Kwanini wasio na elimu wanawachukia wenye elimu?

future lawyer

JF-Expert Member
Jan 28, 2020
404
388
Habari za siku wanajamvi,

Natumai nyote wazima wa afya. Niende moja kwa moja kwenye mada.

Kumekuwa na chuki inayosambaa kwa spidi ya 5G baina ya tabaka lenye elimu "waliosoma" na tabaka wasio na elimu "darasa la 7 " . Kwenye haya matabaka kila moja linajinasibu kuwa bora kuliko lenzie katika nyanja za kimaisha.

Mimi ni kijana nimebahatika kupata degree, baada ya kumaliza chuo Kama mjuavyo Kuna uhaba wa ajira "hakuna kabisa " nimesota kitaa bila matumaini nikachukua maamuzi ya kuendesha bodaboda. Tangu niingie kwenye hii fani nimekuwa nikisemwa vibaya na watu wa Std vii .

Nilichogundua ni kwamba watu "std vii" wanatuchukia sana tulio na elimu zetu wanajifariji kwa maneno yao Kama vile: Elimu yako imekufikisha wapi, una_degree unafanya bodaboda n.k. Kingine wao ndio wanajiona wajanja wanajua kila kitu kuliko wenye degree "sisi washamba hatujui bata wala maisha". Niliona uzi wa mdau humu akilalamika jamaa yake anamsema vibaya kwa watu kuwa ana degree lakini bodaboda.

Nataka nitoe rai kuwa na degree sio dhambi na sio kipimo cha mafanikio Bali ni kipimo cha elimu tu .

ACHENI WIVU ATA HUMU MPO NA NINAWAJUA
 
Kuna mmoja juzi ktk kituo cha redio kikubwa tu ktk kipindi cha usiku eti adiriki kusema degree za makaratasi

Nikasema iv kwann yy akaishindwa kuipata iyo degree ya makaratasi
 
Habari za siku wanajamvi,

Natumai nyote wazima wa afya. Niende moja kwa moja kwenye mada.

Kumekuwa na chuki inayosambaa kwa spidi ya 5G baina ya tabaka lenye elimu "waliosoma" na tabaka wasio na elimu "darasa la 7 " . Kwenye haya matabaka kila moja linajinasibu kuwa bora kuliko lenzie katika nyanja za kimaisha.

Mimi ni kijana nimebahatika kupata degree, baada ya kumaliza chuo Kama mjuavyo Kuna uhaba wa ajira "hakuna kabisa " nimesota kitaa bila matumaini nikachukua maamuzi ya kuendesha bodaboda. Tangu niingie kwenye hii fani nimekuwa nikisemwa vibaya na watu wa Std vii .

Nilichogundua ni kwamba watu "std vii" wanatuchukia sana tulio na elimu zetu wanajifariji kwa maneno yao Kama vile: Elimu yako imekufikisha wapi, una_degree unafanya bodaboda n.k. Kingine wao ndio wanajiona wajanja wanajua kila kitu kuliko wenye degree "sisi washamba hatujui bata wala maisha". Niliona uzi wa mdau humu akilalamika jamaa yake anamsema vibaya kwa watu kuwa ana degree lakini bodaboda.

Nataka nitoe rai kuwa na degree sio dhambi na sio kipimo cha mafanikio Bali ni kipimo cha elimu tu .

ACHENI WIVU ATA HUMU MPO NA NINAWAJUA

Vita hivi ni vingi
Bodaboda vs wenye magari
Wenyenyumba vs wapangaji
Matajiri vs maskini
Walakitimoto ,nyama ya kuku,ngombe,samakivs wala maharage,dagaa,mboga za majani
Wanywa bia vs wanywa soda
 
Elimu ya mtaa ndo mpangomzima yaani malomoni ya kutosha tu Kama Mimi nimesoma Chuo inshallah Nina matumaini ya kuja kupata ajira ila mastori ya town yapo kitaa
Nipeni deal masela nikamate mahela
 
Piga boda yako mzee, siku ikitokea anatakiwa mwenye cheti mahali ndio watajua hawajui, wasiosoma wengi kwa sasa wana hiyo tabia, utawasikia bora yeye kuliko hao wenye PhD wakati mwenzao anakula milion 2 mahali, ndio zao kujifariji, ingia darasani uone balaa lake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom