Kwanini Watanzania hawapendi kusafiri?

Mwanamke aitwaye Cassandra de Pecol kutoka Connecticut, alifanikisha ndoto yake ya kutembelea nchi zote duniani, 193,
akiwa na umri wa miaka ishirini na saba.

Mpaka anafikisha miaka 18, Canada ndiyo nchi pekee aliyokuwa amefika, tena, ni kwa vile mama yake anatokea huko. Sababu kubwa iliyomfanya asisafiri akiwa mdogo ni uwezo mdogo wa kifedha.

Kufanikiwa kwake kuzitembelea nchi 193 ni jitihada zake binafsi. Anavyoonekana si tajiri, ila anapenda kusafiri. Lakini kuna Watanzania ambao pengine wana uwezo mkubwa kifedha kumzidi yeye lakini bado hawasafiri.

Ukizilinganisha nchi za Afrika Mashariki, hasa Kenya, Uganda, na Rwanda, Watanzania ndiyo wanaoongoza kwa kutokusafiri kwenda nchi zingine. Kwa nini hivyo?

1. Umaskini?

2. Lugha?

3. Ugumu wa upatikanaji wa passport?

4. Ushamba?

5. Utamaduni?

Sababu ni nini?
All of the above ikiwemo hali ya kiuchumi.
 
Sio kwamba hatupendi kusafiri ni kwamba nauli ndio changamoto wenzetu wametatua swala la nauli ndio maana wanafanikiwa ukijifungia ndani fursa pia unazifungia kutoka Mkoa au Nchi nyingine ni kufungua fursa huko...
 
Nitajibu Kulingana na Title. UMEWAPA HIZO HELA ZA KUSAFIRIA
1. Kwanza Unatakiwa kujua Pato la Mtanzania Mmoja Mmoja Ni Lipi

2. Mtu anawaza Madeni huo Muda wa Kusafiri Anautoa Wapi.?
 
Asilimia kubwa wanaoishi Ulaya hawawazi kesho watakula nini watavaa nini, hiyo hatua wameshaivuka miaka mingi Sana ndio maana unaona wanawaza kwenda anga za juu kuishi.. kubuni mambo mengii sasa utakuwa mbunifu wa aina gani Kama muda wote unawaza utakula nini? Njaa inakuuma. Stress ?



Sasa wewe mtanzania wa makambako bado unawaza kesho utakula nini, utavaa nguo gani? Kama pesa ya mama mwenye nyumba inakusumbua kuipata hiyo nauli utatoa wapi!.? Ya kwenda nchi za nje? Kwanza kitengo tu cha kwenda kuomba kibali wahusika wanakushangaa wanaanza kukupa ushauri usiende. 😁 wanakuambia ukienda tunajua hautarudi.. utang'ang'ania huko huko.

ndugu zangu watanzania. Pesa ni muhimu Sana hasa kwa sisi wanaume pesa ni muhimu sana. Hakuna mtu asiependa kuishi maisha mazuri hayupo
 
Napenda kuchangia. Binafsi nimesafiri Dubai na Guangzhou kama mkalimani. Njia nyingine unaweza kujifunza lugha za kimataifa kuanzia 5 na kuendelea, uwe competent kweli, then safari za nje utazizoea.
 
Mwanamke aitwaye Cassandra de Pecol kutoka Connecticut, alifanikisha ndoto yake ya kutembelea nchi zote duniani, 193,
akiwa na umri wa miaka ishirini na saba.

Mpaka anafikisha miaka 18, Canada ndiyo nchi pekee aliyokuwa amefika, tena, ni kwa vile mama yake anatokea huko. Sababu kubwa iliyomfanya asisafiri akiwa mdogo ni uwezo mdogo wa kifedha.

Kufanikiwa kwake kuzitembelea nchi 193 ni jitihada zake binafsi. Anavyoonekana si tajiri, ila anapenda kusafiri. Lakini kuna Watanzania ambao pengine wana uwezo mkubwa kifedha kumzidi yeye lakini bado hawasafiri.

Ukizilinganisha nchi za Afrika Mashariki, hasa Kenya, Uganda, na Rwanda, Watanzania ndiyo wanaoongoza kwa kutokusafiri kwenda nchi zingine. Kwa nini hivyo?

1. Umaskini?

2. Lugha?

3. Ugumu wa upatikanaji wa passport?

4. Ushamba?

5. Utamaduni?

Sababu ni nini?
Tuna mambo mengi kichwani ndo maana hatuwezi kusafiri, hata ukiangalia nchi za wenzetu wanafocus na ushoga kwa sababu hawana shida ya maji, umeme, umasikini na afya. Akili zao zinaanza kutafuta shida nyingine maana binadamu tumeumbwa kusolve shida na matatizo. Ndo maana hata wabongo tukishinda vijiweni hatuwezi kujikalia tu tutaanza kuchunguza watu na kufuatilia watu that is our human nature.
 
Jambo moja gumu zaidi ni kutokuwa na kipato cha kutosha, mtu anayelipwa laki tatu au chini ya hapo atawezaje kumudu ghalama za maisha na kusafiri pia?

Hali ngumu ya maisha ndio inayowafanya watanzania wengi kusafiri kuonekane jambo la ajabu kabisa.
 
Mwanamke aitwaye Cassandra de Pecol kutoka Connecticut, alifanikisha ndoto yake ya kutembelea nchi zote duniani, 193,
akiwa na umri wa miaka ishirini na saba.

Mpaka anafikisha miaka 18, Canada ndiyo nchi pekee aliyokuwa amefika, tena, ni kwa vile mama yake anatokea huko. Sababu kubwa iliyomfanya asisafiri akiwa mdogo ni uwezo mdogo wa kifedha.

Kufanikiwa kwake kuzitembelea nchi 193 ni jitihada zake binafsi. Anavyoonekana si tajiri, ila anapenda kusafiri. Lakini kuna Watanzania ambao pengine wana uwezo mkubwa kifedha kumzidi yeye lakini bado hawasafiri.

Ukizilinganisha nchi za Afrika Mashariki, hasa Kenya, Uganda, na Rwanda, Watanzania ndiyo wanaoongoza kwa kutokusafiri kwenda nchi zingine. Kwa nini hivyo?

1. Umaskini?

2. Lugha?

3. Ugumu wa upatikanaji wa passport?

4. Ushamba?

5. Utamaduni?

Sababu ni nini?
Ugali mtamu😄

Kauli hiyo waliitoa walipotakiwa waandamane kipindi kile mkuu wa polisi aliposema wakiandamana watapigwa kipigo cha mbwa koko. Sijui ni ile UKUTA ya chadema?

Kwa asili ni waoga. Lakini kwasababu kuna chakula, watabanana hapo tu maisha yaendelee.

Hata kuku anapata mauchafu ya kula hawezi kuwa na juhudi za kuruka juu kama ndege wengine wala hajishghulishi.
 
Sio kwamba hatupendi kusafiri ni kwamba nauli ndio changamoto wenzetu wametatua swala la nauli ndio maana wanafanikiwa ukijifungia ndani fursa pia unazifungia kutoka Mkoa au Nchi nyingine ni kufungua fursa huko...
Wazungu wana save hela kwa ajili ya vacations pia
Je sisi wabongo tunafanyaga hivyo

Ova
 
Iko hivi ukiangalia wazungu wengi ni watu ambao wanafanya sana saving hata wenye vipato vya kawaida.

Wanaweza saving kwakuwa kwanza kiwango cha utegemezi kwao ni kidogo sana. Yani utakuta baba na mama wana mtoto mmoja au hawana na hamna mtu anaewaomba hela.

Hakuna sijui michango ya ukoo, sijui mtoto wa mjomba ada shule, mara rafiki anaoa, mara bibi anaumwa n.k

Birth control imesaidia wenzetu sana. Sisi huku mtu ana ndugu zaidi ya laki na akipata tu ka ajira ka kulipwa laki saba basi kila mtu anamtolea macho, vizinga visivyoisha.

Huyo mtu ata save sangapi ili aweze kutembelea nchi mbalimbali?

Kingine kwa wenzetu wa nje huko wengi wanakula generational wealth. Yani mtu anazaliwa anakuta familia iko well-off kuanzia vizazi kadhaa vilivyopita. So yeye anaendeleza kutengeneza hela tu na future ya kizazi chake so mambo kama kusafiri ni kawaida tu.

Chamwisho ni nchi yetu hii ina mifumo ya ajabu sana. Mtu kumiliki passport tu inaonekana kama vile ni jambo la ajabu sana. Ukienda uhamiaji kutaka passport inakuwa ni mchakato mgumu utadhani unataka kwenda mbinguni.

Nchi za wenzetu kuwa na passport ni kawaida na kila raia anayo kama document muhimu. Hapa kwetu passport inachukuliwa tofauti sijui kwanini CCM hawataki raia wamiliki passport?
Hapo kwenye kupata paspoti uhamiaji nimekuelewa sana
 
Back
Top Bottom