Asprin
Platinum Member
- Mar 8, 2008
- 68,272
- 96,398
Daaah sitaki ata kusikia habari za maiti... hapa nyumbani kwetu alifariki anti yetu,ule mwili wa marehem anti ukawekwa chumbani kwangu kitandani daaah nilitumwa na mama niende nikafunge chumba sasa wakati wa kufunga mlango nikasema ngoja nikafungue jeneza nione daaah nilijikuta niko chini ya mti nimemwagiwa maji napepewa..na tangu siku hyo nilikuwa naweweseka sana bt nilivyokuja kuombewa ile hali ikatulia. mpka leo sina hamu ya kuaga maiti wala kuiona naogopa sana
Aisee mecheka mpaka chozi limetoka. Khaa...
Bro alifiwa na swahiba wake geto. akanipigia simu niende nikampe kampani. Ikawa ni biashara ya kulala na maiti mpk asubuhi.... Niliomba udhuru kidogo nikatafute kampani na ujasiri wa Konyagi. Nikazimeza kama maji. Kurudi geto pombe ikakata, braza ndo kwanza anakoroma, maiti iko kitandani. Nikaenda kuongeza tena nyagi.... kurudi geto ikakata.... dah
Msala ilipofika saa 10 alfajiri, mitambo ikabuma TBL huko na braza ndo mtaalam. Gari ikaja kumchukua akaokoe jahazi. Akanisihi nibaki pale na maiti aende job fasta.... eti maiti hairuhusiwi kulala peke yake. Siku hiyo iliruhusiwa!!!
Yeye kaenda TBL mimi nikaenda bar maiti ikabaki room.
Kulipokucha ndipo nikajua nilikuwa nimelewa mbaya. hata sijui walizika saa ngapi.
Sina urafiki na maiti. Maiti zinisamehe tu.