Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Siamini masikio wala macho yangu. Watanzania tuna tatizo gani? Lowasa anawapotosha kirahisi namna hii?!? Jamani, mbona mnasahau kirahisi issue iliyomtoa Lowasa Uwaziri Mkuu ni mazingira ya rushwa kupitisha mradi wa Richmond? Hata kama ni kweli alimpigia simu JK kusema wavunje mkataba wa Richmond, haifuti ukweli kwama alipitisha Richmond kwa nguvu katika mazingira ya kifisadi. Hilo ndio hatia yake, na hilo ndilo kamati ya Mwakyembe ililiona na kulisema. Lowasa si mjinga, nahisi alipiga hiyo simu kumtega JK na kujilinda baadaye mambo yakigeuka, akijua wazi walifanya jambo la ufisadi Richmond! Yaani mnadhani Lowasa hakujua wahusika wa Richmond?
Lowasa kawatega, amechukua kakipengele kadogo katika suala la Richmond na wote mkakimbilia huko na kusahau lililo kubwa katika mkataba wa Richmond. Jamani, jamani, jamani, be smart!!!
Hivi kweli kwa kauli moja ya Lowasa basi leo mnaona yale yote yaliyo kwenye taarifa ya Kamati ya Mwakyembe hayafai tena?
Hivi mnamjua Lowassa nyie? Ulizeni watu waliofanya naye kazi akiwa Waziri Wizara ya Ardhi, hadi ikafikia Mtanzania mhindi kusema Lowasa ananuka rushwa! Mhindi kukutuhumu unanuka rushwa, yaani wewe ndio basi tena, maana ana taarifa zote za rushwa wanazotoa wahindi wenzake! Hivi mmesahau Lowasa alituhumiwa nini na Nyerere katika kugombea uraisi hata akafukuzwa toka ukumbini kama mtoto mdogo?
Jamani kweli nawasikitikia Watanzania. Wasahaulifu mno!
Lowasa kawatega, amechukua kakipengele kadogo katika suala la Richmond na wote mkakimbilia huko na kusahau lililo kubwa katika mkataba wa Richmond. Jamani, jamani, jamani, be smart!!!
Hivi kweli kwa kauli moja ya Lowasa basi leo mnaona yale yote yaliyo kwenye taarifa ya Kamati ya Mwakyembe hayafai tena?
Hivi mnamjua Lowassa nyie? Ulizeni watu waliofanya naye kazi akiwa Waziri Wizara ya Ardhi, hadi ikafikia Mtanzania mhindi kusema Lowasa ananuka rushwa! Mhindi kukutuhumu unanuka rushwa, yaani wewe ndio basi tena, maana ana taarifa zote za rushwa wanazotoa wahindi wenzake! Hivi mmesahau Lowasa alituhumiwa nini na Nyerere katika kugombea uraisi hata akafukuzwa toka ukumbini kama mtoto mdogo?
Jamani kweli nawasikitikia Watanzania. Wasahaulifu mno!