Kwanini viongozi wengi wa dini wanahubiri wananchi tudumishe amani bila kuwahimiza kwanza watawala watende HAKI?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Imeandikwa Katika Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 nanukuu "HAKI HUINUA TAIFA, BALI DHAMBI NI ADUI WA WATU WOTE" mwisho wa kunukuu.

Pamoja na kuwa Mimi siyo Askofu wala Sheikh, lakini nafahamu kuwa AMANI na HAKI ni pacha na huwezi kuvitenganisha vitu hivyo viwili, yaani AMANI na HAKI.

Inafahamika kupitia malalamiko mengi ya wananchi, kuwa Katika nchi yetu, watawala wetu hawatutendei Haki, lakini ni watawala wetu hao hao, hupenda kuwahimiza viongozi wetu wa dini, wahubiri amani, bila kwanza wao kututendea Haki, kama ambavyo imeandikwa Katika Biblia, kama nilivyonukuu.

Ni kwanini viongozi wetu wa dini Katika mahubiri yao, sijawasikia hata siku moja, wakiwahubiri watawala wetu, wakubali kutenda HAKI kwa kuiandika upya Katiba yetu, kwani ndiyo sheria mama, kwa kuwa Katiba tuliyo nayo hivi sasa, HAIKIDHI kabisa, mfumo wa vyama vingi, tulio nao hivi sasa na inakipendelea chama tawala cha CCM?

Hata Rais wetu, Samia Suluhu Hassan, anafahamu umuhimu wao viongozi wetu wa dini na akawasihi viongozi wetu wa dini, wahimize wananchi wadumishe amani, kwa kuwa kama alivyoeleza Rais wetu kuwa hao viongozi wetu wa dini, ndiyo wanaosikilizwa zaidi na sisi waumini wao!

Hivi hao viongozi wetu wa dini hawajui kuwa Hawa watawala wetu wa CCM, hawatendi Haki, kwa kupiga "chenga" kuiandika Katiba mpya ya nchi, huku wakiendelea kukumbatia Katiba ya zamani ya mwaka 1977, ambayo wanajua fika kuwa inaipendelea CCM na iliandikwa wakati wa mfumo wa chama kimoja, ilihali wakati huu tupo kwenye mfumo wa vyama vingi, ambapo Katiba hiyo ya zamani HAIKIDHI kabisa, mfumo huu wa vyama vingi?

Hivi viongozi wetu wa dini ni "vipofu" kiasi ambacho hawawezi kuona namna Katiba yetu ya sasa, inavyoviminya vyama vya upinzani, uwepo wake?

Hivi viongozi wetu wa dini, hawaoni namna watawala wetu wasivyovitendea vyama vya upinzani Haki, kwa kuendelea wao CCM kuendelea kufanya mikutano ya hafhara, wakati wanawatuma Polisi wao kuwapiga marufuku, vyama vya upinzani visifanye mkutano wowote wa kisiasa?

Hivi viongozi wetu wa dini, hawaoni namna Rais wetu, ambaye pia ndiyo Mwenyekiti wa Chama chake cha CCM, namna alivyopewa madaraka makubwa mno ya kikatiba, kitu kinachosababisha, aendelee kuviminya vyama vya upinzani?

Hivi viongozi wetu wa dini hawaoni madaraka makubwa aliyopewa Rais wetu ya kuteua wajumbe wote wa Tume ya uchaguzi nchini, Majaji wote wa Mahakama juu, Wakuu wote wa Mikoa, wakuu wote wa wilaya, wakurugenzi wote wa wilaya, ambao pia ndiyo wasimamizi wakuu wa chaguzi zetu?

Hivi upendeleo wote uliopewa chama cha CCM kwenye Katiba yetu, ina maana viongozi wetu wa dini, wamekuwa "vipofu" na hawawezi kabisa kuuona?

Nawasihi viongozi wetu wa dini, Kila watakapokuwa wanatusihi sisi wananchi tuendelee kudumisha amani, wafunguliwe mioyo yao na waone umuhimu mkubwa wa kuwasihi watawala wetu pia wadumishe HAKI Katika utawala wao, kwani huwezi kuitenganisha AMANI na HAKI, kwani vitu hivyo ni PACHA.

Mungu ibariki Tanzania
 
Amani ni zao la haki.

Papa Yohane Paulo aliwahi kusema amani pasipo haki haiwezi kuwa amani, ni ushetani (ulaghai).
Hawa viongozi wengi wa dini hapa nchini naamini watakuwa "wamenunuliwa" na watawala wetu, kwa kuwa siamini kuwa watakuwa "vipofu" hata washindwe kuyasoma maandiko ya kwenye vitabu vya dini, kwa usahihi!🥺
 
Hawa viongozi wengi wa dini hapa nchini naamini watakuwa "wamenunuliwa" na watawala wetu, kwa kuwa siamini kuwa watakuwa "vipofu" hata washindwe kuyasoma maandiko ya kwenye vitabu vya dini, kwa usahihi!🥺
Hata Shehe Ponda kanunuliwa? Simsikii siku hizi!
 
Ni kwanini viongozi wetu wa dini Katika mahubiri yao, sijawadikia hata siku moja, wakiwahibiri watawala wetu, wakubali kuiandika upya Katiba yetu, kwani ndiyo sheria mama, kwa kuwa Katiba tuliyo nayo hivi sasa, HAIKIDHI kabisa, mfumo wa vyama vingi, tulio nao hivi sasa?
Viongozi wa dini wanaweza kuhubiri kuhusu kutenda haki, na huwa wanafanya hivyo mara nyingi tu; lakini hawawezi kuhubiri kuhusu katiba kwa sababu katiba haimo kwenye Biblia. Kama huwa unasubiri wahubiri kuhusu katiba basi utasubiri sana.

Pili, wajibu wa viongozi kutenda haki na wajibu wa wananchi kudumisha amani ni nyajibu zinazoenda simultaneously. Viongozi wanatakiwa kutimiza wajibu wao, na wananchi tunatakiwa kutimiza wajibu wetu, bila kusubilia kundi moja baada ya jingine.
 
Hivi Hawa viongozi wetu wa dini, wanafahamu kuwa nchi nyingi hapa Duniani hutokea machafuko ya umwagikaji wa damu, kutokana na watawala wa hizo nchi, kutowatendea HAKI wananchi wao?🥺

Kama tufahamuvyo KINGA ni bora kuliko TIBA.

Tuchukue tahadhari mapema, kabla maafa hayajatupata.
 
wajibu wa viongozi kutenda haki na wajibu wa wananchi kudumisha amani ni nyajibu zinazoenda simultaneously. Viongozi wanatakiwa kutimiza wajibu wao, na wananchi tunatakiwa kutimiza wajibu wetu, bila kusubilia kundi moja baada ya jingine.
Upo sahihi. Lakini kwa mtazamo wako, unaona viongozi wanatimiza wajibu wao wa kutenda haki?
 
Wengi wanalamba asali and trust me, bila kanisa au misikiti ni ngumu sana kutawala nchi ndio maana serikali iko bega kwa bega na hao viongozi wa dini ambao ndio watu muhimu sana wanaotumika kutupumbaza.
 
Nijuavyo mimi hakuna dini inayohimiza machafuko bali ibada (imani)

Nijuavyo mimi mtu mwenye imani hawezi kuhimiza machafuko bali upendo

Nijuavyo mimi mtu mwenye upendo hujali wenzake kama anavyojali nafsi yake mwenyewe

Nijuavyo mimi hakuna sababu ya machafuko zaidi ya hasira, uchungu na kukata tamaa

Sasa kwanini hao viongozi tajwa wasihubiri ibada ili "watu wote" wawe na upendo na hivyo kuifanya amani iwepo automatically badala yake wahubiri amani?

Huenda kuna sehemu wanakengeuka
 
Nijuavyo mimi hakuna dini inayohimiza machafuko bali ibada (imani)

Nijuavyo mimi mtu mwenye imani hawezi kuhimiza machafuko bali upendo

Nijuavyo mimi mtu mwenye upendo hujali wenzake kama anavyojali nafsi yake mwenyewe

Nijuavyo mimi hakuna sababu ya machafuko zaidi ya hasira, uchungu na kukata tamaa

Sasa kwanini hao viongozi tajwa wasihubiri ibada ili "watu wote" wawe na upendo na hivyo kuifanya amani iwepo automatically badala yake wahubiri amani?

Huenda kuna sehemu wanakengeuka
Ni kweli hakuna dini inayotakiwa kuhimiza machafuko badala ya amani.

Hata hivyo kwenye vitabu hivyo hivyo vya dini, vinasema AMANI ni pacha wa HAKI.

Sasa ni kwanini viongozi wetu wa dini, wanaona dhahiri namna HAKI inavyominywa nchini kwetu, lakini wanakuwa "mabubu" kutokemea?
 
Imeandikwa Katika Biblia, kitabu cha Mithali 14:34 nanukuu "HAKI HUINUA TAIFA, BALI DHAMBI NI ADUI WA WATU WOTE" mwisho wa kunukuu.

Pamoja na kuwa Mimi siyo Askofu wala Sheikh, lakini nafahamu kuwa AMANI na HAKI ni pacha na huwezi kuvitenganisha vitu hivyo viwili, yaani AMANI na HAKI.

Inafahamika kupitia malalamiko mengi ya wananchi, kuwa Katika nchi yetu, watawala wetu hawatutendei Haki, lakini ni watawala wetu hao hao, hupenda kuwahimiza viongozi wetu wa dini, wahubiri amani, bila kwanza wao kututendea Haki, kama ambavyo imeandikwa Katika Biblia, kama nilivyonukuu.

Ni kwanini viongozi wetu wa dini Katika mahubiri yao, sijawasikia hata siku moja, wakiwahubiri watawala wetu, wakubali kutenda HAKI kwa kuiandika upya Katiba yetu, kwani ndiyo sheria mama, kwa kuwa Katiba tuliyo nayo hivi sasa, HAIKIDHI kabisa, mfumo wa vyama vingi, tulio nao hivi sasa na inakipendelea chama tawala cha CCM?

Hata Rais wetu, Samia Suluhu Hassan, anafahamu umuhimu wao viongozi wetu wa dini na akawasihi viongozi wetu wa dini, wahimize wananchi wadumishe amani, kwa kuwa kama alivyoeleza Rais wetu kuwa hao viongozi wetu wa dini, ndiyo wanaosikilizwa zaidi na sisi waumini wao!

Hivi hao viongozi wetu wa dini hawajui kuwa Hawa watawala wetu wa CCM, hawatendi Haki, kwa kupiga "chenga" kuiandika Katiba mpya ya nchi, huku wakiendelea kukumbatia Katiba ya zamani ya mwaka 1977, ambayo wanajua fika kuwa inaipendelea CCM na iliandikwa wakati wa mfumo wa chama kimoja, ilihali wakati huu tupo kwenye mfumo wa vyama vingi, ambapo Katiba hiyo ya zamani HAIKIDHI kabisa, mfumo huu wa vyama vingi?

Hivi viongozi wetu wa dini ni "vipofu" kiasi ambacho hawawezi kuona namna Katiba yetu ya sasa, inavyoviminya vyama vya upinzani, uwepo wake?

Hivi viongozi wetu wa dini, hawaoni namna watawala wetu wasivyovitendea vyama vya upinzani Haki, kwa kuendelea wao CCM kuendelea kufanya mikutano ya hafhara, wakati wanawatuma Polisi wao kuwapiga marufuku, vyama vya upinzani visifanye mkutano wowote wa kisiasa?

Hivi viongozi wetu wa dini, hawaoni namna Rais wetu, ambaye pia ndiyo Mwenyekiti wa Chama chake cha CCM, namna alivyopewa madaraka makubwa mno ya kikatiba, kitu kinachosababisha, aendelee kuviminya vyama vya upinzani?

Hivi viongozi wetu wa dini hawaoni madaraka makubwa aliyopewa Rais wetu ya kuteua wajumbe wote wa Tume ya uchaguzi nchini, Majaji wote wa Mahakama juu, Wakuu wote wa Mikoa, wakuu wote wa wilaya, wakurugenzi wote wa wilaya, ambao pia ndiyo wasimamizi wakuu wa chaguzi zetu?

Hivi upendeleo wote uliopewa chama cha CCM kwenye Katiba yetu, ina maana viongozi wetu wa dini, wamekuwa "vipofu" na hawawezi kabisa kuuona?

Nawasihi viongozi wetu wa dini, Kila watakapokuwa wanatusihi sisi wananchi tuendelee kudumisha amani, wafunguliwe mioyo yao na waone umuhimu mkubwa wa kuwasihi watawala wetu pia wadumishe HAKI Katika utawala wao, kwani huwezi kuitenganisha AMANI na HAKI, kwani vitu hivyo ni PACHA.

Mungu ibariki Tanzania
Labda na wao walishalamba Asali huwezi jua.
 
Ndio kazi yao inayowapa mkate wa kila siku. Siku hizi kuna zaka kidigitali automatically kila mwezi unapata meseji ukalipe zaka. Sasa kama hakuna amani wao hawawezi kupata pesa za kujenga mabangaloo, kuendesha ma fortuner.
 
Back
Top Bottom