sasa kura zinaendaga wapi?
Hujui wanaziibaa??? tume,polic n.k (uchakachuzi) Usirudie tena kkuliza swali kama hilo!!!
sasa kura zinaendaga wapi?
kama mnafikiri mnakubalika kafanyeni mkutano jangwani au k/ndege(moro) hapo muone aibu yake..mnafikiri kila sehemu ni Arusha au Moshi.
nimeona kama mtoa mada ameandika mwanza au nayo iko moshi?kama mnafikiri mnakubalika kafanyeni mkutano jangwani au k/ndege(moro) hapo muone aibu yake..mnafikiri kila sehemu ni Arusha au Moshi.
huwa napenda sana maneno ya viongozi wa chadema wanaposema maneno haya
WAO WANA PESA SISI TUNA MUNGU.
huwa napenda sana maneno ya viongozi wa chadema wanaposema maneno haya
WAO WANA PESA SISI TUNA MUNGU.
Hiyo ni kali na Bado,Kwani watu wameamua kufanya kweli hakuna wa kuwazuia.
hata wazee nao wanakipenda cdm ni waganga tu wakienyeji ndio hawakipendi cdm.
Imetokea jana kwenye Dala dala la Kutoka Airport kwenda Buhongwa (MWANZA), Kama kawaida ya konda ndani ya dala dala anadai chake (Nauli), kabla hajamaliza kudai nauli gali likakata mafuata kiaina (likawa linazimika zimika), ikabidi dereva aingie sheli kuongeza mafuta.
Hatujajua kinachoendelea akainuka mama mmoja kwa asila na kumkoromea konda na dereva, akisema: Mambo ya kutembea na Mafuta ya vidumu mnatuchelewesha kwenye vikao na ntaenda kupigwa faini kwa kuchelewa Tsh. 5,000/=: Mara jirani yake akadakia, Kikao cha nini? Mama akajibu: Kikao cha chama, kwa mshangao wa wengi, kila mmoja alidhani labda kikao cha wakinamama au SACCOS: Mama akadakia tena: Kwenye kikao cha chama cha CHADEMA!
Nkiwa bado nashangaa abiria wote wakadakia: Kama ni kikao cha CHADEMA, tutakuchangia iyo faini, nilidhani kama utani! Kwanza yule konda akamwambia yule mama: wewe ni mjanja, akamrudishaia nauli yake, nkiwa naendelea kushangaa, konda akaanza kukusanya michango kwa ajili ya yule mama. Amini usiamini alichangiwa Tsh. 32,500/=. Chakushangaza zaidi hata watoto wa shule walimchangia yule mama.Nilibaki kushangaa mwanzo mwisho!
Naanza kuisi mabadiliko, kweli hapa Mwanza si mchezo.
Ni mimi nisiyekuwa mwanachama wa chama chochote kwa sasa.