Kwanini wazazi wengi bado wako 'obsessed' na As na Bs za matokeo ya mitihani?

The Assassin

JF-Expert Member
Oct 30, 2018
4,355
17,321
Leo Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya kidato cha 2,4 na mitihani ya ufahamu kwa wanafunzi wote waliofanya hiyo mitihani mwaka 2021.

Mwezi june 2022 itatutangazia matokeo ya form 6 pia kama kawaida ya miaka yote, kila mwaka ni matokeo ya ulinganifu wa nani kafanya vizuri na nani kafanya vibaya.

Kinachonisikitisha ni kwamba pamoja na udhaifu mkubwa sana wa huu mfumo wa elimu tulionao ambao bado unawaandaa wanafunzi kua waajiriwa, bado wazazi wengi kama sio wote wako na tamaa ya kuona watoto wao wanapata A ama B au Div 1 au 2.

Wote tunakubaliana kwamba huu mfumo wa kupima watu uelewa ama ufahamu wa kukabiliana na changamoto zinazowazunguka ni wa hovyo lakini bado wazazi wako very much obsessed na As. Pamoja na kwamba huu mfumo wa mitihani ni mbovu, unaua ubunifu, ugunduzi, uvumbuzi na uchambuzi wa masuala muhimu kwenye jamii lakini bado Tanzania yunaikumbatia na kuushadadia kwa kila hali.

Tujiulize, hao top 10 wa kitaifa wa kila mwaka, yaani Tanzania kila mwaka tunapata watu wenye akili kuliko wote 20, je hao ma genius hua wanasaidia nini taifa? Je wanakua na mchango gani kwa nchi? Utashangaa hao brainy ama geniuses 20 wa kila mwaka huishia kupewa kazi serikalini, kuajiriwa eitha kua waalimu vyuo vikuu ama maafisa wa kawaida wa serikali.

Dhana ya elimu ni kumpa mtu ufahamu, uelewa na ujuzi wa kukabiliana na changamoto na mazingira yanayomzunguka. Sasa hnajiuliza toka lini kupata elimu ikawa mashindano? Kwamba hata kutatua changamoto zinazotuzunguka tunazitatua kwa mashindano? Ama mtu akipata A basi yeye atatatua changamoto haraka zaidi na kwa ufanisi kuliko aliepata D? Mbona hatuoni faida za A ama Div 1 kwenye jamii?

Hivi 1 zilivyo nyingi kila mwaka sitegemei Tanzania bado tungekua na changamoto yoyote inayotuzunguka maana tuna geniuses wa kutosha.

Hii mada inaendelea.
 
Kwa sababu High IQ ni kiashiria cha mafanikio maishani, ofcourse kuna exceptions kama Mondi au “kudra za Mwenyezi Mungu“ lkn watu wengi waliofanikiwa maishani wengi wao high IQ, na kipimo cha IQ ni uwezo wa kusolve problems, hivyo basi ukipata A in maana una uwezo mkubwa wa kusolve problems, utafaulu ukifaulu utapata cheti kizuri kitakacho kubeba mbele ya safari, hiyo ndiyo sababu, …
 
Kwa sababu High IQ ni kiashiria cha mafanikio maishani, ofcourse kuna exceptions kama Mondi au “kudra za Mwenyezi Mungu“ lkn watu wengi waliofanikiwa maishani wengi wao high IQ, na kipimo cha IQ ni uwezo wa kusolve problems, hivyo basi ukipata A in maana una uwezo mkubwa wa kusolve problems, utafaulu ukifaulu utapata cheti kizuri kitakacho kubeba mbele ya safari, hiyo ndiyo sababu, …
Nipe mfano wa hzo problems ambazo zimesoviwa na hao genius!!

Nchi inatangaza magenious kila mwaka afu nch hyo hyo inaenda kujenga stand kuu ya kimataifa kwny swamp area kabisa,,,, like WTF are those u call dem genious
 
Nipe mfano wa hzo problems ambazo zimesoviwa na hao genius!!

Nchi inatangaza magenious kila mwaka afu nch hyo hyo inaenda kujenga stand kuu ya kimataifa kwny swamp area kabisa,,,, like WTF are those u call dem genious

Hilo ni swala lingine na ni tatizo la nchi kiujumla, lkn bado ukweli unabakia kuwa ukweli kwamba mtoto anayefaulu vizuri ( sana) ana nafasi kubwa ya kufanikiwa maishani kuliko yule wa wastani .
 
Nakubaliana na mtoa mada.

Yaan kila mwaka tuna waona Tanzania 1 lakini nchi mpaka leo tuna maisha ya kuunga sanaa...
Tumekuwa hatuna hata wataalam wakutengeneza bara bara ya lami mpaka mkataba apewe mchina.

Majengo makubwa ya Serikali wataalam wanatoka nje.
Yaan wasomi wetu wanakuja mtaam kuendesha boda boda na wengine wanauza mitumba na huku wakijikuta wanafunfisha tution

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Kwa sababu High IQ ni kiashiria cha mafanikio maishani, ofcourse kuna exceptions kama Mondi au “kudra za Mwenyezi Mungu“ lkn watu wengi waliofanikiwa maishani wengi wao high IQ, na kipimo cha IQ ni uwezo wa kusolve problems, hivyo basi ukipata A in maana una uwezo mkubwa wa kusolve problems, utafaulu ukifaulu utapata cheti kizuri kitakacho kubeba mbele ya safari, hiyo ndiyo sababu, …
Hakuna mvumbuzi ama mwanasayansi aliefanikiwa maishani ambae alikua anafauli mitihani. Einstein hakua mzuri kwenye mitihani ila mambo yake unayajua hata kama hujawahi kumuona, Galileo, Newton hawakuwahi kufanya mitihani.

John Keynes mchumi mkubwa Duniani hakua anafaulu uchumi lakini sera zake za uchumi ndio zinaongoza Duniani.

Nitaftie matokeo ya kina Elon Musk, Werren Buffet, Billy Gate, Obama, nk kama walikua wanakua wa kwanza darasani.

Sasa hao wnaokua na division 1 wamesove problem zipi? Hizi za hesabu ambazo problem na solution zilishataftwa miaka na miaka zipo? Una masihara.

Yaani kwamba tukipewa swali la x+y=2, mimi nikakosa na wewe ukapata basi wewe umetatua problem, problem ipi hapo?
 
Hakuna mvumbuzi ama mwanasayansi aliefanikiwa maishani ambae alikua anafauli mitihani. Einstein hakua mzuri kwenye mitihani ila mambo yake unayajua hata kama hujawahi kumuona, Galileo, Newton hawakuwahi kufanya mitihani.

John Keynes mchumi mkubwa Duniani hakua anafaulu uchumi lakini sera zake za uchumi ndio zinaongoza Duniani.

Nitaftie matokeo ya kina Elon Musk, Werren Buffet, Billy Gate, Obama, nk kama walikua wanakua wa kwanza darasani.

Sasa hao wnaokua na division 1 wamesove problem zipi? Hizi za hesabu ambazo problem na solution zilishataftwa miaka na miaka zipo? Una masihara.

Yaani kwamba tukipewa swali la x+y=2, mimi nikakosa na wewe ukapata basi wewe umetatua problem, problem ipi hapo?

Unakwenda kwenye extremes, unaongelea < 1% ya World population hiyo siyo representative, hapa naongelea > 95% ya World population na yes, High IQ ni kiashiria kikubwa cha mafanikio Duniani, kwa maana nyingine uwezekano wa kufanikiwa ukiwa na High IQ ni mkubwa zaidi kulinganisha na mtu wa wastani …
 
Unakwenda kwenye extremes, unaongelea < 1% ya World population hiyo siyo representative, hapa naongelea > 95% ya World population na yes, High IQ ni kiashiria kikubwa cha mafanikio Duniani, kwa maana nyingine uwezekano wa kufanikiwa ukiwa na High IQ ni mkubwa zaidi kulinganisha na mtu wa wastani …
High IQ unaipima kwa kufaulu mitihani?

High IQ inapimwa kwa kuvumbua suluhisho la matatizo yanayoikabili jamii, sio kukariri majibu ya mswali halafu uitwe kwamba una high IQ.

Okay, tuseme uko sahihi, Tanzania kila mwaka ina watu wanapata division 1 za 7 zaidi ya 100 na za 3 form six zaidi ya 100, hao wote zaidi ya 200 kila mwaka, hiyo high IQ yao imetusaidia kutatua changamoto zipi?

Mind you, kaka zangu 2 wamewahi kua kwenye top 10 ya kitaifa, wa kwanza alikua top 3 kitaifa mwaka 1995 akitokea Kibaha, mwingine mwaka 1998 akitokea Tabora boys. Halafu kuna mimi hapa nina 4 yangu ya 32 ila nina mafanikio makubwa kuliko hao vipanga wa nchi.

Tunachokisema, mfumo wa mitihani unaua ubunifu, uvumbuzi na uwezo wa wanafunzi kuchambua mambo. Wao wako conditioned kufaulu tu mitihani, kukariri maswali na majibu yake.

Ndio maana nchi kama Malaysia na nchi nyingine wameondoa hii grading system, wao wanakuandikia tu good, average or poor basi na hawasemi amekua wa ngapi darasani. Nchi nyingi na vyuo vingi wanaondoa hii old school grading system na kuweka alternative grading system ana assessment system.
 
High IQ unaipima kwa kufaulu mitihani?

High IQ inapimwa kwa kuvumbua suluhisho la matatizo yanayoikabili jamii, sio kukariri majibu ya mswali halafu uitwe kwamba una high IQ.

Okay, tuseme uko sahihi, Tanzania kila mwaka ina watu wanapata division 1 za 7 zaidi ya 100 na za 3 form six zaidi ya 100, hao wote zaidi ya 200 kila mwaka, hiyo high IQ yao imetusaidia kutatua changamoto zipi?

Mind you, kaka zangu 2 wamewahi kua kwenye top 10 ya kitaifa, wa kwanza alikua top 3 kitaifa mwaka 1995 akitokea Kibaha, mwingine mwaka 1998 akitokea Tabora boys. Halafu kuna mimi hapa nina 4 yangu ya 32 ila nina mafanikio makubwa kuliko hao vipanga wa nchi.

Tunachokisema, mfumo wa mitihani unaua ubunifu, uvumbuzi na uwezo wa wanafunzi kuchambua mambo. Wao wako conditioned kufaulu tu mitihani, kukariri maswali na majibu yake.

Ndiyo, hakuna kipimo kingine zaidi IQ testing, siyo kwamba kiko sahihi kwa 100% lkn ndicho pekee kinachotumika kupima Problem Solving Skills.

Dunia jinsi ilivyo ni kwamba Ufaulu mkubwa unakufikisha mbali, ukitaka kuwa daktari, engineer, Mwanasheria au karibia chochote kile kitu pekee unachoweza kuwa nacho kwanza ni ufaulu mzuri ili hata tu uweze kufikiriwa kwenye usaili wowote ule, na hii ni Dunia nzima.
 
Mimi elimu isiyo solve matatizo ni ujinga mtupu, hafu nchi hii kupata A sio kipimo Cha akili Kuna janja janja nyingi sana kwenye mambo mengi hasa Hawa private wanaofanya biashara, to me elimu inabidi I solve matatizo kwa jamii, when I was little nilikuwaga nafikiria ma Prof ndio watu wenye Akili kumbe hu crame mambo tu ya madesa ila ikija kwenye real life ni weupe watupu kichwani, so nchi hii kupima mtu kwa ufaulu as kulinganisha na IQ naona sio sahihi
 
Wakati tunazungumzia problem solving tusiangalie mega problems. Hawa pia ni problem solvers kwenye maeneo yao, be it kwenye familia zao.
Lakini pia hata huko wanakoajiriwa pia wanasolve problems.
Sisi sote tunao wajibu wa kuwaunganisha hawa wanaofaulu na zile skills za maisha pia.
Tunapokosea sisi ni kwamba tumetengeneza kama vile kufaulu ndo the end wakati inatakiwa ukiwa umefaulu ndo uanze sasa application ya vile ulivyojifunza. Tuwekeze sasa kwenye kuwapa mazoezi ya kutosha ya vile walivyojifunza.
 
Hilo ni swala lingine na ni tatizo la nchi kiujumla, lkn bado ukweli unabakia kuwa ukweli kwamba mtoto anayefaulu vizuri ( sana) ana nafasi kubwa ya kufanikiwa maishani kuliko yule wa wastani .
Kufanikiwa darasani hakuna uhusiano kabisa na kufanikiwa kimaisha. WafanyA biashara wengi walofanikiwa wala cyo watu walokuwa na ufaulu Sana,tena wengine hata shule hawakukanyaga. Hao ndo kutwa kucha wanawaajili vijana mnaosema wana IQ kubwa na kuwalipa mishahara ya kawaida. Kuna haja ya mtaala kubadilishwa ili ujikite katika kuendeleza vipaji na ubunifu badala ya kuendelea na utaratibu wa sasa ambapo mtahiniwa anapimwa uwezo Wa kukumbuka(memorization). Unakuta kijana anapata Physics "A", Chemistry A na Maths A (PCM) lakini mpaka sasa hajaisaidia nchi kutengeneza vijiti vya kusafishia meno/tooth pics. Likewise,vijana wa aina hiyo wameshindwa kutengeneza hata mashine ndogo ndogo za kumsaidia Mkulima katika kulima,kupanda Mbegu na hata kuvuna. Hao ma- genius wameishia kutembea na mabahasha ya khaki kuomba ajira kwa akina Musukuma na Kishimba!

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Ndiyo, hakuna kipimo kingine zaidi IQ testing, siyo kwamba kiko sahihi kwa 100% lkn ndicho pekee kinachotumika kupima Problem Solving Skills.

Dunia jinsi ilivyo ni kwamba Ufaulu mkubwa unakufikisha mbali, ukitaka kuwa daktari, engineer, Mwanasheria au karibia chochote kile kitu pekee unachoweza kuwa nacho kwanza ni ufaulu mzuri ili hata tu uweze kufikiriwa kwenye usaili wowote ule, na hii ni Dunia nzima.
Hii siyo kwa dunia nzima,hiyo ni kwa Tanzania tu. Nimepiga kazi migodini,vijana walofeli drs LA Saba walikuwa wanazalisha vizuri kuliko walokuwa na degree za miamba na madini toka kwenye hivyo vyuo vikuu vyenu. Kule "process plant" belt zinakatika muhitimu Wa PCM aliyejifunza Purrey system inavyofanya kazi anashindwa kwenda ku-replace belts mpaka std 7 ndo anamwondolea aibu. Mfumo wa Elimu yetu lazima tuubadili,Kama tunataka matokeo makubwa. Mpaka miaka 60 ya Uhuru,elimu yetu imeshindwa hata kuibua vipaji na kuwafanya vijana wawe wabunifu. Tumeshindwa kuendeleza vipaji vya kukimbia vya watoto umasaini ili wakashiriki Olympics na kuzoa pesa,hata vipaji vya kurusha mikuki na matufe(javelin),kuogelea nk.mfumo wa elimu yetu umeshindwa kuendeleza. Sasa mfumo umekalia kukaririsha watoto(memorization),then mnawaita ma-genius,,,thubutu,mnawajua genius!!? Akina Steve Jobs,Bill Gates hawa walisaidia dunia kuja na program mbali mbali za computer zilizosaidia urahisi katika utendaji kazi. Hao wanaokariri siyo genius,tafuteni Majina mengine ya kuwapa!

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Leo Baraza la mitihani limetangaza matokeo ya kidato cha 2,4 na mitihani ya ufahamu kwa wanafunzi wote waliofanya hiyo mitihani mwaka 2021.

Mwezi june 2022 itatutangazia matokeo ya form 6 pia kama kawaida ya miaka yote, kila mwaka ni matokeo ya ulinganifu wa nani kafanya vizuri na nani kafanya vibaya.

Kinachonisikitisha ni kwamba pamoja na udhaifu mkubwa sana wa huu mfumo wa elimu tulionao ambao bado unawaandaa wanafunzi kua waajiriwa, bado wazazi wengi kama sio wote wako na tamaa ya kuona watoto wao wanapata A ama B au Div 1 au 2.

Wote tunakubaliana kwamba huu mfumo wa kupima watu uelewa ama ufahamu wa kukabiliana na changamoto zinazowazunguka ni wa hovyo lakini bado wazazi wako very much obsessed na As. Pamoja na kwamba huu mfumo wa mitihani ni mbovu, unaua ubunifu, ugunduzi, uvumbuzi na uchambuzi wa masuala muhimu kwenye jamii lakini bado Tanzania yunaikumbatia na kuushadadia kwa kila hali.

Tujiulize, hao top 10 wa kitaifa wa kila mwaka, yaani Tanzania kila mwaka tunapata watu wenye akili kuliko wote 20, je hao ma genius hua wanasaidia nini taifa? Je wanakua na mchango gani kwa nchi? Utashangaa hao brainy ama geniuses 20 wa kila mwaka huishia kupewa kazi serikalini, kuajiriwa eitha kua waalimu vyuo vikuu ama maafisa wa kawaida wa serikali.

Dhana ya elimu ni kumpa mtu ufahamu, uelewa na ujuzi wa kukabiliana na changamoto na mazingira yanayomzunguka. Sasa hnajiuliza toka lini kupata elimu ikawa mashindano? Kwamba hata kutatua changamoto zinazotuzunguka tunazitatua kwa mashindano? Ama mtu akipata A basi yeye atatatua changamoto haraka zaidi na kwa ufanisi kuliko aliepata D? Mbona hatuoni faida za A ama Div 1 kwenye jamii?

Hivi 1 zilivyo nyingi kila mwaka sitegemei Tanzania bado tungekua na changamoto yoyote inayotuzunguka maana tuna geniuses wa kutosha.

Hii mada inaendelea.
Kusema div 1 au A nyingi hazina faida kwenye jamii kwa sababu wanaozipata hawatatui changamoto kibao zilizo kwenye jamii,ni upotofu wa fikra.
Ili utatue changamoto unahitaji zaidi ya div 1 na A,na Elimu ya ngazi tofauti.
Kutaka vijana wanapomaliza vyuo waende wakajiajiri wakati kwanza mifumo ya Serikali sio rafiki,mitaji hakuna,(kuanzisha blog au tovuti unatakiwa ulipe milioni moja).
Sio kuwatendea haki.hata kwenye nchi za ulimwengu wa kwanza,ulaya na US,sio hivyo wahitimu wakitoka vyuo wengi wao hutafuta kuajiliwa,Obama alisoma Havard,alipomaliza alianzisha kampuni gani?alifsnya shughuri za kijamii za kujitolea(zenye Malipo),akagombea useneta,mpaka kuwa Raisi.
Kama Swala la kujiajiri na kubuni fulsa ni rahisi kama unsvyolisema,Hawa mawaziri,wabunge wanaolipwa mkwanja mrefu mbona hawana makampuni au viwanda?maana mitaji wanayo!!!
Kwa uzoefu wangu inaweza ikakuchukua miaka 15 ukiwa kwenye ajira,mpaka ufike hatua ya kuweza kujiajiri,
Na hizo A unazoziponda,hizo ndio njia ya kukufikisha kwenye vyuo vikubwa,upate Elimu Bora ya juu,upate ajira world benk,baadae uanzishe kampuni kwa pesa.
KaMA Kijiajiri ni rahisi sana,tulitegemea vijana wanaohitimu Kwenye vyuo huko UK wasingepata tabu ya ajira,lakini wapi,kilichotokea wakati wa Brexit,waingereza wakiona raia wengine wa ulaya wanachukua ajira zao,ndio maana Brexit ikawa na msukumo mkubwa.
UnahitAJi As na ones kusoma kozi kama za IT na computer,n kwa vile Kuna ushindsni mkubwa,hizo passmark ni muhimu
 
Hii siyo kwa dunia nzima,hiyo ni kwa Tanzania tu. Nimepiga kazi migodini,vijana walofeli drs LA Saba walikuwa wanazalisha vizuri kuliko walokuwa na degree za miamba na madini toka kwenye hivyo vyuo vikuu vyenu. Kule "process plant" belt zinakatika muhitimu Wa PCM aliyejifunza Purrey system inavyofanya kazi anashindwa kwenda ku-replace belts mpaka std 7 ndo anamwondolea aibu. Mfumo wa Elimu yetu lazima tuubadili,Kama tunataka matokeo makubwa. Mpaka miaka 60 ya Uhuru,elimu yetu imeshindwa hata kuibua vipaji na kuwafanya vijana wawe wabunifu. Tumeshindwa kuendeleza vipaji vya kukimbia vya watoto umasaini ili wakashiriki Olympics na kuzoa pesa,hata vipaji vya kurusha mikuki na matufe(javelin),kuogelea nk.mfumo wa elimu yetu umeshindwa kuendeleza. Sasa mfumo umekalia kukaririsha watoto(memorization),then mnawaita ma-genius,,,thubutu,mnawajua genius!!? Akina Steve Jobs,Bill Gates hawa walisaidia dunia kuja na program mbali mbali za computer zilizosaidia urahisi katika utendaji kazi. Hao wanaokariri siyo genius,tafuteni Majina mengine ya kuwapa!

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
Kwa jinsi ulivyoandika,hata Elimu ya chuo kikuu huna,hao darasa la saba unaowasema kwamba wapo vzr kwenye kazi kuriko walitoka vyuoni,hayo wanayoyajua walisomea huko darasa la saba au walijifunzia hapo mgodini!!
Wengi wao waliingia migodini wakiwa hawajuhi kitu,wamepata uzoefu kwa kufsnya kazi kama maroboti na kukalili,wengi tumekutana nao makazini,huwa wanajifsnya wajuaji sana,vyuoni wanatoa taaluma,huwezi kumchukua engineer aliyetoka chuoni leo,umpeleke afunge transformer ya umeme,au atrngeneze service line ya nyumba,sasa kwa vile darasa la saba kafanya kazi ya kibsrua kwa muda mrefu anajua taratibu nyingi,huwezi kusema huyu std 7 ni bora kuliko mhitimu wa chuo,huyo std 7anaweza kupiga mahesabu ya kudesign hiyo transformer au,kufsnya analyse ya huo mtsmbo kama unatumia umeme vzr,au unakaribia kuhsribika?hizo power logger tools anaweza kuzitumia??
Kama umepita Elimu ya juu,Kuna kitu kinaitwa mafunzo viwandani,vijana huwa wanaperekwa kupata uzoefu,hayo ndio yaongezwe,
Yaani Elimu ya std 7 ni bora kuliko ya chuo kwa vile tu huyu kijana wa lasaba ameweza kufunga fan belt kuliko wa chuo???!!,realy!!ur fucking kidding me
 
Naona tangia jana watu wanakuja na mada tofauti tofauti mara waliopata division 1 wanaajiriwa na division 3 or 4,mara private schools zinaiba paper,leo naona huyu mtoa mada kaja na thread hii but je MTOA MADA UNATAKA WATU WASISOME ?WEWE ACHA MAMBO YAENDELEE KAMA YALIVYO aliyepata Division 1 au 0 kila mtu atajijua mbele ya safari yake ya maisha aliyopangiwa na Mungu
 
Kila Mtu afanye jambo lenye maslahi kwake kwanza...then jamii inayomzunguka, then Taifa then Dunia ( watu wote)
Hivi ndivyo Empedocles Concentric cycles kwenye Stoic philosophy zinatufundisha

Turudi kwenye mada
Lakini Hawa TOs ni utopolo tu hakuna lolote!

Mtu unakariri mambo then useme wewe jembe
Majembe ni wale wanaoconceptualize vitu vipya na kuleta au kubadili vitu...

Kushangilia Mtu ati TO ni ushamba kama ushamba mwengine.

Kuwa na uwezo wa Kurun mambo na kunavigate life mtaani ndo kipaji chenyewe iko.

Hawa vijana wape pepa ambalo linapima ufahamu unambie wengi ni Mbulula tu, si tunawafahamu!

Akili ni kuona mbele hata miaka arobaini kuanza sasa, kuweka plan, kuanzisha business na kuibembeleza ikue, kuona opportunity anywhere na kuikamata,kuwa mtu huru, kumaster mahisia na haya ndiyo mambo ya msingi ambayo shuleni hayafundishwi siyo Kushangilia UTOPOLO eti TO!
 
Kwa jinsi ulivyoandika,hata Elimu ya chuo kikuu huna,hao darasa la saba unaowasema kwamba wapo vzr kwenye kazi kuriko walitoka vyuoni,hayo wanayoyajua walisomea huko darasa la saba au walijifunzia hapo mgodini!!
Wengi wao waliingia migodini wakiwa hawajuhi kitu,wamepata uzoefu kwa kufsnya kazi kama maroboti na kukalili,wengi tumekutana nao makazini,huwa wanajifsnya wajuaji sana,vyuoni wanatoa taaluma,huwezi kumchukua engineer aliyetoka chuoni leo,umpeleke afunge transformer ya umeme,au atrngeneze service line ya nyumba,sasa kwa vile darasa la saba kafanya kazi ya kibsrua kwa muda mrefu anajua taratibu nyingi,huwezi kusema huyu std 7 ni bora kuliko mhitimu wa chuo,huyo std 7anaweza kupiga mahesabu ya kudesign hiyo transformer au,kufsnya analyse ya huo mtsmbo kama unatumia umeme vzr,au unakaribia kuhsribika?hizo power logger tools anaweza kuzitumia??
Kama umepita Elimu ya juu,Kuna kitu kinaitwa mafunzo viwandani,vijana huwa wanaperekwa kupata uzoefu,hayo ndio yaongezwe,
Yaani Elimu ya std 7 ni bora kuliko ya chuo kwa vile tu huyu kijana wa lasaba ameweza kufunga fan belt kuliko wa chuo???!!,realy!!ur fucking kidding me
Mkuu nina mashaka kama ulisoma hata darasa la kwanza. Hujui tofauti ya A na H, wewe, Hujuhi, Hajuhi, Hamina, Hajira, Akuna, Aji, Hamekwenda nk.

Pia uwe unaweka aya. Mwisho zaidi kila kwenye nukta unaanza na nafasi na herufi kubwa.

Utashangaa ulisoma ukafika chuo kikuu lakini writing skills zero ila ulikariri majibu ukafika chuo kikuu.

Ndio maana tunasema huu mfumo wa elimu ni mbovu unazalisha watu wabovu kama wewe wenye vyeti vizuri.
 
Back
Top Bottom