Kwanini upange sheria nyumbani kwangu?

Kwanini upange sheria nyumbani kwangu?

Wifi mcharuko, alafu wageni design ya mpaka anakwenda disco ugenini wakati wenyeji wake hamwendi hawafai maana mgeni hufuata kile mwenyeji wake anachokipenda


hii ni kweli kabisa......mgeni lazma ufwate sheria ya nyumba husika.....nakumbuka kipindi fulani nilikuwa nakaa arusha kwa kaka yangu.....kwa ajili ya kusoma....na walikuwa wana utaratibu wa kusali usiku.....mkishamaliza kula....mnaimba nyimbo mnapigaa makofi na kusali.....mkimaliza mnasoma biblia na kuitafakari......nilikuwa sipendi lakini ilinipasa kufanya hivyo mana ndiyo sheria ya hiyo nyumba......
 
mi ningemfukuza USIKU
KWANZA NISINGEWAPOKEA KABISAAAAAAA....NINGEWAKODIA GUEST WALALE ASUBUHI WAONDOKE MXIIIIIUUUUU

UNAANZAJE KUOOKEA WATU WENGI KIASI HICHO

Wallah mie sioni tabu wifi zangu au shemeji zangu kuja kwangu ila safari hii imezidi vituko..
 
nikwambie kitu???
ongea na mume wako mwambie kila kitu then mwambie hivi muende somewea this weekend na familiya yako then huyo wifi yako na shoga ake na watoto unawaambia mnaenda mapumzikoni for a week kwa hiyo inabidi warudi walipotoka
LAKINI ORIGINAL IDEA NI KWAMBA MNAENDA KUSPEND ONLY ONE DAY SIKU WATAKAYOONDOKA HAO MNAFUNGA NYUMBA KABISAAAAAAA
TUMIA HIYO NJIA

Shosti niamini Mimi wananiona zuzu ila Sio wanavyo nifikiria na sikutolewa nyongo mamuzi nikiyaona Siyo na hayaniridhi wanakwenda zao wote...
 
Wifi mcharuko, alafu wageni design ya mpaka anakwenda disco ugenini wakati wenyeji wake hamwendi hawafai maana mgeni hufuata kile mwenyeji wake anachokipenda

Yani sikuile alorudi asubuhi Babaangu alikuja kupitia papers flani akawepo niliona Aibu Mimi.. Yani nikimcharuko flani hivi...
 
ushapata la kufanya??embu sema hap tulipime tuone kama sawa

Siongei mengi ivooo zaidi ya kumueleza Mzee nilicho kiona Leo na tabia ya huyo Mdada, halafu yeye hua hapendi kuficha bunge litaanza na mwisho ndio ataamua, lakini mie basiiii naende zake kama wifi yuko mwengine Sio lazima mie..
 
Siongei mengi ivooo zaidi ya kumueleza Mzee nilicho kiona Leo na tabia ya huyo Mdada, halafu yeye hua hapendi kuficha bunge litaanza na mwisho ndio ataamua, lakini mie basiiii naende zake kama wifi yuko mwengine Sio lazima mie..

all the best ila ingekua mimi ningemuondoa kwa njia ngumu sana ambayo asingekaa anisahau maisha yake yote
 
Yan ww una moyo mkubw!...mpk umekuja kuomba ushauri hapa???...mimi ningemtandika viboko siku 1 yy na mshenzi mwenzie aliemleta ningewatimua kama wezi
 
nikwambie kitu???
ongea na mume wako mwambie kila kitu then mwambie hivi muende somewea this weekend na familiya yako then huyo wifi yako na shoga ake na watoto unawaambia mnaenda mapumzikoni for a week kwa hiyo inabidi warudi walipotoka
LAKINI ORIGINAL IDEA NI KWAMBA MNAENDA KUSPEND ONLY ONE DAY SIKU WATAKAYOONDOKA HAO MNAFUNGA NYUMBA KABISAAAAAAA
TUMIA HIYO NJIA

Kwa kweli mtu wa kujiachia mpk kwenye makochi ya familia tena ugenini....hapana kwa kweli....Sioni sababu ya yeye kujizungusha hivyo,amwambie ukweli (black and white) bila kumficha utaratibu wa nyumba yake ni huu,tabia zake hazivumiliki kutokana na anayoyafanya .Hata WiFi yake hana adabu,iweje asijue tabia za shoga.
 
Mtama kwa watoto we ni noma. Una roho ya wema hadi karibia inazidi uwezo!

Iko hivi, hiyo condom naamini 'haikutumika'. Wanakurusha roho Mtama. Hebu jiulize km kuna lililopungua hadi wifi alete zengwe lote hilo.......

Hii stori imefanana na ya mtu naemjua. Dadaake alimletea kifaa ndani ili kimsumbue njia kuu mpaka ajiondoe kwa hasira. Na aliondoka aisee..... kama vile nakuonea huruma maana ushasetiwa tayari mamaangu. Umemkosea nini mumeo? Maskini Mtama... Pole mama!
 
Last edited by a moderator:
Sijasoma comments zingine. Ila tu niulize unaelewana na wifi yako kweli?

Isije kuwa ndio mambo ya mapinduzi!!!!

BTW huyo dada hajitambui mketishe umueleze namna anavyopasa kuishi ugenini, kama mwelewa ataelewa.
 
Kwa kweli mtu wa kujiachia mpk kwenye makochi ya familia tena ugenini....hapana kwa kweli....Sioni sababu ya yeye kujizungusha hivyo,amwambie ukweli (black and white) bila kumficha utaratibu wa nyumba yake ni huu,tabia zake hazivumiliki kutokana na anayoyafanya .Hata WiFi yake hana adabu,iweje asijue tabia za shoga.
hii post imenifikirisha mengi HIVI KWELI UTAKOSA LA KUFANYA KABISA??FUKUZA WOTE
 
umeshajiuliza kwanini anajiamini hivyo?! shoga wa wifi aje na watoto kwako?ya wapi hayo?!halafu ana do nyumbani kwako?!kuna kitu hapo.binafsi napata hisia huyo ni zaidi ya shoga wa wifi yako na watoto wake pia!hujui la kufanya?!ongea na mumeo awaite mdogo wake na shoga yake.amweleze wazi huyo shoga wa mdogo wake afungashe haraka,akishindwa kumwambia lipo usilolijua! unasema mumeo anashangaa huyo mdada kafuata nini?!sidhani kama anashangaa mpaka moyoni! siwazii hata siku moja shoga wa wifi yangu aje likizo kwangu na wanae!!! apite na kanga moja mbele ya mume wangu namuangalia?never!
 
timua huyo haraka sana wewe maana ni chokoooo huyo!!
 
Hakuja hata na pini, Na zaidi asivyo kua na haya yeye ana watoto wa4 watoto hawasikii Juzi kuna mmoja amekula Mpaka ametapika, mtoto ameshakula na wenzie 1 na nusu usiku wamecheza Saa 3 wakunywa maziwa na wenzie halafu kulala ndio routine kwangu, huyu mtoto asione mtu anakula anataka mtoto Hata kama kulala anamuamsha...

dada nimepata shida moyoni utadhan wako kwangu..!
my dia wema usizid kipimo!!! wewe ni shangaz wa hao watoto? au huyo mumeo ni baba yao hawajakujulisha? napata shida kuelewa akili ya wif yako ya kubeba ushoga kuleta kwako? mbona nahic kuna mishen ambayo hujaielewa? (shoga wa wif yangu na watoto wanne mwezi mzima kwangu???) hao watoto hata tuition hawasomi? baba wa hao watoto anaagwa wanaenda wapi mwezi mzima? mamy hebu fungua macho....!!! unauhakika ni ushoga tu hapo..!!!???
napata shida moyon hata nashindwa niandike nini..!!!!
 
dada nimepata shida moyoni utadhan wako kwangu..!
my dia wema usizid kipimo!!! wewe ni shangaz wa hao watoto? au huyo mumeo ni baba yao hawajakujulisha? napata shida kuelewa akili ya wif yako ya kubeba ushoga kuleta kwako? mbona nahic kuna mishen ambayo hujaielewa? (shoga wa wif yangu na watoto wanne mwezi mzima kwangu???) hao watoto hata tuition hawasomi? baba wa hao watoto anaagwa wanaenda wapi mwezi mzima? mamy hebu fungua macho....!!! unauhakika ni ushoga tu hapo..!!!???
napata shida moyon hata nashindwa niandike nini..!!!!

Nadhani ni ukarimu Wangu ndio daima huniponza, huyu wifi yangu anaishi comoro na alisema anakuja holiday Na watoto hakusema wangapi walipelekewa hela ya Nauli tuu, Na pia mie sio wifi peke yangu hapa unguja .. Ah hata sijui nisemeje najionea mazongee tuuuu mie...
 
umeshajiuliza kwanini anajiamini hivyo?! shoga wa wifi aje na watoto kwako?ya wapi hayo?!halafu ana do nyumbani kwako?!kuna kitu hapo.binafsi napata hisia huyo ni zaidi ya shoga wa wifi yako na watoto wake pia!hujui la kufanya?!ongea na mumeo awaite mdogo wake na shoga yake.amweleze wazi huyo shoga wa mdogo wake afungashe haraka,akishindwa kumwambia lipo usilolijua! unasema mumeo anashangaa huyo mdada kafuata nini?!sidhani kama anashangaa mpaka moyoni! siwazii hata siku moja shoga wa wifi yangu aje likizo kwangu na wanae!!! apite na kanga moja mbele ya mume wangu namuangalia?never!

Watoto ni wa wifi yangu yeye ndio shoga wa wifi, yani miguu yangu naona nakosa nguvu kila nikisoma comments zenu .....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom