Sol de Mayo
JF-Expert Member
- Sep 10, 2016
- 6,324
- 5,934
Unaweza leta ushahidi hapa Tanzania ama ukanda wetu huu wa waarabu kutesa watu? Waarabu wengi hasa hao wa Oman munaowasema humu,
1. Oman ni nchi Tajiri wao wanaingiza hela za kigeni na hawatoi utajiri wa nchi kwenda nje
2. Hutasikia scandal za ufisadi toka kwao na wana matajiri kibao
3. Biashara zao ni zile zinazoongeza welfare kwa watu
4. Nadra kuikuta wameshtakiwa ama kufanya crime mbalimbali
5. Shule zao ama miradi yao ni katika iliyo bora kabisa nchi hii.
Kifupi mkuu ni watu ambao wapo respected kwenye jamii zao, ndio maana unakuta waarabu wapo pwani miaka na Miaka hawachukiwi na wazawa wa pwani.
Nenda bara sasa, unakuta mtu si yeye wala baba yake wala babu yake alieishi na mwarabu ila ndio Ana chuki 99%, hajui hata anaongea nini,
Chuki imewakaa kwenye damu tayari, ila wapo baadhi wanajitambua. Na mbaya zaidi wanaendelea kukaririshana kwa watoto, wajukuu mpaka watukuu. Mtihani sana hawa watu mkuu.
Hutoelewa waulize wanaofanya kazi nje huku kwenye nchi za kiarabu hutoamini utakachosikia afu si weupe wote ni wabaya kuna wabaya na wazuri pia
Hicho kitu sijakishuhudia bali nakisikia tuu, hivyo siwezi kuwajaji ilhali hakuna ushahidi wowote. Na swala la unyanyasaji mbona lipo kila mahala a na hamsemi, especially huku kwetu kwa mabinti wa kazi,, sio hayo tuu na ukatili upo tena wa kinyama kabisa lakini mnajitoa ufahamu.
👇
Albino wanakatwa viungo huu sio ukatili?
Vikongwe wanauliwa huu sio ukatili?
Baba anauwa mwanae kwa maagizo ya mganga wake ili atajirike huu sio ukatili?
Wafanyakazi wa ndani wanavyoteswa na waafrika wenzao, na wengine kuuawa huu sio ukatili? Refer yaliyotokea dar yule mdada kauawa dhidi ya madam wake
Mwizi anachomwa moto huu sio ukatili?
Wa boda boda kuchinjwa, kupigwa nyundo za kichwa n.k huu sio ukatili?
Wake kwa waume wanakatana mapanga kisa mapenzi, mali n.k huu sio ukatili?
Watu wanauana kisa hela ndogo, huu sio ukatili?
Wanawake wanauawa na kunyofolewa sehemu za siri kisa upate utajiri wa haraka, huu sio ukatili?
Ubakaji, huu sio ukatili/unyanyasaji?
Tarime watu wanauana kisa mashamba, wanawake, mali n.k huu sio ukatili?
Waendelee na wengine kuorodhesha ukatili wa huku........list bado inaendelea. Ila wewe umekuja na chuki zako hapa, na kulalia kwa waarabu tu, ya kwako huyaoni!!