zinasema nini Tehe!!