Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Kuna watu ambao wamewahi "kujikuta" kwenye kitendo cha ngono na mtu ambaye baadaye au kesho yake wanajutia kwanini ilitokea hivyo. Na mara nyingi inatokea katika mazingira ya sherehe sherehe hivi. Kisa kimoja ambacho kiliwahi kunishangaza sana na jamaa ambaye alijikuta ametoka na mke wa rafiki yake na kisingizio pekee ni kuwa "walikuwa wamelewa". Na wengine wamekuwa wakitumia maneno kuwa "one thing led to another" wakimaanisha kwamba labda walianza kutaniana, kugusana n.k na mwisho wakajikuta kwenye mazingira tamanishi.
Hapa inabidi tuhoji:
a. Je ni kweli suala hilo laweza kweli kutokea kwa bahati mbaya?
b. Je, majuto yanayofuatia ni ishara kuwa mtu kweli hakuwa amefikiria - na hasa watu ambao wanajikuta kweli wanajutia tendo hilo?
c. Je, mtu aliyeingia kwenye mazingira hayo tamanishi anaweza kweli kujiamini tena mbele ya yule mtu mwingine - hata kama hakumbuki?
d. Je kutokea kwa bahati mbaya ni uhalalisho wa kuanzisha "full scale" affair? au kama kweli unajutia usirudie tena? Inakuwaje kwa wale ambao baadaye wanaanza kuwa curious tena?
Lakini je kuna watu ambao wamewahi kujikuta ile "bahati mbaya" imegeuka kuwa ni bahati "nzuri" ya kuanzisha uhusiano wa kudumu? itakuwaje wale wengine ambao wanatengeneza "bahati mbaya" kwa sababu tu wanajua wanaweza kudai kuwa "walikosea"?
Hapa inabidi tuhoji:
a. Je ni kweli suala hilo laweza kweli kutokea kwa bahati mbaya?
b. Je, majuto yanayofuatia ni ishara kuwa mtu kweli hakuwa amefikiria - na hasa watu ambao wanajikuta kweli wanajutia tendo hilo?
c. Je, mtu aliyeingia kwenye mazingira hayo tamanishi anaweza kweli kujiamini tena mbele ya yule mtu mwingine - hata kama hakumbuki?
d. Je kutokea kwa bahati mbaya ni uhalalisho wa kuanzisha "full scale" affair? au kama kweli unajutia usirudie tena? Inakuwaje kwa wale ambao baadaye wanaanza kuwa curious tena?
Lakini je kuna watu ambao wamewahi kujikuta ile "bahati mbaya" imegeuka kuwa ni bahati "nzuri" ya kuanzisha uhusiano wa kudumu? itakuwaje wale wengine ambao wanatengeneza "bahati mbaya" kwa sababu tu wanajua wanaweza kudai kuwa "walikosea"?