Huu ni mtazamo........
Kwanza kabisa nini kinakujulisha kama yesu alikua hakemei au afumbi macho??, biblia yako ina onesha video??, au inatoa sauti za wahusika...??, achana nayo twende kwenye maandiko injili ya yohana 21:25 anasema, hata dunia isingetosha kama aliyoyafanya yesu wakisema yaandikwe, Sasa hapo manake nini, kuna baadhi ya matukio yameachwa hayakuandikwa!!!!, unakubali???, Sasa kama ni Ivo vipi kama hiko unachokihoji ni baadhi ya matukio ambayo hayakusimuliwa??.
Lakini pia kwenye hio injili ya yohana zile sura 14, 15, 16, 17... Mazungumzo ya mwisho kabla yesu hajashikwa na watesi, aliwaambia wanafunzi wake, bado ningali Nina mengi ya kuwaambia ila hamuezi kustahimili kwa sasa, ila atapokuja huyo msaidizi atawafundisha yote. Ambae hapa alikua anazungumziwa roho mtakatifu..., Sasa hoja nini??,
Hatuezi kutengeneza argument kisa baadhi ya matukio hayakuandikwa kwenye biblia, au hayakuonekana sababu tayari kuna ahadi ya mwalimu, Ambae kazi yake kukufundisha yale amabayo bado hujafundishwa, Ambae yesu kristo anamwita roho mtakatifu Ambae ataishi ndani yako.., Sasa ukimpata huyu uwezi kuuliza tena kutegemea maoni ya watu Bali atakua kama table teacher.