Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,905
TULIANZA NA MILO MITATU, TUKAJA MILO MIWILI. SASA TUPO MLO MMOJA. NIMEITISHA KIKAO CHA DHARURA.
Anaandika, Robert Heriel
Sio kama nina Parkinson Disease Kwa jinsi ninavyotetemeka hapa. Hata nikikosea maandishi hapa msinitukane ndugu zanguni. Eleweni njaa haina mbabe. Nina ubao hapa siiiioo mcgezo.
Wengi humu wanajua ninaishi Kwa Shemeji yangu, aliyemuoa Dada yangu kipenzi, Naelijwa, labda mtajiuliza naanika mambo ya familia ya dadaangu Mtandaoni, lakini sina jinsi, hata hivyo dada na Shemeji hawatumii mitandao ya kijamii ingawaje rafiki zao wanaweza kuwa humu. Lakini Mimi sijali wala nini.
Kuhusu Ile kesi niliyompeleka Mahakamani, Taikon niliangukia Pua. Yule Hakimu ni mjinga Sana, tuachaneni na hayo.
Nilipofika hapa kwa Shemeji yangu kipindi kile nilikuta wanakula Milo mitatu. Tulikula Milo mitatu weee mpaka Taikon nikaota shavu. Mboga Saba zilinifanya ninawiri,
Kwa msiojua faida za Kula Milo mitatu na mboga Saba huku juisi embe na mapasheni zikiwa zimesheheni mezani, faida ni hizi;
i. Kunawiri na kuwa na mwili wenye Rutuba
ii. Ngozi kuwa laini
iii. Kuwa na nguvu za kiume
iv. Kuvutia Warembo
Hivyo miezi sita ilinitosha kuwa na mwili wa kushawishi Pisikali za Mjini. Ndipo nikampata huyu mchumba wangu ambaye wote tunakaa Kwa Shemeji.
Nataka nikuambie na wala usije kumuambia mtu, hii ni Siri yetu Mimi na Wewe, chakula kinaleta uzuri Kwa mtu.
Nakumbuka nilipokuja kutoka kijijini Kwetu huko Makanya, nilikuja nikiwa nimezeeka, nilikuwa Sura personal, nilikuwa nimefubaa kama baa za Wanywa mataputapu.
Hivi unajua Kwa nini sipendi uone picha zangu za zamani, ni Kwa sababu nilikuwa kama kioja, kituko kitakachokupa cheko.
Chakula ukila vizuri lazima uzuri uje tu.Hapa asubuhi tulikuwa tunaamkia maziwa na mayai, pamoja na matunda, Mchana tunapiga ugali, Samaki, mboga za majani, maharage, na kajuisi kabariidi. Jioni tunamalizia na chakula laini Kama ndizi au viazi, zilizochanganywa na Nyama au nyama choma na juisi laini.
Taikon Rutuba ikavuta huba, mademu wakaniganda kama Ruba. Nikajisahau kuwa nipo kwa Shemeji, sikukumbuka mambo ya kutafuta kazi mpaka siku nilipoona Mlo mmoja umeondolewa kwenye Ratiba. Mlo wa Asubuhi. Ikabaki Milo miwili. Sasa nikawa sielewi nini kinaendelea. Nikavunga, Tukaanza kupiga Hesabu za Pasi ndefu hapo tungekula chakula saa tano Asubuhi, alafu inapigwa Counterattack ndefu mpaka kumi na moja au kumi na mbili jioni. Hata hivyo Pasi hizo nilishajifunziaga Chuoni Kule Ujerumani kwenye Bundasiliga. Hivyo nikaona It's Okay.
Sijakaa kidogo nashangaa Shemeji amebadilisha mfumo kutoka Counterattack mpaka "One touch" kama mnakumbuka ule mchezo wa mpira WA miguu wa 'one touch' kugusa mara moja. Sasa nikaona application ya mchezo Ile kwenye Really Life.
One touch fomula ilianza Last week. Shemeji nakumbuka weeki mbili zilizopita alituuliza ni saa gani ni katikati ya siku Kwa upande wa mchana, nakumbuka nilitopoka saa sita mchana, aliponiuliza Kwa nini nikamjibu ni Kwa sababu jua lipo utosini. Katikati. Akanisifu Kwa jibu langu.
Sasa nashangaa wiki iliyoanza naamka Asubuhi hola, nahesabu masaa hola, mpaka saa tano ndio namuona Dada anaingia jikoni, anafanya vitu saa sita tukawa mezani, nakumbuka siku ya Kwanza tulikula kimyakimya bila kuongeleshana ungedhani tunakula chakula cha tambiko la mizimu. Sio Shemeji, sio Dada wala sio Mimi. Watoto wapo boarding.
Kesho yake, hivyohivyo, siku ya tatu nako hivyohivyo. Mpaka nikahisi wanataka kunitoa Kafara. Unajua Shemeji yangu ni mtu anayependa Sana kuongelea mambo ya waganga Sana. Sasa kuishi na watu wa namna hii unatakiwa uwe kimachale machale.
Jana nimewaweka kikao cha dharura, kujua Yale yanayoendelea mule ndani, nikamuambia Shemeji yangu imekuwaje tunakula Kama tupo kwenye Meza ya mizimu, pia mbona tunakula mlo mmoja. Shemeji akachukua simu yake akapiga Kwa Mama yake, kisha akaweka Loud;
" Marhàba mwanangu tunakufa njaa, leo hatujala kabisa. Nasubiria ahadi yako. Akiba ya chakula nilikuambia imeisha, mwaka huu mvua hazikunyesha vizuri hivyo hatukuvuna, wala nisingekusumbua mwanangu"
Ilikuwa sauti ya Mamaake na Shemeji yangu. Nilijikuta nipo kimya.
Habari nilizonazo hapa naambiwa Kwa sasa ukila Milo miwili hapo mtaani watu wanakupigia makofi kutokana na Hali kuwa ngumu. Na hao wanaofanya hivyo ni Wale wenye vipato vya Kati na vipato vikubwa.
Wale wenzangu na Taikon Mlo mmoja ukicheza unaweza kuukosa ukalala njaa.
Acha nipumzike,
Ni Yule mpiga One Touch
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam,
Anaandika, Robert Heriel
Sio kama nina Parkinson Disease Kwa jinsi ninavyotetemeka hapa. Hata nikikosea maandishi hapa msinitukane ndugu zanguni. Eleweni njaa haina mbabe. Nina ubao hapa siiiioo mcgezo.
Wengi humu wanajua ninaishi Kwa Shemeji yangu, aliyemuoa Dada yangu kipenzi, Naelijwa, labda mtajiuliza naanika mambo ya familia ya dadaangu Mtandaoni, lakini sina jinsi, hata hivyo dada na Shemeji hawatumii mitandao ya kijamii ingawaje rafiki zao wanaweza kuwa humu. Lakini Mimi sijali wala nini.
Kuhusu Ile kesi niliyompeleka Mahakamani, Taikon niliangukia Pua. Yule Hakimu ni mjinga Sana, tuachaneni na hayo.
Nilipofika hapa kwa Shemeji yangu kipindi kile nilikuta wanakula Milo mitatu. Tulikula Milo mitatu weee mpaka Taikon nikaota shavu. Mboga Saba zilinifanya ninawiri,
Kwa msiojua faida za Kula Milo mitatu na mboga Saba huku juisi embe na mapasheni zikiwa zimesheheni mezani, faida ni hizi;
i. Kunawiri na kuwa na mwili wenye Rutuba
ii. Ngozi kuwa laini
iii. Kuwa na nguvu za kiume
iv. Kuvutia Warembo
Hivyo miezi sita ilinitosha kuwa na mwili wa kushawishi Pisikali za Mjini. Ndipo nikampata huyu mchumba wangu ambaye wote tunakaa Kwa Shemeji.
Nataka nikuambie na wala usije kumuambia mtu, hii ni Siri yetu Mimi na Wewe, chakula kinaleta uzuri Kwa mtu.
Nakumbuka nilipokuja kutoka kijijini Kwetu huko Makanya, nilikuja nikiwa nimezeeka, nilikuwa Sura personal, nilikuwa nimefubaa kama baa za Wanywa mataputapu.
Hivi unajua Kwa nini sipendi uone picha zangu za zamani, ni Kwa sababu nilikuwa kama kioja, kituko kitakachokupa cheko.
Chakula ukila vizuri lazima uzuri uje tu.Hapa asubuhi tulikuwa tunaamkia maziwa na mayai, pamoja na matunda, Mchana tunapiga ugali, Samaki, mboga za majani, maharage, na kajuisi kabariidi. Jioni tunamalizia na chakula laini Kama ndizi au viazi, zilizochanganywa na Nyama au nyama choma na juisi laini.
Taikon Rutuba ikavuta huba, mademu wakaniganda kama Ruba. Nikajisahau kuwa nipo kwa Shemeji, sikukumbuka mambo ya kutafuta kazi mpaka siku nilipoona Mlo mmoja umeondolewa kwenye Ratiba. Mlo wa Asubuhi. Ikabaki Milo miwili. Sasa nikawa sielewi nini kinaendelea. Nikavunga, Tukaanza kupiga Hesabu za Pasi ndefu hapo tungekula chakula saa tano Asubuhi, alafu inapigwa Counterattack ndefu mpaka kumi na moja au kumi na mbili jioni. Hata hivyo Pasi hizo nilishajifunziaga Chuoni Kule Ujerumani kwenye Bundasiliga. Hivyo nikaona It's Okay.
Sijakaa kidogo nashangaa Shemeji amebadilisha mfumo kutoka Counterattack mpaka "One touch" kama mnakumbuka ule mchezo wa mpira WA miguu wa 'one touch' kugusa mara moja. Sasa nikaona application ya mchezo Ile kwenye Really Life.
One touch fomula ilianza Last week. Shemeji nakumbuka weeki mbili zilizopita alituuliza ni saa gani ni katikati ya siku Kwa upande wa mchana, nakumbuka nilitopoka saa sita mchana, aliponiuliza Kwa nini nikamjibu ni Kwa sababu jua lipo utosini. Katikati. Akanisifu Kwa jibu langu.
Sasa nashangaa wiki iliyoanza naamka Asubuhi hola, nahesabu masaa hola, mpaka saa tano ndio namuona Dada anaingia jikoni, anafanya vitu saa sita tukawa mezani, nakumbuka siku ya Kwanza tulikula kimyakimya bila kuongeleshana ungedhani tunakula chakula cha tambiko la mizimu. Sio Shemeji, sio Dada wala sio Mimi. Watoto wapo boarding.
Kesho yake, hivyohivyo, siku ya tatu nako hivyohivyo. Mpaka nikahisi wanataka kunitoa Kafara. Unajua Shemeji yangu ni mtu anayependa Sana kuongelea mambo ya waganga Sana. Sasa kuishi na watu wa namna hii unatakiwa uwe kimachale machale.
Jana nimewaweka kikao cha dharura, kujua Yale yanayoendelea mule ndani, nikamuambia Shemeji yangu imekuwaje tunakula Kama tupo kwenye Meza ya mizimu, pia mbona tunakula mlo mmoja. Shemeji akachukua simu yake akapiga Kwa Mama yake, kisha akaweka Loud;
" Marhàba mwanangu tunakufa njaa, leo hatujala kabisa. Nasubiria ahadi yako. Akiba ya chakula nilikuambia imeisha, mwaka huu mvua hazikunyesha vizuri hivyo hatukuvuna, wala nisingekusumbua mwanangu"
Ilikuwa sauti ya Mamaake na Shemeji yangu. Nilijikuta nipo kimya.
Habari nilizonazo hapa naambiwa Kwa sasa ukila Milo miwili hapo mtaani watu wanakupigia makofi kutokana na Hali kuwa ngumu. Na hao wanaofanya hivyo ni Wale wenye vipato vya Kati na vipato vikubwa.
Wale wenzangu na Taikon Mlo mmoja ukicheza unaweza kuukosa ukalala njaa.
Acha nipumzike,
Ni Yule mpiga One Touch
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam,