Nipo single kwa sababu nilijipangia kuoa nikiwa na Miaka 25, nilipofikisha Miaka 22, nilianza kuchunguza wanandoa ndani ya ukoo wetu, majirani na marafiki. Cha ajabu sikupata hata ndoa moja ya kunivutia kama mfano, zote zilikuwa zinamuonekano mzuri kwa nje, lakini kwa ndani zilikuwa na mbaya mno!
Sikuweza kuchunguza ndoa ya wazazi wangu kwa kuwa niliondoka nyumbani kwenda kutafuta Maisha nikiwa na Miaka 19, lakini naweza kusema haikuwa na kitu kilichonivutia, ilikuwa na usiri mkumbwa mno, sikuwahi kuona hata siku moja baba na mama wakikwaruzana japo baba alikuwa na wake wawili wakiishi nyumba moja na kupika pamoja.
Vijana wengi wa lika langu wengi wameoa na kuacha, hii pia inaonyesha huko siyo salama. kwa sasa Niko hapili singo, na sins mpango wa kuipoteza hiyo furaha.