Kwanini Watanzania tusianze massive constructions of apartments nchi nzima?

Kwanini Watanzania tusianze massive constructions of apartments nchi nzima?

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
5,894
Reaction score
11,786
Kusema ukweli Tanzania tunahitaji apartments kwa sasa. Kwa nini tusijifunze kutoka kwa nchi kama China, South Korea, Singapore nk? Hizi nchi watu wake walikuwa wanaishi kwenye makazi duni sana miaka ya 1960s. Serikali zao zikaanza ujenzi wa apartments ili kuhakikisha wananchi wengi wanapata kuishi kwenye makazi bora. Na leo hii wamefanikiwa, watu wanaishi kwenye makazi mazuri
Nasema hivi kwa sababu clearly hii ya kila mtu kujenga nyumba yake mwenyewe imetushinda. Watu wasijenge nyumba mpaka wajipate, kipindi wanajitafuta wakae kwenye apartments za serikali au kampuni binafsi
NHC wanajenga apartments Dodoma na hata Dar tumeona miradi kama Kawe 711 na Samia Housing Scheme lakini kusema ukweli hii hata haitasaidia kitu. Nyumba za NHC huwa ni expensive ndio maana wanaishia kukaa wahindi na waarabu. Inapaswa zijengwe apartments na bei ziwe rafiki kwa Watanzania wa kawaida ili kupunguza makazi holela, sio hizi za NHC ambazo bei zake Wana afford foreigners tu. Na hata Watanzania wanao afford ni mara kumi wajenge nyumba zao wenyewe maana watapata nyumba nzuri zaidi

Take a look at this

Hapa ni Mbeya
mbeya-tanzania-drone-view-to-city-in-africa-2NAJPB2.jpg

Umeona jinsi nyumba zilivyojengwa bila mpangilio na kuchukua ardhi kubwa bila sababu za msingi? Lakini kama zingejengwa apartment kadhaa, zikapandwa nyasi, miti, mitaro na sewage system mazingira yangekuwa mazuri zaidi ya hivi. Matatizo kama mafuriko, kipindupindu, maeneo kutofikika nk yangepungua na mji ungependeza kimuonekano

Hapa ni Dar
sesq2fk39ga71.jpg

Angalia hicho kipande kidogo kilichojengwa hovyo bila mpangilio
Na hapa pia ni Dar 👇
1770876634409.jpg

.
.

Hapa ni Mwanza
Screenshot_20260215-160426.png

Hawa watu wote wanaoishi kwenye nyumba zinazoonekana kwenye picha wangetosha kama wangekaa kwenye apartment moja pekee.

Kuzuia mambo kama haya ndio maana Wachina waliamua kujenga apartments nyingi nchi nzima

KWA NINI WACHINA WALIAMUA KUJENGA APARTMENTS NYINGI NCHI NZIMA?

Hapa sababu zote zipo applicable hata hapa Tanzania

1. Ukuaji wa haraka wa idadi ya watu na mijini
China ina miji mikubwa yenye watu wengi. Kwa sababu ya uhamiaji mkubwa kutoka vijijini kwenda mijini (urbanization), kuna hitaji kubwa la makazi. Apartments ni suluhisho linaloweza kuchukua watu wengi katika eneo dogo. Ni kama tu hapa Tanzania (Jiji la Dar lina watu takribani milioni 5.3, Jiji la Mwanza watu milioni 1, majiji ya Arusha, Dodoma na Mbeya yana watu takribani laki 6 each)

2. Ufanisi wa ardhi na rasilimali
Ardhi mjini ni ya thamani kubwa. Kujenga nyumba za ghorofa nyingi (high-rise apartments) kunaruhusu kutumia ardhi kidogo lakini kufikia idadi kubwa ya familia.

3. Kurekebisha gharama za makazi
Apartments nyingi kwa mpango mmoja (mass housing) zinafanya gharama ya kila nyumba kuwa nafuu zaidi kuliko kujenga nyumba binafsi. Serikali pia inaweza kudhibiti bei za nyumba kwa urahisi zaidi.
skynews-china-real-estate_6632074.jpg

4. Kurahisisha huduma za kijamii
Wakati watu wengi wakiishi karibu kwenye buildings za makazi, ni rahisi kutoa huduma kama barabara, maji, umeme, shule, hospitali, na usafishaji wa miji.


FAIDA ZA SERIKALI KUJENGA APARTMENT NYINGI TANZANIA NZIMA
1. Bei nafuu kwa wananchi wa kawaida: Serikali inasaidia baadhi ya gharama, hivyo ni rahisi kwa watu wenye kipato cha kati au kidogo. Kuliko kujichanga na kujenga nyumba ambazo ni below standard ni heri mwananchi apange kwenye apartment za bei nafuu

2. Mpango wa usafi na afya
Miji mipya inafanyiwa urban planning, hivyo barabara, mifereji ya maji, na taka zinapangwa vizuri. Kuliko mazingira ya uswazi. Mpangilio mbovu una attract uchafu, watu wanatupa taka hovyo na hawaoni aibu kwa sababu mazingira yenyewe hayavutii. Hii ni human psychology (Broken window theory)
1fae2920e57f10147bb20b54cded75f021e1d903.jpeg

3. Usalama
Blocks za apartments mara nyingi zina milango ya kudhibiti, CCTV, na wakaguzi wa usalama. Ukiangalia nchi zote ambazo wananchi wake wanaishi sana kwenye apartment ndio zinaongoza kwa usalama duniani (China, South Korea, Japan, Singapore)
images (1).jpeg

4. Huduma zinakuwa karibu
Shule, maduka, vituo vya afya na maegesho ya umma mara nyingi vipo ndani ya maeneo hayo.

MUUNDO NA MPANGILIO WA MITAA YA APARTMENTS KWA AJILI YA WANANCHI CHINA (Chinese residential neighborhoods)
gettyimages-169355688.jpeg

1. Apartments zinaunganishwa na barabara pana za magari na njia za watembea kwa miguu.

2. Zinajengewa bustani ndogo, miti, na maeneo ya michezo kwa watoto.

3. Urban planning
Kila block ina eneo lake la park, shule, soko, frame za maduka ya msingi karibu nk
image.jpg

4. Mfumo wa maji na umeme umewekwa ili kuepuka matatizo ya usafi na msongamano.

5. Kunakuwa na njia za baiskeli na barabara za watembea kwa miguu

Kwa sababu ni housing mass-production, bei inabakia chini kuliko nyumba binafsi.
Apartments ndogo zina bei nafuu zaidi, zinazofaa kwa vijana, wafanyakazi wa maofisini, familia zinazojitafuta, na hata zilizojipata

hcpc82y4gme71.jpg

Mitaa ya apartments inavyokuwa, unaweza kukuta residential compounds yenye ghorofa 10–30.
Kila block ina green space: miti midogo, bustani za michezo, na sehemu za kukaa.
Njia za barabara haziwezi kuwa na msongamano mkubwa kwa sababu zoning imepangwa vizuri: makazi, biashara, na huduma za jamii hazichanganyiki bila mpangilio.
20241102_FNP501.jpg
107187824-1675323493114-gettyimages-1246264784-China_Real_Estate_Market.jpeg

Hizi apartments ndio zimesaidia China kutokuwa na mitaa ya hovyo kama ya hapa kwetu Tanzania. Apartments ni better option ya makazi
Fikiria nchi kama USA Ina uchumi mkubwa kuliko China na Ina watu wachache kuliko China (China Ina watu bilioni 1.4, USA Ina watu milioni 350) lakini USA ina homeless people wengi kuliko China. That means Chinese way is more effective
Hapa Tanzania nako homeless sio wengi lakini sasa watu wanakaa kwenye makazi dunia. Ni muda sasa tuanze kujenga apartments nyingi kila kona ya Tanzania ili watu wakae kwenye nyumba nzuri. Kodi ziwe chini na sisi nchi yetu ipendeze, tupunguze urban sprawl, na matumizi ya ardhi yasiyo ya lazima.
NHC waache kujengea nyumba wahindi na waarabu, waweke bei rafiki ili Watanzania waone sababu za kuhamia kwenye apartments.
Wala sio lazima ziwe apartments ndefu kama za China. Huku hata zikijengwa za urefu wa 5 floors each inatosha
Maana hii hali sio nzuri 👇
1770876634409.jpg
 
Idea yako nzuri,
labda mbadilishane na wazungu yani waafrica wote muende mabara mengine na Africa waje wazungu ndio kitu ya namna hio inaweza kutokea
Hii hata Watanzania wenyewe tunaweza kufanya.
Hii ni South Africa
new-township-kwazulu-natal-south-africa-JJ0R87.jpg

SA-houses.jpg

.
.
Hii ni Burkina Faso
photo-2024-07-17-13-14-22ouedoabk.jpg
.
.
Hapa ni Angola
FB_IMG_1771164412058.jpg

.
.
Na hapa ni Tanzania (Kawe 711) project. Tatizo hizi za NHC huwa ni expensive, wana tamaa wanataka faida irudi ndani ya miaka 5 sijui. Tukijipush tunaweza kuanza kujenga kwa lengo la kupunguza makazi duni lakini we're not serious enough
Screenshot_20260215-170804.png
 
Ukiwa na watoto apartments si sehemu nzuri ya malezi
Zanzibar sasahivi wanajenga apartments na Hussein Mwinyi ameeleza vizuri faida zake na kuwa lengo lao ni kupunguza makazi duni. Ni serious project kuliko hizi za huku Tanzania bara ambazo lengo lao ni biashara na sio kupunguza makazi duni
Wachina na Wakorea wanaishi kwenye apartments wengi wao na watoto wao wana malezi mazuri tu.
Pia sio lazima ziwe apartments ndefu, zinaweza kuwa hata za ghorofa 1 au 2 hadi 5
Na pia kunakuwa na ujenzi wa maeneo kama haya pia. Hii ni South Africa, linakuwa chaguo la watu ambao hawataki apartments. Ni bora hivi kuliko uswazi
new-township-kwazulu-natal-south-africa-JJ0R87.jpg


.
Fananisha na hapa Mbeya
mbeya-tanzania-drone-view-to-city-in-africa-2NAJPB2.jpg
 
Tatizo hatuna watu wa mipango miji ,tatizo viongozi ni wabinafsi wanajiangalia wao tu ,hawana plani ya miaka 100 ijayo ,nyumba za chini ni matumizi mabaya ya ardhi....USA wana Housing Projects za kutosha ,matajiri wachache ndiyo wanaishi kwenye nyumba zao ila wengi wanaishi kwenye Projects.

Kuna mbunge alitoa wazo la kuvunja slams zote wajenge maghorofa tu Skyscappers ,sehemu kama Manzese ,Kigogo ,Tandale ,sinza ,Knyama .K /mkwajuni na sehemu karibu na town wavunje pote pale wafanya land scaping ya maana ,drainage and sewage sytem znuri kisha waporomoshe ma skyscappers itakuwa unyama sana.
 
Zanzibar sasahivi wanajenga apartments na Hussein Mwinyi ameeleza vizuri faida zake na kuwa lengo lao ni kupunguza makazi duni. Ni serious project kuliko hizi za huku Tanzania bara ambazo lengo lao ni biashara na sio kupunguza makazi duni
Wachina na Wakorea wanaishi kwenye apartments wengi wao na watoto wao wana malezi mazuri tu.
Pia sio lazima ziwe apartments ndefu, zinaweza kuwa hata za ghorofa 1 au 2 hadi 5
Na pia kunakuwa na ujenzi wa maeneo kama haya pia. Hii ni South Africa, linakuwa chaguo la watu ambao hawataki apartments. Ni bora hivi kuliko uswazi
View attachment 3544391

.
Fananisha na hapa Mbeya
View attachment 3544394
Sawa alizungumza ivo lakini unajua bei za hizo apartments? Na unazijua zikoje? Mwanasheria wangu anaumwa
 
Tatizo hatuna watu wa mipango miji ,tatizo viongozi ni wabinafsi wanajiangalia wao tu ,hawana plani ya miaka 100 ijayo ,nyumba za chini ni matumizi ya ardhi....USA wana Housing Projects za kutosha ,matajiri wachache ndiyo wanaishi kwenye nyumba zao ila wengi wanaishi kwenye Projects.

Kuna mbunge alitoa wazo la kuvunja slams zote wajenge maghorofa tu Skyscappers ,sehemu kama Manzese ,Kigogo ,Tandale ,sinza ,Knyama .K /mkwajuni na sehemu karibu na town wavunje pote pale wafanya land scaping ya maana ,drainage and sewage sytem znuri kisha waporomoshe ma skyscappers itakuwa unyama sana.
USA Wana housing projects za kutosha yeah. Sema wao uchumi wao upo vizuri waka prioritize nyumba kubwa sana na expensive ndio maana ukiwa na kipato kidogo unakuwa homeless
USA licha ya kuwa na homeless people wengi lakini wanaoishi kwenye nyumba nzuri ni wengi zaidi. Asilimia kubwa ya Wamarekani wanakaa kwenye nyumba nzuri kuliko hata China
All in all housing projects kama za USA au China ni nzuri kuliko huu ujenzi holela wa huku Tanzania wa kutaka kila mtu awe na nyumba yake, halafu uwezo wa kujenga decent house hana
 
Sawa alizungumza ivo lakini unajua bei za hizo apartments? Na unazijua zikoje? Mwanasheria wangu anaumwa
Basi hapo ndio shida ilipo. Bei ndio shida. Kwani wakijenga apartments halafu faida wakaja kupata baada ya miaka 30 au 40 shida iko wapi? Watenge budget hata Trilioni 2 kila mwaka za kujenga makazi bora kwa watu wengi. Makazi ni long term investment, ni tofauti sana na hapa kwetu Tz ambako NHC wanajenga Leo halafu ndani ya miaka 5 wanataka faida yote irudi
 
Tatizo hatuna watu wa mipango miji ,tatizo viongozi ni wabinafsi wanajiangalia wao tu ,hawana plani ya miaka 100 ijayo ,nyumba za chini ni matumizi ya ardhi....USA wana Housing Projects za kutosha ,matajiri wachache ndiyo wanaishi kwenye nyumba zao ila wengi wanaishi kwenye Projects.

Kuna mbunge alitoa wazo la kuvunja slams zote wajenge maghorofa tu Skyscappers ,sehemu kama Manzese ,Kigogo ,Tandale ,sinza ,Knyama .K /mkwajuni na sehemu karibu na town wavunje pote pale wafanya land scaping ya maana ,drainage and sewage sytem znuri kisha waporomoshe ma skyscappers itakuwa unyama sana.
Sahihi huyo mbunge nadhani alikuwa ni Selemani Jafo
Idea yake waifanyie kazi tena Tanzania nzima sio Dar tu. Huu ujenzi holela umezidi sasa
 
Kusema ukweli Tanzania tunahitaji apartments kwa sasa. Kwa nini tusijifunze kutoka kwa nchi kama China, South Korea, Singapore nk? Hizi nchi watu wake walikuwa wanaishi kwenye makazi duni sana miaka ya 1960s. Serikali zao zikaanza ujenzi wa apartments ili kuhakikisha wananchi wengi wanapata kuishi kwenye makazi bora. Na leo hii wamefanikiwa, watu wanaishi kwenye makazi mazuri
Nasema hivi kwa sababu clearly hii ya kila mtu kujenga nyumba yake mwenyewe imetushinda. Watu wasijenge nyumba mpaka wajipate, kipindi wanajitafuta wakae kwenye apartments za serikali au kampuni binafsi
NHC wanajenga apartments Dodoma na hata Dar tumeona miradi kama Kawe 711 na Samia Housing Scheme lakini kusema ukweli hii hata haitasaidia kitu. Nyumba za NHC huwa ni expensive ndio maana wanaishia kukaa wahindi na waarabu. Inapaswa zijengwe apartments na bei ziwe rafiki kwa Watanzania wa kawaida ili kupunguza makazi holela, sio hizi za NHC ambazo bei zake Wana afford foreigners tu. Na hata Watanzania wanao afford ni mara kumi wajenge nyumba zao wenyewe maana watapata nyumba nzuri zaidi

Take a look at this

Hapa ni Mbeya
View attachment 3544366
Umeona jinsi nyumba zilivyojengwa bila mpangilio na kuchukua ardhi kubwa bila sababu za msingi? Lakini kama zingejengwa apartment kadhaa, zikapandwa nyasi, miti, mitaro na sewage system mazingira yangekuwa mazuri zaidi ya hivi. Matatizo kama mafuriko, kipindupindu, maeneo kutofikika nk yangepungua na mji ungependeza kimuonekano

Hapa ni Dar
View attachment 3544367
Angalia hicho kipande kidogo kilichojengwa hovyo bila mpangilio
Na hapa pia ni Dar 👇
View attachment 3544369
.
.

Hapa ni MwanzaView attachment 3544368
Hawa watu wote wanaoishi kwenye nyumba zinazoonekana kwenye picha wangetosha kama wangekaa kwenye apartment moja pekee.

Kuzuia mambo kama haya ndio maana Wachina waliamua kujenga apartments nyingi nchi nzima

KWA NINI WACHINA WALIAMUA KUJENGA APARTMENTS NYINGI NCHI NZIMA?

Hapa sababu zote zipo applicable hata hapa Tanzania

1. Ukuaji wa haraka wa idadi ya watu na mijini
China ina miji mikubwa yenye watu wengi. Kwa sababu ya uhamiaji mkubwa kutoka vijijini kwenda mijini (urbanization), kuna hitaji kubwa la makazi. Apartments ni suluhisho linaloweza kuchukua watu wengi katika eneo dogo. Ni kama tu hapa Tanzania (Jiji la Dar lina watu takribani milioni 5.3, Jiji la Mwanza watu milioni 1, majiji ya Arusha, Dodoma na Mbeya yana watu takribani laki 6 each)

2. Ufanisi wa ardhi na rasilimali
Ardhi mjini ni ya thamani kubwa. Kujenga nyumba za ghorofa nyingi (high-rise apartments) kunaruhusu kutumia ardhi kidogo lakini kufikia idadi kubwa ya familia.

3. Kurekebisha gharama za makazi
Apartments nyingi kwa mpango mmoja (mass housing) zinafanya gharama ya kila nyumba kuwa nafuu zaidi kuliko kujenga nyumba binafsi. Serikali pia inaweza kudhibiti bei za nyumba kwa urahisi zaidi.
View attachment 3544376
4. Kurahisisha huduma za kijamii
Wakati watu wengi wakiishi karibu kwenye buildings za makazi, ni rahisi kutoa huduma kama barabara, maji, umeme, shule, hospitali, na usafishaji wa miji.


FAIDA ZA SERIKALI KUJENGA APARTMENT NYINGI TANZANIA NZIMA
1. Bei nafuu kwa wananchi wa kawaida: Serikali inasaidia baadhi ya gharama, hivyo ni rahisi kwa watu wenye kipato cha kati au kidogo. Kuliko kujichanga na kujenga nyumba ambazo ni below standard ni heri mwananchi apange kwenye apartment za bei nafuu

2. Mpango wa usafi na afya
Miji mipya inafanyiwa urban planning, hivyo barabara, mifereji ya maji, na taka zinapangwa vizuri. Kuliko mazingira ya uswazi. Mpangilio mbovu una attract uchafu, watu wanatupa taka hovyo na hawaoni aibu kwa sababu mazingira yenyewe hayavutii. Hii ni human psychology (Broken window theory)
View attachment 3544375
3. Usalama
Blocks za apartments mara nyingi zina milango ya kudhibiti, CCTV, na wakaguzi wa usalama. Ukiangalia nchi zote ambazo wananchi wake wanaishi sana kwenye apartment ndio zinaongoza kwa usalama duniani (China, South Korea, Japan, Singapore)
View attachment 3544377
4. Huduma zinakuwa karibu
Shule, maduka, vituo vya afya na maegesho ya umma mara nyingi vipo ndani ya maeneo hayo.

MUUNDO NA MPANGILIO WA MITAA YA APARTMENTS KWA AJILI YA WANANCHI CHINA (Chinese residential neighborhoods)
View attachment 3544372
1. Apartments zinaunganishwa na barabara pana za magari na njia za watembea kwa miguu.

2. Zinajengewa bustani ndogo, miti, na maeneo ya michezo kwa watoto.

3. Urban planning
Kila block ina eneo lake la park, shule, soko, frame za maduka ya msingi karibu nk
View attachment 3544373
4. Mfumo wa maji na umeme umewekwa ili kuepuka matatizo ya usafi na msongamano.

5. Kunakuwa na njia za baiskeli na barabara za watembea kwa miguu

Kwa sababu ni housing mass-production, bei inabakia chini kuliko nyumba binafsi.
Apartments ndogo zina bei nafuu zaidi, zinazofaa kwa vijana, wafanyakazi wa maofisini, familia zinazojitafuta, na hata zilizojipata

View attachment 3544374
Mitaa ya apartments inavyokuwa, unaweza kukuta residential compounds yenye ghorofa 10–30.
Kila block ina green space: miti midogo, bustani za michezo, na sehemu za kukaa.
Njia za barabara haziwezi kuwa na msongamano mkubwa kwa sababu zoning imepangwa vizuri: makazi, biashara, na huduma za jamii hazichanganyiki bila mpangilio.
View attachment 3544378View attachment 3544379
Hizi apartments ndio zimesaidia China kutokuwa na mitaa ya hovyo kama ya hapa kwetu Tanzania. Apartments ni better option ya makazi
Fikiria nchi kama USA Ina uchumi mkubwa kuliko China na Ina watu wachache kuliko China (China Ina watu bilioni 1.4, USA Ina watu milioni 330) lakini USA ina homeless people wengi kuliko China. That means Chinese way is more effective
Hapa Tanzania nako homeless sio wengi lakini sasa watu wanakaa kwenye makazi dunia. Ni muda sasa tuanze kujenga apartments nyingi kila kona ya Tanzania ili watu wakae kwenye nyumba nzuri. Kodi ziwe chini na sisi nchi yetu ipendeze, tupunguze urban sprawl, na matumizi ya ardhi yasiyo ya lazima.
NHC waache kujengea nyumba wahindi na waarabu, waweke bei rafiki ili Watanzania waone sababu za kuhamia kwenye apartments.
Wala sio lazima ziwe apartments ndefu kama za China. Huku hata zikijengwa za urefu wa 5 floors each inatosha
Maana hii hali sio nzuri 👇View attachment 3544369
Inawezekana ila gharama atalipia nani?

Jambo la msingi sio kutibu dalili Bali kinga ya ugonjwa.

Plots zote zipimwe kusiwe na ujenzi holela
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom