Kwanini tunaibeba DP World kiasi hiki?

Kwanini tunaibeba DP World kiasi hiki?

Inauma sana kuona kuwa wabaya wa kwanza wa nchi yetu ni watawala wetu wenyewe na chawa wao - inauma asilani! Tusumbuliwe na kushindana na wa nje, hata watu wetu wa ndani nao watusumbue na kushindana nao??!!

Hivi kwanini tunatesana, tunalitesa taifa na kuvitesa vizazi vijavyo kwa kuukubali utumwa wa kifikra na wa kiuchumi??!!
Screenshot_20230716-000531.jpg
F0S-9CpX0AA8ieA.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ni kafara la kukimbiza moto basi limetubamba kisawasawa...Na kama ni dozi ya upumbavu aliyetunywesha katu overdose kasoro wachache mno...!

Kwa makosa makubwa na ya wazi kiasi kile kwenye ule mkataba wa DPW na Tanzania kama sisi ndio tunataka kuwekeza kwao wallah nakwambieni ungechanwa mapema asubuhi tena kwa matusi na kejeli za kila aina!

Sisi sote tu mashuhuda namna tunavyotendewa nje ya nchi kwa makosa madogo mno tena sometimes kwenye nyaraka tuu ambayo yanaweza kurekebishwa hapo hapo

Mali zetu nyingi zilizokamatwa nje ya nchi si kwamba zote zilikamatwa kihalali, nyingine ni makosa madogo tu ya kisheria
Fidia tulizolipa na tunazoendelea kulipa nje ya nchi baada ya kushindwa kesi, nyingine zinatokana na kukosa uzalendo tu wa wanasheria wetu na wahusika wetu na kushindwa kupigania na kuonesha shida ilipo

Kipindi kile cha corona ni wangapi wamesahau namna mamlaka za Dubai zilivyowanyanyasa na kuwadhalilisha wabongo ambao nyaraka zao za chanjo zilikuwa na makosa madogo mnoo.. Kuna baadhi walirudishwa airport na kupoteza muda na nauli zao

Magereza za Dubai zina watanzania kibao kwa kesi mbalimbali ambazo nyingine ni za kubambikiwa, kushukiwa na nyingine makosa madogo mno... Sisemi kutenda kosa hata liwe dogo ni halali la hasha bali kuna baadhi ya makosa yanahitaji kuelimishwa tuu

Wakenya wanaweza kuwa mashuhuda wazuri kwa mabinti zao wanaokwenda arabuni kufanya kazi mbalimbali hasa za ndani, yale wanayofanyiwa kule hakuna mwafrika anaweza thubutu kumfanyia mgeni
Kwahiyo linapokuja swala la nchi yao.. Wenzetu hawana utani hawana huruma na hawana chembe ya utu wala ubinadamu.. Wananyoosha rula..!

Sisi huku bongo ndio kwanza tunawasaidia wageni
Kuvunja sheria mbalimbali
Kuwatetea wanapoharibu
Kuiba
Kukwepa kodi
Kuwatendea ndugu zetu mabaya nknk..
Kwao wao hawana huu upuuzi hata nukta.. Sana sana utashirikiana naye ila akikupa kisogo unadakwa.. Kakuchomam, na ndio atakuwa shahidi wa kukuangamiza ukipandishwa kizimbani

Sasa hili bango la watanzania wenzetu kuutetea mkataba mbovu mbovu mbovu kiasi kile huu uthubutu wanaupata wapi? Na mbaya zaidi wakiongoza na CCM wenyewe.. Hii ni aibu ni fedheha na ni laana kwa taifa hili.. Huku ni kudhalilishwa kulikovuka mipaka yote!

Hakuna anayekataa uwekezaji, kinachokataliwa na wananchi wazalendo ni mkataba mbovu, wenye makosa yasiyorekebishika na usio na maslahi yoyote kwa taifa.. Kwani kuna shida gani mamlaka zikitamka kuukataa na kuufuta?
Kwani kuna shida gani kuanza upya?
Kwani kuna shida gani kuwatafuta wawekezaji wengine?
Kwani ni lazima huyu dp na si mwingine yoyote? Kwanini?

Yanayofanyika sirini yakiwekwa bayana matokeo huwa hasi! Mambo haya yalianza 2022 kwa siri, taifa halikushirikishwa tangu mwanzo.. Kila kitu kingekuwa bayana tangu awali kwa uwazi na kwa uzalendo wa taifa.. Tusingefika leo hapa tulipo

Natambua wazi nguvu ya pesa ilivyoshawishi maamuzi yote mpaka sasa japo hili litakanushwa kwa viwango vyote, lakini mwenye macho haambiwi tazama!
Natambua ubinafsi wa viongozi wengi wa ccm wanaotegemea kujikomba na kujipendekeza dpw itakapoanza kazi ili wapate chochote na kuwatafutia vibarua ndugu, jamaa, marafiki na michepuko yao.. Hapa ndio ukomo wao wa kufikiri unapoishia..!

Huu unaotutikisa mpaka sasa ni mmoja tu kati ya ile 37 iliyosainiwa huko...

Good morning TanganyikaView attachment 2690651

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndo tumeshanasa kwenye dude linaloitwa makubaliano mkataba, liko kama sumaku.
 
Huu mkataba unavyotetewa kwa nguvu zote lazima Rupia imeshapenyezwa
Mwarabu anawauliza ccm mnatoa hamtoi
watu wanajua wanachofanya
Sidhani kama wanaosaini mikataba hawajui kuwa mikataba ni ya hovyo. Inawezekana hii mikataba ni deal kabisa..... wanasaini wakiwa wanajua kabisa huko mbele itavunjwa na wanakubaliana na mwekezaji mshiko wao kabisa mkataba utakapovunjwa na taifa kupigwa faini.

Haiingii akilini kwamba tangu miaka ya tisini serikali ile Ile ya chama kile kile iendelee kusaini madeal ya ajabu ajabu. Kwamba haijajifunza kitu tangu lile deal la kwanza la hovyo la air Tanzania kukaundwa air alliance? Mikataba ya migodini, gesi....this might be Front and back corruption
 
Hata mimi nina wasiwasi na hilo! Mtu anadai eti DPw watawajengea uwezo TPA kuendesha bandari kisasa, lakini mkataba unataja kuwa DPW watawapa TPA technolojia ya kuendeshea bandari ya majahazi zitakazokuwa chini yao (soma appendix 1, kipengele namba 2 na namba 7 kwa pamoja). Sasa kweli bandari ya majahazi ndo kujengewa uwezo kweli?
Lugha ya malikia Ile, shule zenyewe kayumba, mashungi mwenyewe alifeligi karisitigi.
 
Nguvu Ccm wanayoitumia kwenye hili jambo kuielimisha wananchi ingetumika na kwenye mingine ningewaona wana uchungu na hii nchi.

 
Kama ni kafara la kukimbiza moto basi limetubamba kisawasawa...Na kama ni dozi ya upumbavu aliyetunywesha katu overdose kasoro wachache mno...!

Kwa makosa makubwa na ya wazi kiasi kile kwenye ule mkataba wa DPW na Tanzania kama sisi ndio tunataka kuwekeza kwao wallah nakwambieni ungechanwa mapema asubuhi tena kwa matusi na kejeli za kila aina!

Sisi sote tu mashuhuda namna tunavyotendewa nje ya nchi kwa makosa madogo mno tena sometimes kwenye nyaraka tuu ambayo yanaweza kurekebishwa hapo hapo

Mali zetu nyingi zilizokamatwa nje ya nchi si kwamba zote zilikamatwa kihalali, nyingine ni makosa madogo tu ya kisheria
Fidia tulizolipa na tunazoendelea kulipa nje ya nchi baada ya kushindwa kesi, nyingine zinatokana na kukosa uzalendo tu wa wanasheria wetu na wahusika wetu na kushindwa kupigania na kuonesha shida ilipo

Kipindi kile cha corona ni wangapi wamesahau namna mamlaka za Dubai zilivyowanyanyasa na kuwadhalilisha wabongo ambao nyaraka zao za chanjo zilikuwa na makosa madogo mnoo.. Kuna baadhi walirudishwa airport na kupoteza muda na nauli zao

Magereza za Dubai zina watanzania kibao kwa kesi mbalimbali ambazo nyingine ni za kubambikiwa, kushukiwa na nyingine makosa madogo mno... Sisemi kutenda kosa hata liwe dogo ni halali la hasha bali kuna baadhi ya makosa yanahitaji kuelimishwa tuu

Wakenya wanaweza kuwa mashuhuda wazuri kwa mabinti zao wanaokwenda arabuni kufanya kazi mbalimbali hasa za ndani, yale wanayofanyiwa kule hakuna mwafrika anaweza thubutu kumfanyia mgeni
Kwahiyo linapokuja swala la nchi yao.. Wenzetu hawana utani hawana huruma na hawana chembe ya utu wala ubinadamu.. Wananyoosha rula..!

Sisi huku bongo ndio kwanza tunawasaidia wageni
Kuvunja sheria mbalimbali
Kuwatetea wanapoharibu
Kuiba
Kukwepa kodi
Kuwatendea ndugu zetu mabaya nknk..
Kwao wao hawana huu upuuzi hata nukta.. Sana sana utashirikiana naye ila akikupa kisogo unadakwa.. Kakuchomam, na ndio atakuwa shahidi wa kukuangamiza ukipandishwa kizimbani

Sasa hili bango la watanzania wenzetu kuutetea mkataba mbovu mbovu mbovu kiasi kile huu uthubutu wanaupata wapi? Na mbaya zaidi wakiongoza na CCM wenyewe.. Hii ni aibu ni fedheha na ni laana kwa taifa hili.. Huku ni kudhalilishwa kulikovuka mipaka yote!

Hakuna anayekataa uwekezaji, kinachokataliwa na wananchi wazalendo ni mkataba mbovu, wenye makosa yasiyorekebishika na usio na maslahi yoyote kwa taifa.. Kwani kuna shida gani mamlaka zikitamka kuukataa na kuufuta?
Kwani kuna shida gani kuanza upya?
Kwani kuna shida gani kuwatafuta wawekezaji wengine?
Kwani ni lazima huyu dp na si mwingine yoyote? Kwanini?

Yanayofanyika sirini yakiwekwa bayana matokeo huwa hasi! Mambo haya yalianza 2022 kwa siri, taifa halikushirikishwa tangu mwanzo.. Kila kitu kingekuwa bayana tangu awali kwa uwazi na kwa uzalendo wa taifa.. Tusingefika leo hapa tulipo

Natambua wazi nguvu ya pesa ilivyoshawishi maamuzi yote mpaka sasa japo hili litakanushwa kwa viwango vyote, lakini mwenye macho haambiwi tazama!
Natambua ubinafsi wa viongozi wengi wa ccm wanaotegemea kujikomba na kujipendekeza dpw itakapoanza kazi ili wapate chochote na kuwatafutia vibarua ndugu, jamaa, marafiki na michepuko yao.. Hapa ndio ukomo wao wa kufikiri unapoishia..!

Huu unaotutikisa mpaka sasa ni mmoja tu kati ya ile 37 iliyosainiwa huko...

Good morning TanganyikaView attachment 2690651

Sent using Jamii Forums mobile app

eb5ae8d3-fdc5-4954-a51f-6268c5b129e5-jpeg.1971057
 
Kama ni kafara la kukimbiza moto basi limetubamba kisawasawa...Na kama ni dozi ya upumbavu aliyetunywesha katu overdose kasoro wachache mno...!

Kwa makosa makubwa na ya wazi kiasi kile kwenye ule mkataba wa DPW na Tanzania kama sisi ndio tunataka kuwekeza kwao wallah nakwambieni ungechanwa mapema asubuhi tena kwa matusi na kejeli za kila aina!

Sisi sote tu mashuhuda namna tunavyotendewa nje ya nchi kwa makosa madogo mno tena sometimes kwenye nyaraka tuu ambayo yanaweza kurekebishwa hapo hapo

Mali zetu nyingi zilizokamatwa nje ya nchi si kwamba zote zilikamatwa kihalali, nyingine ni makosa madogo tu ya kisheria
Fidia tulizolipa na tunazoendelea kulipa nje ya nchi baada ya kushindwa kesi, nyingine zinatokana na kukosa uzalendo tu wa wanasheria wetu na wahusika wetu na kushindwa kupigania na kuonesha shida ilipo

Kipindi kile cha corona ni wangapi wamesahau namna mamlaka za Dubai zilivyowanyanyasa na kuwadhalilisha wabongo ambao nyaraka zao za chanjo zilikuwa na makosa madogo mnoo.. Kuna baadhi walirudishwa airport na kupoteza muda na nauli zao

Magereza za Dubai zina watanzania kibao kwa kesi mbalimbali ambazo nyingine ni za kubambikiwa, kushukiwa na nyingine makosa madogo mno... Sisemi kutenda kosa hata liwe dogo ni halali la hasha bali kuna baadhi ya makosa yanahitaji kuelimishwa tuu

Wakenya wanaweza kuwa mashuhuda wazuri kwa mabinti zao wanaokwenda arabuni kufanya kazi mbalimbali hasa za ndani, yale wanayofanyiwa kule hakuna mwafrika anaweza thubutu kumfanyia mgeni
Kwahiyo linapokuja swala la nchi yao.. Wenzetu hawana utani hawana huruma na hawana chembe ya utu wala ubinadamu.. Wananyoosha rula..!

Sisi huku bongo ndio kwanza tunawasaidia wageni
Kuvunja sheria mbalimbali
Kuwatetea wanapoharibu
Kuiba
Kukwepa kodi
Kuwatendea ndugu zetu mabaya nknk..
Kwao wao hawana huu upuuzi hata nukta.. Sana sana utashirikiana naye ila akikupa kisogo unadakwa.. Kakuchomam, na ndio atakuwa shahidi wa kukuangamiza ukipandishwa kizimbani

Sasa hili bango la watanzania wenzetu kuutetea mkataba mbovu mbovu mbovu kiasi kile huu uthubutu wanaupata wapi? Na mbaya zaidi wakiongoza na CCM wenyewe.. Hii ni aibu ni fedheha na ni laana kwa taifa hili.. Huku ni kudhalilishwa kulikovuka mipaka yote!

Hakuna anayekataa uwekezaji, kinachokataliwa na wananchi wazalendo ni mkataba mbovu, wenye makosa yasiyorekebishika na usio na maslahi yoyote kwa taifa.. Kwani kuna shida gani mamlaka zikitamka kuukataa na kuufuta?
Kwani kuna shida gani kuanza upya?
Kwani kuna shida gani kuwatafuta wawekezaji wengine?
Kwani ni lazima huyu dp na si mwingine yoyote? Kwanini?

Yanayofanyika sirini yakiwekwa bayana matokeo huwa hasi! Mambo haya yalianza 2022 kwa siri, taifa halikushirikishwa tangu mwanzo.. Kila kitu kingekuwa bayana tangu awali kwa uwazi na kwa uzalendo wa taifa.. Tusingefika leo hapa tulipo

Natambua wazi nguvu ya pesa ilivyoshawishi maamuzi yote mpaka sasa japo hili litakanushwa kwa viwango vyote, lakini mwenye macho haambiwi tazama!
Natambua ubinafsi wa viongozi wengi wa ccm wanaotegemea kujikomba na kujipendekeza dpw itakapoanza kazi ili wapate chochote na kuwatafutia vibarua ndugu, jamaa, marafiki na michepuko yao.. Hapa ndio ukomo wao wa kufikiri unapoishia..!

Huu unaotutikisa mpaka sasa ni mmoja tu kati ya ile 37 iliyosainiwa huko...

Good morning TanganyikaView attachment 2690651

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna mambo muhimu sana watu hawajadili kwenye huu mkataba
Mfano;
1. Je mwekezaji atanufaishaje watanzania (Kodi kiasi gani na Ajira?)
2. Ni mtaji kiasi gani unahitajika ili tuweze kupata Kodi tajwa hapo juu
3. Kuna watanzania au shirika la kitanzania linaweza kufanya huo uwekezaji?
4. Je mwekezaji anapewa nini hasa kwenye bandari (kushusha mizigo? technologia? etc

Sijawahi kusikia Biashara yoyote Duniani inayojadiliwa bila kutumia nguvu kubwa kujua ni faida kiasi gani Nchi itapata halafu wakisha ona inalipa ndio wanaenda upande wa pili kuhakikisha mkataba unakaa vizuri.
(kwa mjadala unaoendelea, sioni faida tutakayopata ikijadiliwa kitu kinachonifanya nione kuwa, wanaoendesha huu mjadala sio wafanya biashara)

Ninachomaanisha ni kuwa; Kama Biashara inalipa; tutumie wataalam wetu kurekebisha mkataba ukae vizuri tupate mapato na naamini kabisa watu wengi wanalalamika kwa ushabiki na hata wakiulizwa wanacho lalamikia wala hawakijui....wanabakia tu bandari inauzwa.........ukiwauliza wamesoma wapi hawajui.....
 
Kwa Malumbano yanayoendelea naona kweli kuna ukwasi kwenye mkataba
Ila Mama aangalie ikiwezekana/ikimpendeza aseme sasa tunaanza upya maana wengi naona hawakatai uwekezaji bali muundo wa mkataba
 
watu wanajua wanachofanya
Sidhani kama wanaosaini mikataba hawajui kuwa mikataba ni ya hovyo. Inawezekana hii mikataba ni deal kabisa..... wanasaini wakiwa wanajua kabisa huko mbele itavunjwa na wanakubaliana na mwekezaji mshiko wao kabisa mkataba utakapovunjwa na taifa kupigwa faini.

Haiingii akilini kwamba tangu miaka ya tisini serikali ile Ile ya chama kile kile iendelee kusaini madeal ya ajabu ajabu. Kwamba haijajifunza kitu tangu lile deal la kwanza la hovyo la air Tanzania kukaundwa air alliance? Mikataba ya migodini, gesi....this might be Front and back corruption
Kuna watu ndani ya ccm wanatakiwa wahukumiwe kunyong'wa hadi kufa
mana ni zaidi ya majangili.
 
Sijawahi ona mkataba unaotetewa kama huu, sijui hawaoni kwamba jinsi wanavyokazana ndiyo nasi mashaka yanaongezeka!
Ni kama serikali inatubembeleza jamani kubalini jamani vinginevyo....
Sitaki kufikiria Samia ana wakati mgumu kiasi gani kwa sasa...sijui ni pori gani aliloingia huyu mama round hii...anyways muda utaongea
 
Kuna tetesi ccm wanahitaji pesa za uchaguzi mwakani hayati mkapa kwenye kitabu chake amekiri kuiba zaidi ya bil 300 kufanyia kampeni mwaka 2005 sasa imepita miaka 19 sasa pesa nyingi zinahitajika kufanyia kampeni mwakani

Chama kinachowaza kupata ushindi wa kishindo ni ngumu kuleta maendeleo matokeo yake ndio haya
You right
 
Back
Top Bottom