Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kazi ndogo sana hiyo.
Alikuwepo.
Yupo.
Atakuwepo milele.
He is the ancient of days.

Kazi ya kukuaminisha naiweka kwenye file lenye jina PROJECT MSHAMBA HACHEKWI.

Hili file likikamilika lazima uje tuimbe wote kwaya.
Nataka kujiunga na kwaya yenu
 
Kwa sababu niligundua Mungu hayupo na habari za kuwapo Mungu ni hadithi za kutungwa na watu tu.

Niligundua hivyo baada ya kufikiri sana kuhusu "the problem of evil", yani jinsi gani Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaoweza kuwa na mabaya, dhambi na shida ni contradiction, na mpaka leo hakuna aliyeweza kutatua contradiction hii.
Kuna muda huwa inatubidi kufikiri mbali zaidi, ili kupata majibu yasiyojibika
 
Huwezi kumkuta Muislamu hata akiwa haendi msikitini ,haswali na mfanya maasi akijianika na kujisifia kuwa haendi msikitini ,labda huyo awe ameachana na imani ya mara nyingi huwa ujasiri huo hana kwani nafsi yake itakuwa inamsuta.

Misingi ya Uislamu ni haitakiwi mtu kutangaza uovu wake ikiwa Mwenyezi Mungu amemsitiri kwani ni uovu mkubwa mtu kufanya kibri katika maasi na kujisifia kuliko hata uovu wa kosa lenyewe.Na kuna uwezekano mkubwa asitubie kwa kuona ni kitu kizuri ila yule mwenye hofu na akaficha aibu zake kuna uwezekano mkubwa wa kupata rehma akatubu au kusamehewa.

Ila nashangaa upande wenu kila mtu anafunguka bila wasiwasi kama amefanya jambo ambalo zuri , huu sio uzi wa kwanza upo uzi mwingine watu wakijisifia masiku ambayo wasiyoenda Kanisani wakijiona watabe . Unakuta na mtu humu anahubiri neno la biblia lakini u amkuta kesho anapost uzi jinsi anavyogegeda watoto wa watu tena wakati mwingine akijisifu bila aibu.
Wako sahihi kufunguka ila umenikumbusha kitu, siku moja tulikuwa kwenye harusi ya kiislam nami nilikuwa mwanakamati kwenye bajeti zilikuwepo na bia na zikanunuliwa na kuletwa ukumbini lkn cha ajabu sikuona hata chupa moja ya bia kwenye meza ya mtu lkn mwisho wa sherehe kreti zilrudi tupu.
 
MUNGU HAYUPO, SHETANI HAYUPO, UCHAWI HAUPO.....

hivi vitu unavipa nguvu kwenye akili yako ndo maana unaona vipo....
ili biashara ikue inabidi utoe huduma bora kwa wateja wako kuliko ushindani wako, basi.... hamna nguvu ya ziada.....

najua utabisha, fanya utafiti wako mwenyewe utaweza elewa ninachomaanisha
Tembea uone ndugu.
 
Mwanzo niliacha bila sababu nilijua nitarejea ila baada ya kujua ukweli kwamba roman catholic ni miongon mwa secret societies, na madhebu yote yalianzishwa na watu baada ya kuhasi kanisa la roman catholic, nimeapa kwamba sito kwenda kanisani na kama nitaenda basi nitaenda kimwili kuifurahisha jamii na si kiroho( vatican wana siri nyingi mno)
Na wengi tuko hivyo, ni sababu za kijamii tu wala hakuna la ziada na unashauliwa kwenda kanisani au kujishughulisha na mambo ya kanisa pale unapostaafu shughuli za kiserikali, hii usaidia sana kuongeza umri.
 
Kwanza kitendo cha Mungu kumtoa mwanae kafara, binadamu watoe kafara na Mungu atoe kafara. Tena Mungu alianza na binadamu akagundua swala la misukule. Nikagundua ni michongo tu ya wajanja. Sasa najikita katika imani yangu ya jadi.
 
Pastor aliniombea kwa mbwe mbwe sana akijua nna mapepo alivyoona sianguki akanisukuma kwa nguvu ili nidondoke, aisee hapo uvumilivu ulinishinda nilimtembezea kichapo, huo ndio ulikua mwisho.
Unachangamsha genge kwa stori za kijinga.
 
Nilipo gundua dini inanijenga niwe na hofu ya kitu nisichokijua na kunihusisha na ugomvi wa viumbe nisiowajua ,nakunishauri niamni tu huku wakichukua cheji zangu, nikigoma wanatishia hawatanizika as if wakiniacha bila kunizika ni shida zangu.
Sababu za kijinga mno
 
Na wengi tuko hivyo, ni sababu za kijamii tu wala hakuna la ziada na unashauliwa kwenda kanisani au kujishughulisha na mambo ya kanisa pale unapostaafu shughuli za kiserikali, hii usaidia sana kuongeza umri.
Aisee umetoboa mwamba sasa.! Ni kweli RC ina siri nyingi sana.
 
Hivi kanisani na misikitini kuna nini mwenye kujua anijuze ?
 
Back
Top Bottom