Kama ni kafara la kukimbiza moto basi limetubamba kisawasawa...Na kama ni dozi ya upumbavu aliyetunywesha katu overdose kasoro wachache mno...!
Kwa makosa makubwa na ya wazi kiasi kile kwenye ule mkataba wa DPW na Tanzania kama sisi ndio tunataka kuwekeza kwao wallah nakwambieni ungechanwa mapema asubuhi tena kwa matusi na kejeli za kila aina!
Sisi sote tu mashuhuda namna tunavyotendewa nje ya nchi kwa makosa madogo mno tena sometimes kwenye nyaraka tuu ambayo yanaweza kurekebishwa hapo hapo
Mali zetu nyingi zilizokamatwa nje ya nchi si kwamba zote zilikamatwa kihalali, nyingine ni makosa madogo tu ya kisheria
Fidia tulizolipa na tunazoendelea kulipa nje ya nchi baada ya kushindwa kesi, nyingine zinatokana na kukosa uzalendo tu wa wanasheria wetu na wahusika wetu na kushindwa kupigania na kuonesha shida ilipo
Kipindi kile cha corona ni wangapi wamesahau namna mamlaka za Dubai zilivyowanyanyasa na kuwadhalilisha wabongo ambao nyaraka zao za chanjo zilikuwa na makosa madogo mnoo.. Kuna baadhi walirudishwa airport na kupoteza muda na nauli zao
Magereza za Dubai zina watanzania kibao kwa kesi mbalimbali ambazo nyingine ni za kubambikiwa, kushukiwa na nyingine makosa madogo mno... Sisemi kutenda kosa hata liwe dogo ni halali la hasha bali kuna baadhi ya makosa yanahitaji kuelimishwa tuu
Wakenya wanaweza kuwa mashuhuda wazuri kwa mabinti zao wanaokwenda arabuni kufanya kazi mbalimbali hasa za ndani, yale wanayofanyiwa kule hakuna mwafrika anaweza thubutu kumfanyia mgeni
Kwahiyo linapokuja swala la nchi yao.. Wenzetu hawana utani hawana huruma na hawana chembe ya utu wala ubinadamu.. Wananyoosha rula..!
Sisi huku bongo ndio kwanza tunawasaidia wageni
Kuvunja sheria mbalimbali
Kuwatetea wanapoharibu
Kuiba
Kukwepa kodi
Kuwatendea ndugu zetu mabaya nknk..
Kwao wao hawana huu upuuzi hata nukta.. Sana sana utashirikiana naye ila akikupa kisogo unadakwa.. Kakuchomam, na ndio atakuwa shahidi wa kukuangamiza ukipandishwa kizimbani
Sasa hili bango la watanzania wenzetu kuutetea mkataba mbovu mbovu mbovu kiasi kile huu uthubutu wanaupata wapi? Na mbaya zaidi wakiongoza na CCM wenyewe.. Hii ni aibu ni fedheha na ni laana kwa taifa hili.. Huku ni kudhalilishwa kulikovuka mipaka yote!
Hakuna anayekataa uwekezaji, kinachokataliwa na wananchi wazalendo ni mkataba mbovu, wenye makosa yasiyorekebishika na usio na maslahi yoyote kwa taifa.. Kwani kuna shida gani mamlaka zikitamka kuukataa na kuufuta?
Kwani kuna shida gani kuanza upya?
Kwani kuna shida gani kuwatafuta wawekezaji wengine?
Kwani ni lazima huyu dp na si mwingine yoyote? Kwanini?
Yanayofanyika sirini yakiwekwa bayana matokeo huwa hasi! Mambo haya yalianza 2022 kwa siri, taifa halikushirikishwa tangu mwanzo.. Kila kitu kingekuwa bayana tangu awali kwa uwazi na kwa uzalendo wa taifa.. Tusingefika leo hapa tulipo
Natambua wazi nguvu ya pesa ilivyoshawishi maamuzi yote mpaka sasa japo hili litakanushwa kwa viwango vyote, lakini mwenye macho haambiwi tazama!
Natambua ubinafsi wa viongozi wengi wa ccm wanaotegemea kujikomba na kujipendekeza dpw itakapoanza kazi ili wapate chochote na kuwatafutia vibarua ndugu, jamaa, marafiki na michepuko yao.. Hapa ndio ukomo wao wa kufikiri unapoishia..!
Huu unaotutikisa mpaka sasa ni mmoja tu kati ya ile 37 iliyosainiwa huko...
Good morning Tanganyika
View attachment 2690651
Sent using
Jamii Forums mobile app