Ushimen
JF-Expert Member
- Oct 24, 2012
- 42,510
- 105,142
Na hapo ukihoji, utasikia eti usiwaseme vibaya watumishi wa Mungu.Mkuu haya ndio yaliliosababisha yote haya yashuhudiwayo.
Kwenda kanisani ni ibada mojawapo, na ibada yoyote ile lazima iwe na sadaka.
Miaka ya hivi karibuni yametokea mabadiliko makubwa sana katika imani, viongozi wa imani ndio waliobadilika na kusababisha haya yote.
Hii imepelekea sadaka kanisa kuwa Kama fashion fulani hivi.
Huku kwetu nisingependa kukutaja, tunaujenzi wa kanisa.
Mimi Ni muamiaji wa eneo hilo kwa Sasa Ni miaka mitano, nilipokuja hapa nilikuta harakati za ujenzi zikiendela na kupamba moto kiasi Cha kusema mwakani tu kanisa tayari.
Lakini huwezi amini mpaka leo hii Ni msingi peke yake ndio umekamilika.
Kipindikile 2016 taarifa za mapato ya ujenzi zilikua zinasoma milioni 800.
Kila siku kila mwezi kila nyakati Ni mchango wa ujenzi wa kanisa.
Jumuiyani huko kila ukipumua Ni ujenzi wa kanisa.
Nimesali makanisa kadhaa mikoa mbali mbali lakini sijawahiona kanisa lenye waumini wanaojitoa Kama hili, sadaka za ibada kwa wiki Ni milion 7.
Michango ya ujenzi milioni 60 kwa mwezi, lakini mwaka karibu wa kumi Ni msingi pekee ulio kamilika katika ujenzi wa kanisa.
Sasa kwa hapa unadhani Ni wangapi waliokatishwa tamaa na hali hii na kupelekea kutokuhudhuria kanisani?
Yaani kuna mmoja ninamfahamu, amezaa na bidada flani hapa mtaani na anamuhudumi kama kawaida na anaenda pale kama mume kabisa.
Kuna mwingine yeye tunakatanae maji baa kila jioni.
Kuna mwingine yeye alipata ajali na gari la kanisa, akilwa na mhudumu wa bar ambae akafariki papohapo.
Kwakweli minaenda kanisani ili nikamuabudu Mungu wangu tu, mengine huwa sitaki hata kuyafikiria


