Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 5,894
- 11,786
Kusema ukweli Tanzania tunahitaji apartments kwa sasa. Kwa nini tusijifunze kutoka kwa nchi kama China, South Korea, Singapore nk? Hizi nchi watu wake walikuwa wanaishi kwenye makazi duni sana miaka ya 1960s. Serikali zao zikaanza ujenzi wa apartments ili kuhakikisha wananchi wengi wanapata kuishi kwenye makazi bora. Na leo hii wamefanikiwa, watu wanaishi kwenye makazi mazuri
Nasema hivi kwa sababu clearly hii ya kila mtu kujenga nyumba yake mwenyewe imetushinda. Watu wasijenge nyumba mpaka wajipate, kipindi wanajitafuta wakae kwenye apartments za serikali au kampuni binafsi
NHC wanajenga apartments Dodoma na hata Dar tumeona miradi kama Kawe 711 na Samia Housing Scheme lakini kusema ukweli hii hata haitasaidia kitu. Nyumba za NHC huwa ni expensive ndio maana wanaishia kukaa wahindi na waarabu. Inapaswa zijengwe apartments na bei ziwe rafiki kwa Watanzania wa kawaida ili kupunguza makazi holela, sio hizi za NHC ambazo bei zake Wana afford foreigners tu. Na hata Watanzania wanao afford ni mara kumi wajenge nyumba zao wenyewe maana watapata nyumba nzuri zaidi
Take a look at this
Hapa ni Mbeya
Umeona jinsi nyumba zilivyojengwa bila mpangilio na kuchukua ardhi kubwa bila sababu za msingi? Lakini kama zingejengwa apartment kadhaa, zikapandwa nyasi, miti, mitaro na sewage system mazingira yangekuwa mazuri zaidi ya hivi. Matatizo kama mafuriko, kipindupindu, maeneo kutofikika nk yangepungua na mji ungependeza kimuonekano
Hapa ni Dar
Angalia hicho kipande kidogo kilichojengwa hovyo bila mpangilio
Na hapa pia ni Dar 👇
.
.
Hapa ni Mwanza
Hawa watu wote wanaoishi kwenye nyumba zinazoonekana kwenye picha wangetosha kama wangekaa kwenye apartment moja pekee.
Kuzuia mambo kama haya ndio maana Wachina waliamua kujenga apartments nyingi nchi nzima
KWA NINI WACHINA WALIAMUA KUJENGA APARTMENTS NYINGI NCHI NZIMA?
Hapa sababu zote zipo applicable hata hapa Tanzania
1. Ukuaji wa haraka wa idadi ya watu na mijini
China ina miji mikubwa yenye watu wengi. Kwa sababu ya uhamiaji mkubwa kutoka vijijini kwenda mijini (urbanization), kuna hitaji kubwa la makazi. Apartments ni suluhisho linaloweza kuchukua watu wengi katika eneo dogo. Ni kama tu hapa Tanzania (Jiji la Dar lina watu takribani milioni 5.3, Jiji la Mwanza watu milioni 1, majiji ya Arusha, Dodoma na Mbeya yana watu takribani laki 6 each)
2. Ufanisi wa ardhi na rasilimali
Ardhi mjini ni ya thamani kubwa. Kujenga nyumba za ghorofa nyingi (high-rise apartments) kunaruhusu kutumia ardhi kidogo lakini kufikia idadi kubwa ya familia.
3. Kurekebisha gharama za makazi
Apartments nyingi kwa mpango mmoja (mass housing) zinafanya gharama ya kila nyumba kuwa nafuu zaidi kuliko kujenga nyumba binafsi. Serikali pia inaweza kudhibiti bei za nyumba kwa urahisi zaidi.
4. Kurahisisha huduma za kijamii
Wakati watu wengi wakiishi karibu kwenye buildings za makazi, ni rahisi kutoa huduma kama barabara, maji, umeme, shule, hospitali, na usafishaji wa miji.
FAIDA ZA SERIKALI KUJENGA APARTMENT NYINGI TANZANIA NZIMA
1. Bei nafuu kwa wananchi wa kawaida: Serikali inasaidia baadhi ya gharama, hivyo ni rahisi kwa watu wenye kipato cha kati au kidogo. Kuliko kujichanga na kujenga nyumba ambazo ni below standard ni heri mwananchi apange kwenye apartment za bei nafuu
2. Mpango wa usafi na afya
Miji mipya inafanyiwa urban planning, hivyo barabara, mifereji ya maji, na taka zinapangwa vizuri. Kuliko mazingira ya uswazi. Mpangilio mbovu una attract uchafu, watu wanatupa taka hovyo na hawaoni aibu kwa sababu mazingira yenyewe hayavutii. Hii ni human psychology (Broken window theory)
3. Usalama
Blocks za apartments mara nyingi zina milango ya kudhibiti, CCTV, na wakaguzi wa usalama. Ukiangalia nchi zote ambazo wananchi wake wanaishi sana kwenye apartment ndio zinaongoza kwa usalama duniani (China, South Korea, Japan, Singapore)
4. Huduma zinakuwa karibu
Shule, maduka, vituo vya afya na maegesho ya umma mara nyingi vipo ndani ya maeneo hayo.
MUUNDO NA MPANGILIO WA MITAA YA APARTMENTS KWA AJILI YA WANANCHI CHINA (Chinese residential neighborhoods)
1. Apartments zinaunganishwa na barabara pana za magari na njia za watembea kwa miguu.
2. Zinajengewa bustani ndogo, miti, na maeneo ya michezo kwa watoto.
3. Urban planning
Kila block ina eneo lake la park, shule, soko, frame za maduka ya msingi karibu nk
4. Mfumo wa maji na umeme umewekwa ili kuepuka matatizo ya usafi na msongamano.
5. Kunakuwa na njia za baiskeli na barabara za watembea kwa miguu
Kwa sababu ni housing mass-production, bei inabakia chini kuliko nyumba binafsi.
Apartments ndogo zina bei nafuu zaidi, zinazofaa kwa vijana, wafanyakazi wa maofisini, familia zinazojitafuta, na hata zilizojipata
Mitaa ya apartments inavyokuwa, unaweza kukuta residential compounds yenye ghorofa 10–30.
Kila block ina green space: miti midogo, bustani za michezo, na sehemu za kukaa.
Njia za barabara haziwezi kuwa na msongamano mkubwa kwa sababu zoning imepangwa vizuri: makazi, biashara, na huduma za jamii hazichanganyiki bila mpangilio.
Hizi apartments ndio zimesaidia China kutokuwa na mitaa ya hovyo kama ya hapa kwetu Tanzania. Apartments ni better option ya makazi
Fikiria nchi kama USA Ina uchumi mkubwa kuliko China na Ina watu wachache kuliko China (China Ina watu bilioni 1.4, USA Ina watu milioni 350) lakini USA ina homeless people wengi kuliko China. That means Chinese way is more effective
Hapa Tanzania nako homeless sio wengi lakini sasa watu wanakaa kwenye makazi dunia. Ni muda sasa tuanze kujenga apartments nyingi kila kona ya Tanzania ili watu wakae kwenye nyumba nzuri. Kodi ziwe chini na sisi nchi yetu ipendeze, tupunguze urban sprawl, na matumizi ya ardhi yasiyo ya lazima.
NHC waache kujengea nyumba wahindi na waarabu, waweke bei rafiki ili Watanzania waone sababu za kuhamia kwenye apartments.
Wala sio lazima ziwe apartments ndefu kama za China. Huku hata zikijengwa za urefu wa 5 floors each inatosha
Maana hii hali sio nzuri 👇
Nasema hivi kwa sababu clearly hii ya kila mtu kujenga nyumba yake mwenyewe imetushinda. Watu wasijenge nyumba mpaka wajipate, kipindi wanajitafuta wakae kwenye apartments za serikali au kampuni binafsi
NHC wanajenga apartments Dodoma na hata Dar tumeona miradi kama Kawe 711 na Samia Housing Scheme lakini kusema ukweli hii hata haitasaidia kitu. Nyumba za NHC huwa ni expensive ndio maana wanaishia kukaa wahindi na waarabu. Inapaswa zijengwe apartments na bei ziwe rafiki kwa Watanzania wa kawaida ili kupunguza makazi holela, sio hizi za NHC ambazo bei zake Wana afford foreigners tu. Na hata Watanzania wanao afford ni mara kumi wajenge nyumba zao wenyewe maana watapata nyumba nzuri zaidi
Take a look at this
Hapa ni Mbeya
Umeona jinsi nyumba zilivyojengwa bila mpangilio na kuchukua ardhi kubwa bila sababu za msingi? Lakini kama zingejengwa apartment kadhaa, zikapandwa nyasi, miti, mitaro na sewage system mazingira yangekuwa mazuri zaidi ya hivi. Matatizo kama mafuriko, kipindupindu, maeneo kutofikika nk yangepungua na mji ungependeza kimuonekano
Hapa ni Dar
Angalia hicho kipande kidogo kilichojengwa hovyo bila mpangilio
Na hapa pia ni Dar 👇
.
.
Hapa ni Mwanza
Hawa watu wote wanaoishi kwenye nyumba zinazoonekana kwenye picha wangetosha kama wangekaa kwenye apartment moja pekee.
Kuzuia mambo kama haya ndio maana Wachina waliamua kujenga apartments nyingi nchi nzima
KWA NINI WACHINA WALIAMUA KUJENGA APARTMENTS NYINGI NCHI NZIMA?
Hapa sababu zote zipo applicable hata hapa Tanzania
1. Ukuaji wa haraka wa idadi ya watu na mijini
China ina miji mikubwa yenye watu wengi. Kwa sababu ya uhamiaji mkubwa kutoka vijijini kwenda mijini (urbanization), kuna hitaji kubwa la makazi. Apartments ni suluhisho linaloweza kuchukua watu wengi katika eneo dogo. Ni kama tu hapa Tanzania (Jiji la Dar lina watu takribani milioni 5.3, Jiji la Mwanza watu milioni 1, majiji ya Arusha, Dodoma na Mbeya yana watu takribani laki 6 each)
2. Ufanisi wa ardhi na rasilimali
Ardhi mjini ni ya thamani kubwa. Kujenga nyumba za ghorofa nyingi (high-rise apartments) kunaruhusu kutumia ardhi kidogo lakini kufikia idadi kubwa ya familia.
3. Kurekebisha gharama za makazi
Apartments nyingi kwa mpango mmoja (mass housing) zinafanya gharama ya kila nyumba kuwa nafuu zaidi kuliko kujenga nyumba binafsi. Serikali pia inaweza kudhibiti bei za nyumba kwa urahisi zaidi.
4. Kurahisisha huduma za kijamii
Wakati watu wengi wakiishi karibu kwenye buildings za makazi, ni rahisi kutoa huduma kama barabara, maji, umeme, shule, hospitali, na usafishaji wa miji.
FAIDA ZA SERIKALI KUJENGA APARTMENT NYINGI TANZANIA NZIMA
1. Bei nafuu kwa wananchi wa kawaida: Serikali inasaidia baadhi ya gharama, hivyo ni rahisi kwa watu wenye kipato cha kati au kidogo. Kuliko kujichanga na kujenga nyumba ambazo ni below standard ni heri mwananchi apange kwenye apartment za bei nafuu
2. Mpango wa usafi na afya
Miji mipya inafanyiwa urban planning, hivyo barabara, mifereji ya maji, na taka zinapangwa vizuri. Kuliko mazingira ya uswazi. Mpangilio mbovu una attract uchafu, watu wanatupa taka hovyo na hawaoni aibu kwa sababu mazingira yenyewe hayavutii. Hii ni human psychology (Broken window theory)
3. Usalama
Blocks za apartments mara nyingi zina milango ya kudhibiti, CCTV, na wakaguzi wa usalama. Ukiangalia nchi zote ambazo wananchi wake wanaishi sana kwenye apartment ndio zinaongoza kwa usalama duniani (China, South Korea, Japan, Singapore)
4. Huduma zinakuwa karibu
Shule, maduka, vituo vya afya na maegesho ya umma mara nyingi vipo ndani ya maeneo hayo.
MUUNDO NA MPANGILIO WA MITAA YA APARTMENTS KWA AJILI YA WANANCHI CHINA (Chinese residential neighborhoods)
1. Apartments zinaunganishwa na barabara pana za magari na njia za watembea kwa miguu.
2. Zinajengewa bustani ndogo, miti, na maeneo ya michezo kwa watoto.
3. Urban planning
Kila block ina eneo lake la park, shule, soko, frame za maduka ya msingi karibu nk
4. Mfumo wa maji na umeme umewekwa ili kuepuka matatizo ya usafi na msongamano.
5. Kunakuwa na njia za baiskeli na barabara za watembea kwa miguu
Kwa sababu ni housing mass-production, bei inabakia chini kuliko nyumba binafsi.
Apartments ndogo zina bei nafuu zaidi, zinazofaa kwa vijana, wafanyakazi wa maofisini, familia zinazojitafuta, na hata zilizojipata
Mitaa ya apartments inavyokuwa, unaweza kukuta residential compounds yenye ghorofa 10–30.
Kila block ina green space: miti midogo, bustani za michezo, na sehemu za kukaa.
Njia za barabara haziwezi kuwa na msongamano mkubwa kwa sababu zoning imepangwa vizuri: makazi, biashara, na huduma za jamii hazichanganyiki bila mpangilio.
Hizi apartments ndio zimesaidia China kutokuwa na mitaa ya hovyo kama ya hapa kwetu Tanzania. Apartments ni better option ya makazi
Fikiria nchi kama USA Ina uchumi mkubwa kuliko China na Ina watu wachache kuliko China (China Ina watu bilioni 1.4, USA Ina watu milioni 350) lakini USA ina homeless people wengi kuliko China. That means Chinese way is more effective
Hapa Tanzania nako homeless sio wengi lakini sasa watu wanakaa kwenye makazi dunia. Ni muda sasa tuanze kujenga apartments nyingi kila kona ya Tanzania ili watu wakae kwenye nyumba nzuri. Kodi ziwe chini na sisi nchi yetu ipendeze, tupunguze urban sprawl, na matumizi ya ardhi yasiyo ya lazima.
NHC waache kujengea nyumba wahindi na waarabu, waweke bei rafiki ili Watanzania waone sababu za kuhamia kwenye apartments.
Wala sio lazima ziwe apartments ndefu kama za China. Huku hata zikijengwa za urefu wa 5 floors each inatosha
Maana hii hali sio nzuri 👇