Khantwe
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 59,468
- 119,623
Habari ya usiku huu wakuu,
Nimekuwa nikisikia maneno haya inapotokea kijana ametangulia mbele ya haki akiwa hajaoa wala kuzaa utasikia 'Maskini bora hata angekuwa ameoa/ana mtoto'.
Hivi hii imekaaje wadau maana mimi huwa nadhani mtu akiacha watoto na mjane ni maumivu zaidi kwa hao anaowaacha wakiwa bado wanahitaji uwepo wake. Wanadai eti akiacha mtoto jina halipotei.
Naomba maoni yako ni lipi bora ni bora yule anayeaga dunia huku nyuma akiacha yatima na wajane Au yule anayeondoka peke yake na huku duniani hajaacha kumbukumbu.
Nimejisikia kuwashirikisha hili maana mara kadhaa nimeona vijana hasa wa kiume wanahimizwa kuoa na kuzaa pale umri unapofika ili wapate wa kuendeleza majina yao just in case.
Karibuni
Nimekuwa nikisikia maneno haya inapotokea kijana ametangulia mbele ya haki akiwa hajaoa wala kuzaa utasikia 'Maskini bora hata angekuwa ameoa/ana mtoto'.
Hivi hii imekaaje wadau maana mimi huwa nadhani mtu akiacha watoto na mjane ni maumivu zaidi kwa hao anaowaacha wakiwa bado wanahitaji uwepo wake. Wanadai eti akiacha mtoto jina halipotei.
Naomba maoni yako ni lipi bora ni bora yule anayeaga dunia huku nyuma akiacha yatima na wajane Au yule anayeondoka peke yake na huku duniani hajaacha kumbukumbu.
Nimejisikia kuwashirikisha hili maana mara kadhaa nimeona vijana hasa wa kiume wanahimizwa kuoa na kuzaa pale umri unapofika ili wapate wa kuendeleza majina yao just in case.
Karibuni