Nipe tofauti ya waisraeli na wayahudi
Je unafahamu wapo waisraeli waislam ndani ya jeshi la Israel?
Kwa nini kichwa cha mada yako kiseme waislam wanaitaka jerusalem angali wapo waisraeli waislam wanasema pia jerusalem ni mji wao na wayahudi hawapingi hilo?
Hivi unasoma kwa kina kweli au unakurupuka tu kujibu🤔
Wewe ndio unakurupuka ,na hausomi kwa kutafakari , nitakujibu kadri niwezavyo
kwanza tuweke sawa
"Mwisraeli" ni jina la uraia mtu yeyote aliyezaliwa au aliepata uraia ndani ya taifa la kisasa la Israel, iwe ni Myahudi, Mwislamu, Mkristo au hata msioamini kabisa kuhusu Mungu kama wewe japo unaonekana ni Kobazi au ulikuwa kobazi,
"Myahudi" ni mtu wa taifa la kale la Kiyahudi, uzao wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo (Israeli), na mfuasi wa dini ya Kiyahudi. Si kila Mwisraeli ni Myahudi, na si kila Myahudi ni Mwisraeli (kwa sababu wengine wanaishi diaspora Marekani, Ufaransa, n.k.).
Kwa hiyo ni kweli kabisa wapo Waisraeli Waislam, na wengine wako ndani ya jeshi la Israel (IDF) wakihudumu kama askari, madaktari na hata wabunge. Hili halina ubishi.
Lakini sasa ngoja nirudi kwenye msingi wa mada
“Waislam wanaitaka Jerusalem.”
Sasa, hii mada haikuzaliwa kwa ubaguzi bali kwa muktadha wa kisiasa na kidai la ardhi. Wanaodai kuwa Jerusalem ni mji wa Kiislamu ni Wapalestina (hasa kundi la Hamas, Fatah, n.k.) na washirika wao wa Kiislam wa mataifa mengine kama Iran, Pakistan n.k. si Waisraeli Waislam walio ndani ya mfumo wa kisheria wa Israel.
Waisraeli Waislam wanaoishi ndani ya taifa hilo hawapingani na haki ya Wayahudi kwa Jerusalem, bali wanaishi kwa amani, wakifaidika na uhuru wa kuabudu kuanzia Msikiti wa Al-Aqsa hadi makanisa na sinagogi.
Hakuna rekodi ya Waisraeli Waislam kuongoza maandamano ya kuiita Jerusalem "mji wa Kiislamu" dhidi ya Wayahudi. Hilo linafanywa na mataifa au vikundi vya Kiislam vinavyopinga kuwepo kwa taifa la Israeli kabisa.
Kwa hiyo kaka, sijasema kila Mwislamu anaitaka Jerusalem bali hoja ni kuwa Uislamu wa kisiasa (Islamist ideology) unatumia madai hayo kupinga mizizi ya Kiyahudi katika mji huo mtakatifu.,hata huku waislamu wa buza wanadandia hiyo hoja