Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Kwanini uliacha kwenda kanisani?

Mkuu haya ndio yaliliosababisha yote haya yashuhudiwayo.

Kwenda kanisani ni ibada mojawapo, na ibada yoyote ile lazima iwe na sadaka.

Miaka ya hivi karibuni yametokea mabadiliko makubwa sana katika imani, viongozi wa imani ndio waliobadilika na kusababisha haya yote.

Hii imepelekea sadaka kanisa kuwa Kama fashion fulani hivi.

Huku kwetu nisingependa kukutaja, tunaujenzi wa kanisa.
Mimi Ni muamiaji wa eneo hilo kwa Sasa Ni miaka mitano, nilipokuja hapa nilikuta harakati za ujenzi zikiendela na kupamba moto kiasi Cha kusema mwakani tu kanisa tayari.

Lakini huwezi amini mpaka leo hii Ni msingi peke yake ndio umekamilika.

Kipindikile 2016 taarifa za mapato ya ujenzi zilikua zinasoma milioni 800.

Kila siku kila mwezi kila nyakati Ni mchango wa ujenzi wa kanisa.

Jumuiyani huko kila ukipumua Ni ujenzi wa kanisa.

Nimesali makanisa kadhaa mikoa mbali mbali lakini sijawahiona kanisa lenye waumini wanaojitoa Kama hili, sadaka za ibada kwa wiki Ni milion 7.

Michango ya ujenzi milioni 60 kwa mwezi, lakini mwaka karibu wa kumi Ni msingi pekee ulio kamilika katika ujenzi wa kanisa.

Sasa kwa hapa unadhani Ni wangapi waliokatishwa tamaa na hali hii na kupelekea kutokuhudhuria kanisani?
Na hapo ukihoji, utasikia eti usiwaseme vibaya watumishi wa Mungu.
Yaani kuna mmoja ninamfahamu, amezaa na bidada flani hapa mtaani na anamuhudumi kama kawaida na anaenda pale kama mume kabisa.
Kuna mwingine yeye tunakatanae maji baa kila jioni.
Kuna mwingine yeye alipata ajali na gari la kanisa, akilwa na mhudumu wa bar ambae akafariki papohapo.
Kwakweli minaenda kanisani ili nikamuabudu Mungu wangu tu, mengine huwa sitaki hata kuyafikiria
 
Unakuta Msanii ambae Ni KIOO Cha jamii,

Mlevi wa sigara na pombe wa kupindukia, anaimba matusi kibao kwenye nyimbo zake, anachezesha wanawake uchi kwny video zake.

anatuharibia VIJANA wetu.

Akishapata pesa kutoka kwenye iyo kazi yake haramu, Anaituma mkoani kujengea nyumba ya ibada.

Siku moja kabla uzinduzi,
Anapanda usafiri wa Umma, anawalipia nauli watu wote na pombe za bure.

Alfajiri,
Watu wanafika wamelewa mpk wamejinyea.

Saa 3 asbuhi,
anaenda kuzindua nyumba ya ibada.
Viongoz wa dini wanampokea na kumlaki Kama shujaa.

Saa 8 mchana,
Anapiga show kwenye uwanja wa mpira, wamama,wababa, VIJANA, na watoto wanalewa pombe,wanacheza nyimbo za ngono.

Viongozi wa dini wako kimya
 
Na hapo ukihoji, utasikia eti usiwaseme vibaya watumishi wa Mungu.
Yaani kuna mmoja ninamfahamu, amezaa na bidada flani hapa mtaani na anamuhudumi kama kawaida na anaenda pale kama mume kabisa.
Kuna mwingine yeye tunakatanae maji baa kila jioni.
Kuna mwingine yeye alipata ajali na gari la kanisa, akilwa na mhudumu wa bar ambae akafariki papohapo.
Kwakweli minaenda kanisani ili nikamuabudu Mungu wangu tu, mengine huwa sitaki hata kuyafikiria
Yaan boss kwa hali ya Sasa huko kanisani kusema unaenda kumuabudu Mungu huwenda ukajidanganya aisee labda kusema tunaenda kujumuika tu na jamii.

Mimi binafsi sina shida na matendo ya kiongozi wangu wa kiroho, kujulika anataembea na fulani au ana mahusiano na mtu mfulani au anakunywa sana pombe kwangu sio shida! Ni bahati mbaya tuu imejulikana ila kila mmoja ana matendo yake mimi na we na nafsi zetu sina tuhukumu.

Kilicho nisikitisha kwa upande wangu Ni ile wakiwa katika ibada waliacha kulihubiri kwa usahihi Neno la Mungu kwa kiasi walichojaliwa badala yake wamegeukia mipasho na umbea! Mpaka maungamo ya watu wanayasema ila tu hawataji jina, na tunakoelekea watakuja kutaja tu fulani jana aliungama hivi na vile.

Wao kwa wengi wao mahubiri yanayolenga michango na matoleo ndio yaelezwa kwa usahihi na kwa muda mrefu sana.
Nayo haya ndio sababu ya vijana wengi kutoenda kanisani, achilimbali matabaka wanayoweka ya wenye nacho na wasio nacho.
 
Naendaga mara mojamoja kumwabudu Mungu wangu mengine nayajua mengi sana ambayo hata mimi nayafanya na ninafanya nao ila nikiwaza sote ni binadamu na nikikumbuka bila unafki maisha hayaendi nawaza ukuu wa Mungu ndani yangu licha ya maovu yangu natakiwa kushukuru.

Leo nimenda kanisani but last time kwenda ilikua usiku wa pasaka kidogo niaibike kumbe kwenye kutakiana amani waumini wana-wave mimi nilikua nataka kushika mtu mkono

Anyway nasubiri mvua ikate niende home.
Have a blessed Sunday
 
Niliacha kwa sababu ya wale dada zetu wanao tuvalia nguo za kutamanisha kanisani.

Niliona wazi na jiongezea dhambi tu ndani ya kanisa kwa kuwa taman
Hapo ninatilia mashaka na afya yako ya mwili au akili.

Hakuna mwanaume 'timamu' anayelaani kuangalia mwanamke mzuri hapa duniani.

Kuangalia urembo wa asili walioumbwa nao wanawake si dhambi pia ni dawa inayotibu msongo wa mawazo.

Nimeshangaa sana kukutana na comment kama hii itokayo kwa mtu mwanaume anayedai kulaani kuangalia wanawake wazuri wazuri!
 
Viongozi wa kanisa langu kubaki kimya kipindi serikali inatesa, kuua na kubambikia kesi wapinzani.

Siendi church labda nje ya nchi au nijiridhishe nyendo za anayeongoza kanisa kuhusu itikadi zake.
 
Huwa kuna sababu mbalimbali ambazo humfanya mtu kutokupenda kuhudhuria ibada siku ya Jumamosi au Jumapili (kutokana na dhehebu).

Mimi sababu ilinifanya nisiwe nahudhuria kanisani ni pale mchungaji alipokuwa anahubiri kuhusu sadaka na matoleo tu kwa ibada tatu mfululizo.

Nini sababu yako?
Mimi mapdri wangu wamekua kituko,kila shetani akienda kusali wanampa nafasi ya kuropoka madhabahuni...kanisa limekua jukwaa la kumsifu shetani
 
Baada ya kugundua pasi shaka kuwa Yesu kristo wa Nazareth ni Mwafrika Mweusi. Baaasi nikaona kweli niliingizwa chaka mbaya!!!! siku hizi wanaongea nawatazamaaa juuu halafu nawashushaaa then napumuaaa!!!

Halafu kama wananusaga hivi, siku hizi hawanishobokei km zamani!
 
Missada lazima inatoka vatican hawataki msiende
 
Dah mimi hata sielewii nilijikuta tu sipendi kwenda kanisani tu
 
Dahhhh.....
Ila kwetu michango imezidi mnoooo.....
1. Zaka
2.Sadaka
3. Mavuno
4. Utoto mtakatifu
5. Ujenzi wa nyumba ya Paroko
6. Ukarabati wa kanisa
7. Mfuko wa parokia
8. Wageni wa kanisa
9. Viti vya jumuiya
Ongeza
Ujenzi wa Ukuta
Ujenzi wa Duka la Kanisa
Ujenzi wa Ukumbi
Chakula cha Seminary

Ili hali ukipeleka mtoto shule hawakupi discount wala kwenye ukumbi.


Michango ya Jumuiya na vyama vya kanisa kibao, kufuatana hadi nyumbani hii ndio huwa siipendi
 
Huwa kuna sababu mbalimbali ambazo humfanya mtu kutokupenda kuhudhuria ibada siku ya Jumamosi au Jumapili (kutokana na dhehebu).

Mimi sababu ilinifanya nisiwe nahudhuria kanisani ni pale mchungaji alipokuwa anahubiri kuhusu sadaka na matoleo tu kwa ibada tatu mfululizo.

Nini sababu yako?
VIWAWA, KAPU LA MAMA, KAPU LA PAROKO, KAPU LA MAKATEKISTA, KAPU LA MASISTA, KAPU LA REDIO MARIA, UJENZI WA KANISA, SADAKA, SHUKURANI, KUMSHIKA MKONO BABA PAROKO, KAPU LA BABA ASKOFU, alafu wao tunavyolalamika maisha magumu mambo hayaendi wao wamekalia kusifia na kujipendekeza kwa Mzee wa Chato
 
Ninyi endeleeni tu kutokwenda kanisani kwa amani, hakuna anayewahukumu, japokuwa naamini hapa yenyewe nafsi zenu zinawasuta ndiyo maana mnajifanya kutafuta justification tu ya matendo yenu hamna lolote..!
Halafu we mdada nimeanza kukupenda bure...
 
Carleen Ungekuwa muumini wa kanisa la Gwajiboy ungeendelea kwenda kanisani.. kwa sasa akiwa ni mchungaji/mwanasiasa. Ukijumuisha na swala la wazi lililotokea Kawe linalovunja amri ya 'Usiibe' na 'Usiseme uongo'....Kuna msemo unasema 'hauwezi kuwa mwanasiasa bila kusema uongo'
Tunasubiri kutimiza aliyotuahidi wana Kawe Sasa. Hapo ndipo mtego ulipo na huduma yake
 
Back
Top Bottom