Sina hakika ninachokiandika kitawafikia wahusika lakini baada ya kuona threads mbili zinazomhusu Sheikh Khalifa akimlaumu Magufuli kwa udini wa kupendelea wakristo wenzie nimeona nichangie kidogo.
Sheikh Khalifa amekuwa akizungumza haya toka wakati wa Mwinyi ndio Rais
cha ajabu alipoingia Kikwete Ikulu sheikh Khalifa akanyamaza kimyaa
kuzungumzia msalahi ya waislam na mara kwa mara alikuwa
akimualika Kikwete msikitini na alishiriki kuwapigia kampeni wote
Mkapa,Kikwete na Magufuli.
Sasa leo anaanza kuongea haya haya aliyo yaongea zaidi ya miaka 20 iliyopita
na watu wanamshangilia.
Maswali ya kujiuliza ni haya?
Je, ni lazima waislam waiunge mkono CCM?
Why kila mara malalamiko haya haya lakini ukija uchaguzi hawa hawa kina Khalifa wanaipigia debe CCM?
Je, masuala ya uteuzi hasa teuzi za wakuu wa mikoa na wilaya si masuala ya kikatiba?
Si katiba ya Warioba kwa mfano ilipinga Rais kuteua wakuu wa wilaya?
Je, kina Khalifa walikuwa wapi kuwashawishi waislam waunge mkono katiba ingine ambayo itaondoa Rais kufanya teuzi na wananchi wakiwemo waislam kuja kuchagua viongozi moja kwa moja?
Nionavyo mimi badala ya kumbembeleza Magufuli au Rais yeyote kuteua wakuu wa wilaya, waislam na wakuu wa mikoa waislam ni bora hizo nafasi ziwe za kuchaguliwa kwa kura na wananchi wachague wanaeona anawafaa.
Suluhisho la madai ya teuzi kwa waislam ni katiba ambayo itawapa wananchi nguvu ya kuchagua wanao wataka ngazi za mikoa na wilaya.
Rais apunguziwe mamlaka ya kuteua watu wengi ambao wengine ndo kama hivyo asilimia 95 ni wa dini yake.
Hivyo ili hilo lifanyike waislam waungane na wote wanaopenda demokrasia kudai katiba mpya ambayo wananchi watakuwa na nguvu na katiba itakayoleta tume huru ya uchaguzi.
Hili la kumlalamikia Magufuli linapaswa kukomeshwa. Nyerere alalamikiwe
na Magufuli pia? Madai yale yale miaka zaidi ya 30?
Waislam hawajifunzi kitu?