tikatika
JF-Expert Member
- May 6, 2011
- 2,330
- 4,119
Kuna hoja inajirudia mara kwa mara toka pande mbili za wana CCM na wasio wana CCM juu ya JK na JPM. Hoja yenyewe na wale waliompinga JK hadi kufikia kumuita dhaifu na sasa wanaonekana wanamkubali.
Majibu naweza kuyajibu kwa mifano ifuatayo.
Kama ulizoea kula wali maharage, ugali maharage na siku moja ukapelekwa meza iliyojaa mboga saba na vitu tofauti tofauti walai utabeza chakula chako cha awali. Kwani umepata chakula bora kuliko cha awali. Lakini unaonaje badala ya chakula cha awali ukaja ukapewa ugali na chumvi,Mhogo mkavu, kwa vyovyote utasema bora wali maharage na ugali maharage kuliko ugali na chumvi. Lakini hitaji lako sio hivyo ni meza iliyojaa mboga saba na mapochopocho.
Haiwezekani ulikuwa unasafiri kwa kutumia bodaboda kwenda mkoani umechoka unatamani ubadilishe usafiri unapewa baiskeli badala ya kupewa vx, kwanini usiikumbuke bodaboda yako!?
Wote mnaopenda JPM na mnamponda JK hata mara ya kwanza tulipompinga JK hamkuwahi kumponda so sishangai saa hizi mkiwa mnamuunga mkono huyu hapa.
Tulipinga safari za nje mlizitetea, amekuja huyu na kuzifuta mnamnanga yule kwa kumsema alizoea sana kuruka. Mbona awali hamkumpinga?
Sina sababu ya kuelezea sababu zinazotufanya tumkumbuke JK na kumpinga huyu. Hasa hasa suala uhuru wa kuongea na kufanya siasa. Kwanini tusimwone JK anafaa?
Tulitegemea aje mwingine aweke uwazi na uhuru zaidi sasa huyu anazidi kutunyima uhuru wa kukosoa. Bunge hataki liwe live.
Kesi za ajabu ajabu zinafunguliwa ili kutisha wengine wasithubutu kukosoa. Kwanini tusimwone JK alikuwa afadhari?
Mifano hiyo hapo juu na sababu chache hizi hapa zinatufanya tumkumbuke JK.
Lakini ukweli tulihitaji mtu bora zaidi ya yule wa awali ila imekuwa kinyume. Je, mmetuelewa tunaomkumbuka JK?
Majibu naweza kuyajibu kwa mifano ifuatayo.
Kama ulizoea kula wali maharage, ugali maharage na siku moja ukapelekwa meza iliyojaa mboga saba na vitu tofauti tofauti walai utabeza chakula chako cha awali. Kwani umepata chakula bora kuliko cha awali. Lakini unaonaje badala ya chakula cha awali ukaja ukapewa ugali na chumvi,Mhogo mkavu, kwa vyovyote utasema bora wali maharage na ugali maharage kuliko ugali na chumvi. Lakini hitaji lako sio hivyo ni meza iliyojaa mboga saba na mapochopocho.
Haiwezekani ulikuwa unasafiri kwa kutumia bodaboda kwenda mkoani umechoka unatamani ubadilishe usafiri unapewa baiskeli badala ya kupewa vx, kwanini usiikumbuke bodaboda yako!?
Wote mnaopenda JPM na mnamponda JK hata mara ya kwanza tulipompinga JK hamkuwahi kumponda so sishangai saa hizi mkiwa mnamuunga mkono huyu hapa.
Tulipinga safari za nje mlizitetea, amekuja huyu na kuzifuta mnamnanga yule kwa kumsema alizoea sana kuruka. Mbona awali hamkumpinga?
Sina sababu ya kuelezea sababu zinazotufanya tumkumbuke JK na kumpinga huyu. Hasa hasa suala uhuru wa kuongea na kufanya siasa. Kwanini tusimwone JK anafaa?
Tulitegemea aje mwingine aweke uwazi na uhuru zaidi sasa huyu anazidi kutunyima uhuru wa kukosoa. Bunge hataki liwe live.
Kesi za ajabu ajabu zinafunguliwa ili kutisha wengine wasithubutu kukosoa. Kwanini tusimwone JK alikuwa afadhari?
Mifano hiyo hapo juu na sababu chache hizi hapa zinatufanya tumkumbuke JK.
Lakini ukweli tulihitaji mtu bora zaidi ya yule wa awali ila imekuwa kinyume. Je, mmetuelewa tunaomkumbuka JK?