Kwanini siku hizi vijana wadogo wana kiwango kikubwa cha stress na depression?

mdhalendo

JF-Expert Member
Dec 14, 2011
282
273
Wadau wa JF.
Leo ningependa tujadili kidogo hali ya afya ya akili inayoendelea kuwatafuna vijana wetu mitaani bila jamii kuangazia.

Leo ni hali ya kawaida kukuta kijana teenager anayesoma sekondari au chuo kikuu akilalamika kuwa na msongo mkubwa wa mawazo au kitaalamu inaitwa Sonona (depression). Hali hiyo imepelekea baadhi yao kujizuru hadi kufikia hatua ya kujaribu kujiua.

Swali la kujiuliza: Nini kimepelekea ongezeko kubwa la vijana wadogo kuwa na depression: Je, ni kukosa malezi mazuri?, kushindwa kufikia ndoto na malengo yao? Je, mitandao ya kijamii imesababisha wao kutamani maisha ya kifahari wanayoyaona kwenye 'status' za wenzao? Je, ni hali ngumu za kiuchumi kwenye familia zao? Je, ni changamoto za kimapenzi?

Leo ningetamani nipate maoni yako, nini kinachangia ongezeko kubwa la sonona kwa vijana tofauti na ilivyokuwa miaka 15 na kurudi nyuma iliyopita Karibu tujadiliane pamoja

.
depress.jpg
 
Utafiti unaonyesha tangu kutokea kwa mapinduzi ya mitandao ya kijamii.

Kiwango cha maradhi ya misongo ya mawazo na kujinyonga vimeongezeka maradufu.

Unajua kwanini?

Kila mwanadamu hasa vijana tuna kawaida ya kujiringanisha na wengine hasa hali za kimaisha. Tunasahau mitandaoni hasa huku kwetu africa tunitumia isivyofaa kama njia ya kujionyesha. Fikilia ww huenda hata kula yako ya leo ni shida. Mwingine anapost anakula bata kwenye maeneo ya gharama.

Unaanza kujiuliza hivi mimi nakosea wapi. Mbona nimesoma, najituma. Ukishaanza kuwa na maswali mengi yasiyo na majibu. Tatizo huanzia hapo.
 
Nyingi ya hypothesis ulizotaja sioni zikiwaandama sana kundi la vijana uliowataja... yaani wanafunzi!!

Kinyume chake, naona zina nafasi kubwa kwa vijana ambao tayari wameanza maisha... labda mtu kamaliza chuo na sasa yupo mtaani, au hata kaishia elimu ile ambayo kutokana na sababu moja au nyingine, haimwezeshi kwa muda huo kuendelea zaidi, na badala yake, anatakiwa kuanza maisha!

Sasa hebu turudi kwa vijana waliomaliza vyuo! Siku hizi nasikia mwamba ambae umetumia picha yake kama avatar yako amegoma kabisa kuajiri!

Kwamba, kuna Walimu na Madaktari kibao na watu wa fani zingine wame-graduate tangia 2015 lakini bado wapo tu mtaani!

Sasa hivi watu kama hao utashangaa wakiwa na depression hasa ukizingatia wengi wanatoka familia maskini?!

Najua wapo watakaosema kwanini wasijiajiri... yeyote atayesema hivyo ni stupid kwa sababu kwa maisha haya hakuna mwenye resources za kujiajiri halafu akaacha kujiajiri!

Haya turudi wale walio vyuoni! Wakati nipo Mwaka wa II chuo, alikuja chuo mshikaji mmoja ambae alikuwa ame-graduate chini ya mwaka mmoja tu uliopita!

Jamaa alikuja pale akiwa kama mwajiriwa wa NHIF, na alikuwa kanona kweli kweli! Akawa anatupatia story za washikaji zake wengine waliokuwa wameajiriwa hapa na pale! Ile kwetu sie ilitupa moyo sana na kuona kumbe hata sisi, it's a matter of time kabla hatujalamba ajira!

What about wanafunzi wa vyuoni hivi sasa?! Wale waliowatangulia ndo kwanza wanakutana nao mitaani wakiwa choka mbaya, huku wengine wakisukuma maisha kwa ku-bet!!!

Hivi utashangaa wanafunzi nao wakiwa katika hali ya kukosa utulivu kama tuliyokuwa nayo sie?! Yaani mshikaji na AA zake zote zile anaishia ku-bet?!!

Hao wanaondesha maisha kwa ku-bet sasa!!! Trust me, maisha yako hayawezi kutegemea kamali halafu usiwe na msongo wa mawazo!!
 
Wanawaza Vyura tu.. maji ya kuwafuga hao vyura hawana. Mbaya zaidi akili hazijakaa kujiongeza namna ya kupata hayo maji.. ila akili zinawaza zaidi jinsi ya kushuka vyura tu.
Vyura watamu bwana...hizo stress za kutafuta maji wacha tupambane nazo
 
> Mapenzi
> Ugumu Wa Maisha
Mapenzi is just a subset of ugumu wa maisha!!!

Mtu una mtoto wa mzuri, pesa ya matunzo hauna!! Kesho na kesho kutwa anakukimbia anaenda kwa wanaoweza kuhudumia, au hata kama hajakukimbia, kwake unakuwa second best kwa sababu huna hela!!!

Na kwenye mapenzi bora ukimbiwe moja kwa moja kuliko kuwa second best....

So, msingi hapo sio mapenzi bali mapenzi yanyohitaji huduma ambayo in turn yanahitaji kitu mavumba, sio mtu una elf 20 yako, unaamua uka-bet ili iongezeke kidogo ndipo ukahonge!!!
 
Back
Top Bottom