Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,928
Wakati wowote yanapotokea majanga, aidha ndani ya nchi zao u hata nje ya nchi zao raia wa nchi zilizoendelea wamekuwa na haraka ya kusaidia na kutoa misaada kwa haraka zaidi. Ninauliza hili nikilinangisha na mwitikio wa watu wetu kwenye majanga vile vile.
Leo hii wakati Haiti imekumbwa na tetemeko la ardhi, tayari wenzetu wameshaweka utaratibu wa watu wa kawaida kuchangia taasisi mbalimbali ikiwemo chama cha msalaba mwekundu. Na tayari hadi watoto wa shule hapa nilipo wameanza kukusanya nguo na vyakula vya makopo kupeleka huko Haiti!
Kwanini sisi, inakuwa mbinde sana kujitokeza kusaidia!? Yawezekana ni kweli Mungu amewapendelea wenzetu hawa kwa kuwapa moyo wa ukarimu zaidi kulikop watu weusi? Yawezekana wenzetu wanajali wenzao hata wageni zaidi kuliko sisi wengine? Yawezekana labda sisi tunapenda sana kuzungumza na kuonesha madhaifu kuliko kuonesha mfano wa kutenda?
Na wale Watanzania ambao wamejitokeza kuchangia hadi hivi sasa ndugu zao waliopatwa na mafuriko yawezekana wamefanya hivyo kwa sababu ni matajiri zaidi au ni moyo wao wa kutoa?
Kwa kweli nahisi kuchanganyikiwa!
Leo hii wakati Haiti imekumbwa na tetemeko la ardhi, tayari wenzetu wameshaweka utaratibu wa watu wa kawaida kuchangia taasisi mbalimbali ikiwemo chama cha msalaba mwekundu. Na tayari hadi watoto wa shule hapa nilipo wameanza kukusanya nguo na vyakula vya makopo kupeleka huko Haiti!
Kwanini sisi, inakuwa mbinde sana kujitokeza kusaidia!? Yawezekana ni kweli Mungu amewapendelea wenzetu hawa kwa kuwapa moyo wa ukarimu zaidi kulikop watu weusi? Yawezekana wenzetu wanajali wenzao hata wageni zaidi kuliko sisi wengine? Yawezekana labda sisi tunapenda sana kuzungumza na kuonesha madhaifu kuliko kuonesha mfano wa kutenda?
Na wale Watanzania ambao wamejitokeza kuchangia hadi hivi sasa ndugu zao waliopatwa na mafuriko yawezekana wamefanya hivyo kwa sababu ni matajiri zaidi au ni moyo wao wa kutoa?
Kwa kweli nahisi kuchanganyikiwa!