Kwanini Yesu hakuwahi kuombea Mgonjwa?

Kwanini Yesu hakuwahi kuombea Mgonjwa?

Kwenye lugha ya kitheolojia na kiutamaduni wa Mashariki ya Kati, kuketi mkono wa kuume maana yake ni kuwa na mamlaka sawa, nguvu sawa, na utukufu mmoja.
Twende mdogo mdogo we guluguja wa kigalatia.

Ntaendelea kukupiga nyundo mpaka kesho uone aibu kuokota sadaka za mazezeta ya kigalatia.

Huyu Mungu wa pekee ni yupi na yesu kristo aliyetumwa ni yupi?

Je aliyetumwa anaweza kuwa na nguvu sawa na aliyemtuma?
Screenshot_20260803-213657_Chrome.jpg
 
Kijana unatafsiri Biblia kama unasoma hadithi za Alfu Lela Ulela!
Acha porojo na longolongo.

Mbona maandiko ya kutoa sadaka na fungu la kumi mnayatafsri kama vitabu vya hadithi za alfu Lela ulela.

Acheni utapeli.
 
Kwanza unaaminije biblia vipi kama ni story za kutunga maana hamna solid evidence
Unajua aliyekufunza hiyo lugha na kila kitu ukijuacho leo hii ndiye aliyekuletea Biblia?
 
Twende mdogo mdogo we guluguja wa kigalatia.

Ntaendelea kukupiga nyundo mpaka kesho uone aibu kuokota sadaka za mazezeta ya kigalatia.

Huyu Mungu wa pekee ni yupi na yesu kristo aliyetumwa ni yupi?

Je aliyetumwa anaweza kuwa na nguvu sawa na aliyemtuma?View attachment 3642699
Bado haujajua kuishirikisha akili yako vizuri, na unaitumia vibaya sana kwa kukariri mifumo ya kibinadamu! Yani hili swali ulilo uliza ni kama umefikiri kwa kutumia mfumo wa bosi na mfanyakazi wake.

Kwenye Uungu, sivyo ilivyo.Kwenye muktadha wa kidiplomasia, balozi anapotumwa na nchi yake anakuwa na mamlaka kamili ya nchi nzima nyuma yake, neno la balozi ni neno la nchi iliyomtuma. Sasa weka picha hiyo kwenye Yohana 17:3 mstari unaoupenda. Yesu alitumwa duniani kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa mission ya kiungu ya ukombozi.

Aliyetumwa na aliyemtuma ni wamoja katika asili na nguvu, hakuna aliyemzidi mwenzake nguvu, bali walitofautiana majukumu kwa muda tu hapa duniani, logic rahisi kama hii unaweza kueleweshwa hata na mtu ambaye hajasoma kabisa theolojia.
 
Aliyetumwa na aliyemtuma ni wamoja katika asili na nguvu, hakuna aliyemzidi mwenzake nguvu,
Tapeli mkubwa wewe.

Wewe na Yesu tumsikilize nani?

Yani niache kumsikilza yesu anayesema baba ni mkuu kuliko yeye nikusikilize wewe tapeli unayedanganya ili upewe sadaka kama yule muuza mafuta na udongo pale kawe?

Hivi nyie wajasiliadini mtaacha lini utapeli?
Screenshot_20260803-215322_Chrome.jpg
 
Hapa umetoka nje ya mada kijana, usichanganye Uungu wa Yesu na njaa za wachungaji wenu wa sasa.
Yesu na baba nani mkuu?

Jubu swali acha longolongo.

Je andiko la Yohana 14:28 yesu anaposema Baba ni mkuu kuliko yeye limekosewa au lipo sahihi?
 
Bibila na yesu mwenywe aliseme na inasema Yesu ni mwana wa Mungu- aliyetumwa na Mungu. kwenye issue ya maombi kuna sehemu ya kumwomba Mungu na kuna sehemu ya kukemea au kutamka. Na mtu akapona. NB maombi hayafanyi kazi kwa kila mtu au kwa kila hali.
 
Tapeli mkubwa wewe.

Wewe na Yesu tumsikilize nani?

Yani niache kumsikilza yesu anayesema baba ni mkuu kuliko yeye nikusikilize wewe tapeli unayedanganya ili upewe sadaka kama yule muuza mafuta na udongo pale kawe?

Hivi nyie wajasiliadini mtaacha lini utapeli?View attachment 3642712
Nina muda mwingi sana leo wa kukufungua fahamu zako zilizo fungwa.

Hiyo Yohana 14:28 ndio fimbo yenu ya kila siku, lakini huwa hamuelewi kabisa maana ya neno Mkuu. Iko hivi kuna utofauti kati ya kuwa mkuu kwa cheo na kuwa bora kwa asili.

Mwanamke na mwanaume ni sawa kabisa kiutu na kiasili, lakini kwenye familia mume ni mkuu kicheo. Rais wa nchi ni mkuu kuliko mimi na wewe kicheo, lakini kiasili sote ni binadamu wale wale 100%. Yesu alipokuja duniani, alijishusha kwa hiari na kuwa mdogo kicheo kuliko Baba ili akamilishe kazi ya msalaba, soma Wafilipi 2 utaelewa. Utu wake ulikuwa chini ya Baba, lakini Uungu wake ni mmoja na Baba.

Wewe bado una tatizo la kuisoma Biblia kama hadithi za paka na panya ndiyo maana inakupiga chenga pakubwa sana mdogo wangu.
 
Yesu na baba nani mkuu?

Jubu swali acha longolongo.

Je andiko la Yohana 14:28 yesu anaposema Baba ni mkuu kuliko yeye limekosewa au lipo sahihi?
Sasa hivi mimi nikisema Rais wa nchi ni mkuu kuliko mimi andiko langu litakuwa limekosewa? Litakuwa sahihi kabisa. Lakini je, Rais ni mkuu kiasili? Hapana, wote ni binadamu wale wale 100%, hakuna aliye nusu mtu au robo mtu. Yesu aliposema Baba ni mkuu kuliko mimi alikuwa anaongelea cheo na nafasi yake ya unyenyekevu kama mwanadamu hapa duniani, sio asili yake ya Uungu. Andiko liko sahihi, uelewa wako ni finyu tu.
 
Bado haujajua kuishirikisha akili yako vizuri, na unaitumia vibaya sana kwa kukariri mifumo ya kibinadamu! Yani hili swali ulilo uliza ni kama umefikiri kwa kutumia mfumo wa bosi na mfanyakazi wake.

Kwenye Uungu, sivyo ilivyo.Kwenye muktadha wa kidiplomasia, balozi anapotumwa na nchi yake anakuwa na mamlaka kamili ya nchi nzima nyuma yake, neno la balozi ni neno la nchi iliyomtuma. Sasa weka picha hiyo kwenye Yohana 17:3 mstari unaoupenda. Yesu alitumwa duniani kwa sababu hiyo ndiyo ilikuwa mission ya kiungu ya ukombozi.

Aliyetumwa na aliyemtuma ni wamoja katika asili na nguvu, hakuna aliyemzidi mwenzake nguvu, bali walitofautiana majukumu kwa muda tu hapa duniani, logic rahisi kama hii unaweza kueleweshwa hata na mtu ambaye hajasoma kabisa theolojia.
wacha nikae kimyaaaa..
mkuu unajua kwanini Baraza la Nicea liikaa?

kuan hivi vitu kaangalie Homoousios "same substance" (homos = same, ousia = essence/being).. na usome na Homoiousios... ukimaliza kusoma hivi vitu andika tena ulichoandika...
Trinity-560x560.jpg
 
Sasa hivi mimi nikisema Rais wa nchi ni mkuu kuliko mimi andiko langu litakuwa limekosewa? Litakuwa sahihi kabisa. Lakini je, Rais ni mkuu kiasili? Hapana, wote ni binadamu wale wale 100%, hakuna aliye nusu mtu au robo mtu. Yesu aliposema Baba ni mkuu kuliko mimi alikuwa anaongelea cheo na nafasi yake ya unyenyekevu kama mwanadamu hapa duniani, sio asili yake ya Uungu. Andiko liko sahihi, uelewa wako ni finyu tu.
hapana mkuu Mi naomba nipingane na wewe Hakuna yesu alizungumzia divinity yaani uungu..
divinity tunamuwekea sisi..

natamani unionyeshe alipozungumzia divinity yaani yeye ni Mungu
 
du labda sijaelewa swali...
alimponya mwenye ukoma
alimuombea na kumfufua mgonjwa ambae alipofika alimkuta kafariki

....
 
wacha nikae kimyaaaa..
mkuu unajua kwanini Baraza la Nicea liikaa?

kuan hivi vitu kaangalie Homoousios "same substance" (homos = same, ousia = essence/being).. na usome na Homoiousios... ukimaliza kusoma hivi vitu andika tena ulichoandika...View attachment 3642750
Hebu nikukumbushe historia kidogo. Baraza la Nicea lilikaa kupinga uzushi wa mzee mmoja anaitwa Arius, ambaye alikuwa anasema Yesu si Mungu kamili bali ni kiumbe tu, na alikuwa anapigania neno Homoiousios kwamba Yesu anafanana tu asili na Mungu.

Baraza la Nicea likamkataa Arius na likapitisha neno Homoousios kwamba Yesu na Baba wana ASILI MOJA, UUNGU MMOJA, NA UTUKUFU MMOJA WA Milele!

Ukidai Yesu sio Mungu, si unakuwa unashikilia msimamo wa Arius aliyelaaniwa na hilo baraza? Baraza la Nicea lilithibitisha Uungu wa Yesu, wewe unalitaja kama fimbo ya kunipiga mimi? Umesoma vizuri lakini au umegoogle juu juu tu Mkuu?
 
hapana mkuu Mi naomba nipingane na wewe Hakuna yesu alizungumzia divinity yaani uungu..
divinity tunamuwekea sisi..

natamani unionyeshe alipozungumzia divinity yaani yeye ni Mungu
Kaka, unakosea sana unaposema sisi ndio tunamvesha Uungu. Yesu alitamka mwenyewe kwa mdomo wake, tena mbele ya Wayahudi waliokuwa wanaijua Torati vizuri sana.

Fungua Yohana 8:58, Yesu anawaambia, Amin, amin, nawaambia, Mbele Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO. Kumbuka neno Mimi Niko ndilo jina takatifu kabisa ambalo Mungu alijitambulisha nalo kwa Musa kule kwenye kichaka kinachowaka moto. Wayahudi walimuelewa vizuri sana kwamba anajiita Mungu, ndio maana mstari uliofuata walipiga chini porojo wakaokota mawe ili wampige kwa makosa ya kukufuru, mbona alizungumzia Uungu wake mchana kweupe, hata ukisoma Yohana 10:30, Yesu anasema kwa kifupi kabisa Mimi na Baba tu mmoja!
 
Wewe hujasoma biblia vizuri Yesu alikesha mlima Horebu akisali kabla ya kumponya mwenye pepo bubu. Soma Marko 9:2-29
 
Hebu nikukumbushe historia kidogo. Baraza la Nicea lilikaa kupinga uzushi wa mzee mmoja anaitwa Arius, ambaye alikuwa anasema Yesu si Mungu kamili bali ni kiumbe tu, na alikuwa anapigania neno Homoiousios kwamba Yesu anafanana tu asili na Mungu.

Baraza la Nicea likamkataa Arius na likapitisha neno Homoousios kwamba Yesu na Baba wana ASILI MOJA, UUNGU MMOJA, NA UTUKUFU MMOJA WA Milele!

Ukidai Yesu sio Mungu, si unakuwa unashikilia msimamo wa Arius aliyelaaniwa na hilo baraza? Baraza la Nicea lilithibitisha Uungu wa Yesu, wewe unalitaja kama fimbo ya kunipiga mimi? Umesoma vizuri lakini au umegoogle juu juu tu Mkuu?

Kwanza historia ya dini nimeisoma na nakumbuka miaka 30 iliyopita nilifanya reseach kuhusu hiyo historia mpaka israel so ilikuwa ni moja ya my specialtykwahiyo tunaweza kuizungumzia wiki nzima bila kuchoka.. pili Nimeitumia njia yako mwenyewe ya hoja ili kukuonyesha jambo moja muhimu. Umeniletea uamuzi wa Baraza la Nicea ili kuthibitisha uungu wa Yesu, lakini kwa kufanya hivyo umekiri kwamba hoja yako inategemea tafsiri na maamuzi ya wanatheolojia wa karne ya nne, si maandiko.

Kwa mantiki hiyo hiyo, kumbuka kwamba neno "Utatu" (Trinity) halipo popote katika Biblia. Ni neno lililotungwa baadaye na wanatheolojia ili kuelezea mafundisho fulani. kama tunarudi kwenye mamlaka ya Biblia, basi hoja yetu lazima isimame juu ya maandiko yaliyoandikwa, sio kwenye maamuzi ya mabaraza ya kanisa, ambayo ukitaka tunaweza kudiscuss udhaifu wa mabaraza yote kuanzia baraza la nicea mpaka Council of Trent..

Mimi sitaki tujadili kuhusu liturujia, mapokeo ya kanisa, wala dogma zilizokuja baadaye. Nataka tujadili kile kilichoandikwa katika Biblia.

Kwa mfano, Biblia ina maandiko kama aliyotoa mtoa post wa nyuma hapo na kakupa ila hujajibu ila umeleta porojo kama:
  • Yohana 17:3 – Yesu anamwita Baba "Mungu wa pekee wa kweli."
  • Marko 12:29 – Yesu ananukuu: "Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja."
  • Yohana 20:17 – Yesu anasema: "Ninakwenda kwa Baba yangu na Baba yenu, kwa Mungu wangu na Mungu wenu."
  • 1 Wakorintho 8:6 – "Kwetu sisi yuko Mungu mmoja, Baba... na Bwana mmoja, Yesu Kristo."
  • 1 Timotheo 2:5 – "Yuko Mungu mmoja, na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, mwanadamu Kristo Yesu."
Naomba unioneshe andiko linalosema wazi na bila utata "Yesu ndiye Mungu Mwenyezi," au "Mungu ni Utatu wa Nafsi Tatu." Kama lipo, tulisome pamoja katika muktadha wake.

Kwa taarifa yako, mimi ni mwanatheolojia na nimejifunza na kufundisha theolojia kwa takribani miaka 39. Kwa hiyo, siogopi mjadala wa kisomi wa kiblia, Lakini ningependa mjadala wetu ujengwe juu ya Sola Scriptura yaani, kile Biblia inasema ,badala ya maamuzi ya mabaraza ya kanisa, liturujia au dogma zilizotungwa baada ya enzi za mitume.

Tukubaliane jambo moja tuache kunukuu mamlaka za watu, turudi kwenye mamlaka ya Maandiko. Hapo ndipo mjadala utakuwa wa haki na wenye manufaa.
nakuwasilishia
 
Back
Top Bottom