Kwanini Watanzania hawaendi uwanjani inapocheza timu ya taifa

Kwanini Watanzania hawaendi uwanjani inapocheza timu ya taifa

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
Tanzania tumepata bahati ya ku host mashindano Makubwa ya CHAN 2025 pamoja na Kenya na Uganda

Kwa wenzetu Kenya tunaona viwanja vinajaa na TV zinawekwa kwenye maeneo ya wazi, Watu wana hamasa mno
Hapa kwetu Tanzania tumeonekana hata kufika watu 10, 000 kwenye uwanja wa kubwa watu 64, 000 hatuwezi

Sababu zinaweza kuwa zifuatazo
1. Siasa, wapambe na viongozi wamekuwa waki dedicate ushindi wa Taifa stars Kwa viongozi wa Kisiasa, ambaye haungwi mkono na watu wengi

2. Dhulumat na uhuni pale TFF
Tumeona Rais Karia akijitengenezea mazingira ya kushindwa bila kuwaruhusu wengine kugombea. Hili linagawa watu wengi

3. Hamasa ndogo Kwa wachezaji.

4. Kuitwa Kwa kikosi Kwa vi memo.
Tumeona timu ya taifa imejaza Wazanzibar wengi, kwakuwa coach ni Mzanzibar na kuwaacha wachezaji wengi kutoka Tanganyika kama Chikola, Mtasingwa, Mgunda n.k

5. Hali ngumu kiuchumi

6. Siasa za upande mmoja yaani CCM
 
Tulianza kupenda SSC & YNG kabla ya kupenda Mpira
 
CCM imejipenyeza ndani ya TFF hatimaye TFF imekuwa kama taasisi ya chama tawala yaani haina tofauti na UVCCM ni kama ilivyofanywa BAKWATA na KKKT!...Aibu sana taasisi kubwa kama hizo kushikiwa akili na Ccm
 
Stars ikishinda inatakiwa sifa ziende kwa mama ambaye kwa kweli hapendwi na watanzania wengi lakini ikifungwa mama ahusiki na anatafutwa mchawi.

Kwa hali ilivyo kwa sasa inatakiwa wanasiasa waachane kabisa na mambo ya mpira na watilie maanani namna gani ya kupigana kuondoa umaskini uliokithiri nchini huku wenyewe wakiendelea kuneemeka.
 
Back
Top Bottom