Kwanini tunaibeba DP World kiasi hiki?

Kwanini tunaibeba DP World kiasi hiki?

Hivi kwa akili zako hizi za kucharuka kwa masoko hayo ya hisa ya shanghai etc sheria zake leo 2023 ndio hizo hizo zilitawala mwaka 1979 wakati wa mageuzi ya kiuchumi halafu umekaa nchi za watu kwa hiyo sisi hata tukitaka kujikwamua tufuate sera za mageuzi ya wakati ule wa kujikwamua au unataka tufuate sera za sasa za modern rich china iliyojitosheleza kila kitu tatizo sio kuwa na fikra je fikra zako zitakukwamua hapo ulipo kimkakati mwenzio alishapanda sasa anavuna wewe ndio kwanza unapanda halafu unajiweka kwenye same position ndugu yangu mbona ushafeli acha mhemko mambo yanataka fikra kuu na strategy usione vyaelea lazima ukae chini uviunde kwa utulivu
Kwahiyo kwasababu ya umasikin wako unaweza kuruhusu tajiri aje ajenge gorofa hapo kwako alimiliki milele upewe visenti kidogo tu kisa na wewe uonekane uko kwenye gorofa. Hiv huu umasikin wa akili umetokea wapi nchi hii Mzee. Dunia yote inatembea katika mfumo wa win win situation wewe unamuachia mkeo tajiri kisa anawapa hela. Poor minded
 
Hembu tuambiane ukweli ni mradi gani Tanzania uliofanywa ambao utaingiza trillioni 27 directly achilia mbali other multiplier, strategically ni win ,ila too emotional individuals watapiga tu makelele. Hata akina Deng Xiaping walionekana wamemsaliti MaO ila wakajenga modern day China muda utaongea .
Usijidanganye nothing will benefit this country out of this stupid contract!
 
Wakati wa dubai wenyewe pale kwao wanayo mahakama maalumu ndani ya zile free economic zone yaani DIFC COURT ambayo haitumii sheria za serikali ya dubai yenyewe inatumia common english law kusolve dispute zote kwa kampuni zote zilizomo au zinazofanya shughuli zake ndani ya dubai financial international centre na zile free economic zone sisi unadhani hayo tunayaweza halafu sisi wapiga kelele huku tunataka investor na fdi hapo unapata jibu kwa nini wawekezaji wakubwa wanakimbilia huko na wao pia sheria zao zinaruhusu mtu kupata land for 99 years au private ownership ktk zile special economic zone zao nadhani na wao walishauza nchi yao ama vipi ???
Sasa kama wao waliuza na sisi tufuate ujinga wao tuuze?
 
Swali la kijuinga kabisa limebeba bichwa la hii habari.

Namuuliza, anawafahamu Hutchinson waliokuwepo bandari ya Dar kwa jina la TICTS?

Walikuwepo kwa miaka mingapi?


Pia namuuliza tena, hao DP World wapo bandari ipi ya Tanzania hivi sasa?


Nafahamu hakuna ataeyajibu hayo maswali kiwepesi wake.
 
Ilitabiriwa na Wazee kuwa NCHI YETU itatawaliwa na RAIS ambaye hakushiriki Kufanya Campain Wala kupigiwa Kura .

Maana yake MIPANGO anaweza AKAWA RAIS Muda wowote.
MAMA SAA 100 AMEUZA BANDARI.
 
Mapaka👇😁😁😁
16884572500841.jpg
 
Ilitabiriwa na Wazee kuwa NCHI YETU itatawaliwa na RAIS ambaye hakushiriki Kufanya Campain Wala kupigiwa Kura .

Maana yake MIPANGO anaweza AKAWA RAIS Muda wowote.
MAMA SAA 100 AMEUZA BANDARI.
Maana yake MIPANGO anaweza AKAWA RAIS Muda wowote.
MAMA SAA 100 AMEUZA BANDARI

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa kama wao waliuza na sisi tufuate ujinga wao tuuze?
Ndio tuache nongwa maana mazingira na terms za uwekezaji kona nyingi za maana zenye tija ulimwenguni ziko hivyo ,tuache kubehave kama tuko zama za azimio la Arusha huko tulishatoka siku nyingi .
 
Ndio tuache nongwa maana mazingira na terms za uwekezaji kona nyingi za maana zenye tija ulimwenguni ziko hivyo ,tuache kubehave kama tuko zama za azimio la Arusha huko tulishatoka siku nyingi .
Sawa mlitoka zama za Azimio la Arusha siku nyingi na sasa mko zama za TOZO kila kona!! Do you think you will be better off with this stupid DpWorld contract? Ukidhani hivyo utakuwa kama hao wenzio wasio kuwa na ubongo!!
 
Sawa mlitoka zama za Azimio la Arusha siku nyingi na sasa mko zama za TOZO kila kona!! Do you think you will be better off with this stupid DpWorld contract? Ukidhani hivyo utakuwa kama hao wenzio wasio kuwa na ubongo!!
Tatizo unaendeshwa na hofu hofu ya kutokuelewa ,hapo hapo unalalamika tozo huwezi kujiendesha bila kodi usipotaka uwekezaji mkubwa wenye mageuzi basi jiandae kuendelewa kukamuliwa maana tozo ni kodi na ni our civic duty kuilipa kwa ajili ya maendeleo yetu.
 
Ninachojua WaTz ni maandazi... They know nothing, useless hopeless... Kilakitu kwao Alhamdulillah wakat watu wachache wanapiga maisha kupitia upumbav wao
 
Tatizo unaendeshwa na hofu hofu ya kutokuelewa ,hapo hapo unalalamika tozo huwezi kujiendesha bila kodi usipotaka uwekezaji mkubwa wenye mageuzi basi jiandae kuendelewa kukamuliwa maana tozo ni kodi na ni our civic duty kuilipa kwa ajili ya maendeleo yetu.
Unajua kitu kimoja ni kuwa tatizo kubwa la serikali hii sio makusanyo ya kodi bali ni matumizi mabaya ya hayo Mapato ndiyo yanasababisha kuongeza kodi mara ka mara !! Serikali yenye weledi haiwezi kutumia 62% ya baleti yake kwenye adminstration na kununua vitafunio vya wakubwa ofisini!! Kwa kufanya hivyo lazıma mtalazimika kuwakamua wananchi wenu kila mwaka. Kwa ujinga wenu mtahamisha kodi /tozo kutoka kwenye miamala ya Simu na kuipeleka kwenye cement!!

It is high time WaTanaganyika wakagoma kulipa kodi mpaka pale watapokoridhika kuwa kodi zao zinatumika kwa maendeleo Yao na sio kununua Ma V8 wakati mashule hayana madawati, hospitali hazina dawa na wananchi hawana maji safi na yaliyo salama!!

Sasa kati ya mimi na wewe nani hana uelewa; kwa kudhani kuuza bandari kwa mkataba wa kimangungo ndio suluhisho la Mapato ya nchi?
 
Viongozi wa Kiafrica mbele ya milungula huwa wanafanya mambo ya ajabu sana ,mwarabu kashampa shekeli anataka kutuingiza mkenge na kutuachiza zigo la "VIMA" tuangaike nayo.

Huo Mkataba ni wa kipuuzi sana sijui kwanini wanaubeba ,kama una faida mbona zanzibar bandari zao hawajapewa? Zanzibar hawataki kuongeza ufanisi/mapato/ajira?
 
Kwahiyo kwasababu ya umasikin wako unaweza kuruhusu tajiri aje ajenge gorofa hapo kwako alimiliki milele upewe visenti kidogo tu kisa na wewe uonekane uko kwenye gorofa. Hiv huu umasikin wa akili umetokea wapi nchi hii Mzee. Dunia yote inatembea katika mfumo wa win win situation wewe unamuachia mkeo tajiri kisa anawapa hela. Poor minded
Ujinga ni wewe kuendelea kungangania hicho kijumba chako chenye fremu mbili ukijiona unapata faida badala ya kuingia makubaliano na huyo tajiri ajenge ghorofa 16 hoteli na anakuachia ghorofa 4 uzipangishe upate fedha na akupe ghorofa moja ya makazi na katika hizo floor huyo tajiri anawekeza hoteli na watoto wako wanapata kazi humo humo na pia mnakubaliana baada ya miaka 20 ghorofa lote linarudi na kuwa mali yako na hapo hapo mke wako anapata kazi ya umeneja wa kusimamia hizo apartment zako wewe unazopangisha , na wewe ulichotoa ni eneo lako tu hayo mabadiliko yatokee ila sasa wewe mhemko hutaki unataka mgawane nusu kwa nusu yaani hutaki 25% kwa kuwa unaeneo na pia miaka 20 ikipita yeye akiondoka bado litakuwa mali yako lakini unaona unaibiwa yaani roho inakutoka kabisa bora tu ubakiwe na kijumba na fremu zako mbili ambayo moja mke wako aendelee kuuza sato hapo, ukiambiwa utumie akili husikiii.
 
Unajua kitu kimoja ni kuwa tatizo kubwa la serikali hii sio makusanyo ya kodi bali ni matumizi mabaya ya hayo Mapato ndiyo yanasababisha kuongeza kodi mara ka mara !! Serikali yenye weledi haiwezi kutumia 62% ya baleti yake kwenye adminstration na kununua vitafunio vya wakubwa ofisini!! Kwa kufanya hivyo lazıma mtalazimika kuwakamua wananchi wenu kila mwaka. Kwa ujinga wenu mtahamisha kodi /tozo kutoka kwenye miamala ya Simu na kuipeleka kwenye cement!!

It is high time WaTanaganyika wakagoma kulipa kodi mpaka pale watapokoridhika kuwa kodi zao zinatumika kwa maendeleo Yao na sio kununua Ma V8 wakati mashule hayana madawati, hospitali hazina dawa na wananchi hawana maji safi na yaliyo salama!!

Sasa kati ya mimi na wewe nani hana uelewa; kwa kudhani kuuza bandari kwa mkataba wa kimangungo ndio suluhisho la Mapato ya nchi?
Ukisema watanzania hawana maji swali la msingi hayo maji huwa wanapewa bure jibu hapana huwa wanayalipia kila mwezi kama wanayalipia kila mwezi kwa nini hawayapati maeneo yote je uwezo mdogo kumfikishia kila mtu basi kwa nini tusiwape watu binafsi hii biashara waanzishe kampuni zao za kusambaza maji na hizi za ummah ziwepo tu washindane kwenye kukamata soko la watumiaji, wasambaze maji kwa kuwa watumiaji wanalipia na soko lipo maana watu wengi wanayahitaji huko majumbani na mashambani , halafu tutoze kodi kampuni binafsi kutokana na huduma za kusambaza maji tuongeze pato letu ili tupunguziwe hizo tozo unazolalamika , ukiangalia mengi ya shida ya mtanzania za kila siku ni fursa za kibiashara lakini sera ndio hazikubali ndio maana tukiona kuna watu wanaleta mageuzi lazima kuwasupport
 
Hahaha we uniquote halafu unaomba nisikusemeshe usipaniki wewe acha kuquote tu sitakujibu
Ndio maana wenye mamlaka wameamua kutumia vizuri kabisa nafasi hii ya kuingia makubaliano ya uendeshaji wa bandari na magwiji wa tasnia show me your friend i can predict your future ,wewe kwa lugha zako na maoni yako ndio wale wale wapingaji saa nyingine unapinga kwa hofu tuu what if ,what if acha wenye clear mind wasio na hofu na wenye kujiamini wafanye mambo na tuondoe uwoga uwoga wa kuona tunaibiwa that how business is done. Wasipopatikana walipa kodi wakubwa basi tujue tutalipa sisi wadogo huhitaji kuwa nani au kuwa madigrii 7 kujua hilo.
Mtu yeyote mwenye akili timamu lazima awe na hofu. Kama unaweza muondolee hiyo unayoiita hofu kwa kujibu hoja na maswali yake ya msingi.
 
Mtu yeyote mwenye akili timamu lazima awe na hofu. Kama unaweza muondolee hiyo unayoiita hofu kwa kujibu hoja na maswali yake ya msingi.
hofu nyingine huwa zinaisha baada ya kuona matokeo hata umwambie nini aliezaliwa na mashaka na hofu atendelea tu na ndio maana kuna watu wao kuajiriwa tu ndio salama yao maana ukiwaambia biashara hawawezi hata kidogo shauri ya hofu , hofu ya kuibiwa kila saa kila dakika na watakuwa hivyo hivyo mfano mlimani city ile miaka hiyo makelele nchi imeuzwa leo si ile pale ipo hao waliowekeza wameondoka nayo kwani ajira ngapi zimepatikana na kampuni nyingi kubwa zipo pale kama tunahitaji kuwa kitovu cha shughuli za kibiashara Africa ni lazima tuwe na utengemano na magwiji wa kwenye masuala ya biashara.
 
Back
Top Bottom