Bunchari
JF-Expert Member
- Aug 31, 2017
- 489
- 531
Habari wakuu,
Sio lengo langu kufundisha mamlaka husika namna ya utendaji wa majukumu yao wala kuelekeza nini cha kufanya lakini mimi pia sio mwanasiasa, mahusiano yangu na serikali yapo upande wa ulipaji kodi pekee nawapa chao nabaki na changu.
Mapema leo nimeona nami nitoe maoni yangu kuhusu kinachoendelea katika medani za kisiasa na serikali kwa ujumla, kwanini muda mwingi mnamzungumzia JPM tatizo nini? Kwanini msitumie huo muda na nguvu kumpa ushirikiano aliepo madarakani ili kuua mijadala ya kulinganisha uongozi kwamba huyu mbaya huyu mzuri.
Najua JPM alikuwa mtu mbaya kwa makundi fulani ya watu na mkombozi kwa baadhi,nimejaribu kufanya utafiti ninyi watumishi wa umma mnapenda majungu ndio mmekua chanzo cha hizi kelele za kulinganishana,sote tunajua jamaa aliziba mianya ya pesa za chap chap kwaupande mwingine net amount due hazipo vizuri lazima jamaa angeonekana mbaya tu...Wacha jamaa apumzike kibaya kwako kizuri kwa wengine na kizuri kwako kibaya kwa wengine.
Viva Tanzania mama anaupiga mwingi nchi inasonga,vituo vya afya kila mahali.
Sio lengo langu kufundisha mamlaka husika namna ya utendaji wa majukumu yao wala kuelekeza nini cha kufanya lakini mimi pia sio mwanasiasa, mahusiano yangu na serikali yapo upande wa ulipaji kodi pekee nawapa chao nabaki na changu.
Mapema leo nimeona nami nitoe maoni yangu kuhusu kinachoendelea katika medani za kisiasa na serikali kwa ujumla, kwanini muda mwingi mnamzungumzia JPM tatizo nini? Kwanini msitumie huo muda na nguvu kumpa ushirikiano aliepo madarakani ili kuua mijadala ya kulinganisha uongozi kwamba huyu mbaya huyu mzuri.
Najua JPM alikuwa mtu mbaya kwa makundi fulani ya watu na mkombozi kwa baadhi,nimejaribu kufanya utafiti ninyi watumishi wa umma mnapenda majungu ndio mmekua chanzo cha hizi kelele za kulinganishana,sote tunajua jamaa aliziba mianya ya pesa za chap chap kwaupande mwingine net amount due hazipo vizuri lazima jamaa angeonekana mbaya tu...Wacha jamaa apumzike kibaya kwako kizuri kwa wengine na kizuri kwako kibaya kwa wengine.
Viva Tanzania mama anaupiga mwingi nchi inasonga,vituo vya afya kila mahali.