Jabali la Siasa
JF-Expert Member
- Jul 10, 2020
- 2,542
- 2,174
EPforR I ilitoa TZS 208b kwa JK mwaka FY2014|15 to 2020|21, why EPforR II imetoa TZS 196b kwa Rais Samia FY2021|22 mwaka mmoja baadaye,Je waligoma au hawakuwa na pesa?
==============
Katika kile kinachotajwa kama Kuimarika kwa diplomasia ya Uchumi na ukuaji wa demokrasi na Utawala wa sheria nchini Rais Samia Suluhu Hassan apokea msaada wa Tshs 196bl kutoka nchi ya Sweden ( SIDA ) kwaajili mradi wa Education Programme for Results phase two ( EPforR II),
FY2014|15 Rais Jakaya Mrisho Kikwete rais wa awamu ya nne alipokea Tshs 208bl toka hukohuko Sweden kwaajili ya mradi wa elimu wa Education Programme for Result Phase One (EPforR I) ambao ulikuwa ni mkataba wa miaka mitano mitano yaani FY2014|15 hadi FY2020|21,
Swali langu kwenu,kwanini Swedeni (Sida) hawakutupa pesa hizi FY2020|21 kama mkataba ulivyoonesha na badala yake wametupa Leo FY2021|22 yaani mwaka mmoja baadae? Je, nikweli sasa dunia imekubali mapigo ya Rais Samia Suluhu juu ya Ujenzi mpya wa diplomasia kimataifa na ongezeko la nafasi kwa Watanzania kwenye Uhuru wa kujieleza, Uhuru wa habari na vyombo vya habari,Utawala wa sheria pamoja na demokrasi?
Je,Vipi kuhusu hawa mabwana watatu yaani Yule bwana wa Singida,Yule bwana wa Arusha na Yule bwana wa Bukoba|Kagera unadhani wazungu kwa kumpa Rais Samia hizi Tshs 196bl wameamua kutuma ujumbe gani kwao baada ya wao kuwazuia mwaka jana? Je,tusubiri wafukuzwe kama mbwa au tuwashauri warudi nyumbani kwa hiari yao kwakuwa Tanzania ya Sasa ni salama zaidi na wahisani wametambua yakuwa Tanzania kwa sasa ni salama pengine kuliko wakati wowote wa uhai wake,
Kama hawa jamaa walishavunja mkataba kwa sababu walizozijua wao, Je bila diplomasia ya Rais Samia Tanzania ingepata hizi pesa leo? "Tunaposema hakuna kama Samia lazima mtuelewe pesa hii ya msaada inaweza kujenga madarasa elfu 10 mapya kwaajili ya watoto hawa wa masikini, Watanzania je hili ni jambo baya?"
#KAZI IENDELEE KWA KASI & WELEDI ZAIDI
VIVA SAMIA VIVA ||VIVA TANZANIA VIVA