Kwanini Serikali inawajengea nyumba walimu?

Kwanini Serikali inawajengea nyumba walimu?

Barbarosa

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
22,584
Reaction score
27,838
Nimekuwa sielewi ni kwanini Serikali yetu inatumia fedha nyingi sana kuwajengea walimu nyumba za kuishi? Ni kwanini hiyo fedha tunayotumia kujenga nyumba za walimu tusiziwekeze kwenye kuboresha Shule zetu kwa kuwanunulia Wanafunzi vitabu au hata kuwapa watoto chakula cha mchana badala ya kuwajengea Walimu nyumba?

Nasema hivi kwa maana sielewi mantiki ya kuwajengea walimu nyumba wakati wao ni waajiriwa kama waajiriwa wengine wote na wanalipwa mshahara sasa ni kwa nini jukumu la wao wataishi wapi liwe la Serikali na siyo lao walimu wenyewe?
Mbona wafanyakazi wengine wa Serikali wanajitegemea kwenye malazi?

Ni kwanini Serikali isijitoe kwenye hili na kuwaacha walimu wapange nyumba au wajenge wenyewe kwa kuchukua mkopo kama wakipenda?


Kwa Hesabu tu ya kawaida haiwezekani kwa Serikali kuweza kuwajengea Walimu wote nyumba huku ni kujidanganya na kupoteza fedha ambazo zingeweza kutumika kuwahudumia wanafunzi ambao hawana mahitaji muhimu na isitoshe wanafunzi wengi wanatoka nyumba ambazo wazazi wao hata chanzo cha kipato hawana sasa ni kwa nini Serikali iwahudumie walimu ambao wana wanalipwa mshahara?
 
We Unakichaa, Umejiuliza Kwanini Waalimu Hawalipwi POSHO WALA NIGHT NA WAFANYAKAZI WENGINE WANALIPWA WAKATI KAZI WANAZOZIFANYA HADI KULIPWA POSHO WANALIPWA MSHAHARA? Kwanini Hizo Posho Zisiende Kwenye Ujenzi Wa Barabara Vijijini?

Umewahi Kujiuliza Mwalimu Wa Digrii Anapoanza Kazi Analipwa Laki Sita Na Daktari Anaeanza Kazi Mwenye Digrii Hy Hy Analipwa Milioni Moja Na Laki Tano? Kwanini Na Wao Walipwe Pesa Zote Hz?

Kwanini Wasilipwe Viwango Sawa Na Waalimu?

FICHA UJINGA WAKO.
 
Sijaipata mantiki ya hoja yako!..Kwani hizo ni nyumba za walimu au ni za serikali kwa ajili ya walimu?

Mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila Mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na Serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa Mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa Serikali asijitegmee kwenye makazi?
Yaani Mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la Serikali bali liwe tatizo binafsi la Mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!
 
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila Mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na Serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa Mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa Serikali asijitegmee kwenye makazi?
Yaani Mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la Serikali bali liwe tatizo binafsi la Mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!

JIBU NIMESHAKUPA MBONA HUJAJIBU? NIMEKUULIZA Kwanini Wafanyakazi Wengne Wanalipwa Posho Na Waalimu Hawalipwi Posho? Kwanini Wafanyakazi Wengine Wanalipwa Mishahara Mizito Inayowawezesha Kujenga Nyumba Bora Kwa Kipindi Kifupi Wakati Mwalimu Analipwa Mshahara Mdogo? MBONA HUJIBU?
 
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila Mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na Serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa Mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa Serikali asijitegmee kwenye makazi?
Yaani Mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la Serikali bali liwe tatizo binafsi la Mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!
Kwani shule zote ziko mijini ambako kuna nyumba za kupanga? shule iliyoko kijijini kwenu ambako mnakunya porini kama wanyama wasipelekwe walimu? au unataka walimu wakaishi kwenye tembe la babu yako alilolijaza mahirizi na ngozi za alubino?
 
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila Mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na Serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa Mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa Serikali asijitegmee kwenye makazi?
Yaani Mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la Serikali bali liwe tatizo binafsi la Mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!

Nadhani wewe huyajui vizuri mazingira ya nchi hii, unadhani kila sehemu kuna nyumba za kupanga? Halafu huyo mwl atakuwa akijenga kila anapohamia? Watumishi wengine hao uliowataja wanayo house allowance ambayo mwl hana.
 
jamani kazi ya walimu ni ngumu sana achilia mbali kufundisha ,kuna kupitia madaftali ya wanafuzi wote
assume mwalimu ana wanafunzi 45ktk darasa moja
ana madarasa matatu anayofundisha 3*45=
ana vpindi labda vitatu kila darasa kwa wiki 3*3*45-=
kila siku anahitaji posho au overtime
 
We Unakichaa, Umejiuliza Kwanini Waalimu Hawalipwi POSHO WALA NIGHT NA WAFANYAKAZI WENGINE WANALIPWA WAKATI KAZI WANAZOZIFANYA HADI KULIPWA POSHO WANALIPWA MSHAHARA? Kwanini Hizo Posho Zisiende Kwenye Ujenzi Wa Barabara Vijijini? Umewahi Kujiuliza Mwalimu Wa Digrii Anapoanza Kazi Analipwa Laki Sita Na Daktari Anaeanza Kazi Mwenye Digrii Hy Hy Analipwa Milioni Moja Na Laki Tano? Kwanini Na Wao Walipwe Pesa Zote Hz?Kwanini Wasilipwe Viwango Sawa Na Waalimu? FICHA UJINGA WAKO.

Ok... Na kwa nini wanajeshi wananunua vitu kwa bei rahisi wakati nao wanalipwa mshahara kama wengine..?? Na kwa nini wawe na maduka yao makambini..??

Swali litabaki kuwa la kijinga kama tu halitaulizwa..
 
jamani kazi ya walimu ni ngumu sana achilia mbali kufundisha ,kuna kupitia madaftali ya wanafuzi wote
assume mwalimu ana wanafunzi 45ktk darasa moja
ana madarasa matatu anayofundisha 3*45=
ana vpindi labda vitatu kila darasa kwa wiki 3*3*45-=
kila siku anahitaji posho au overtime

Unaweza ukanitajia kazi rahisi..??
 
Shida kuna watu toka wazaliwe hawajui shida humu. Nafikiri mtoa mada hajui vizuri mazingira halisi ya mwalimu. Toka azaliwe "baba mkurugenzi wa madini kanda ya……….., mama barozi wa tanzania………. "Mtu kama huyu hawezi jua shida inayompata mwalimu wa kitanzania anayefundisha Kantalampa, namanyele, Tanganyika masgati, kibungo juu, na lindi vijijini.
Unapokosa la kuongea jf tulia comment za wenzako f.ala we.
 
jibu nimeshakupa mbona hujajibu? Nimekuuliza kwanini wafanyakazi wengne wanalipwa posho na waalimu hawalipwi posho? Kwanini wafanyakazi wengine wanalipwa mishahara mizito inayowawezesha kujenga nyumba bora kwa kipindi kifupi wakati mwalimu analipwa mshahara mdogo? Mbona hujibu?

akukibu nini mkuu wakati amekurupuka?wale wale hajui aliko toka.
 
Kwani shule zote ziko mijini ambako kuna nyumba za kupanga? shule iliyoko kijijini kwenu ambako mnakunya porini kama wanyama wasipelekwe walimu? au unataka walimu wakaishi kwenye tembe la babu yako alilolijaza mahirizi na ngozi za alubino?
How you present your strong opinion.. destroys maana nzima iliyobeba ujumbe wako...
 
Wala asiwasumbue huyo ana nguvu ya ziada ya viloba na vimemlevya kisawasawa hadi amesahau alikotoka na anakokwenda!
 
Mantiki ya hoja yangu ni kwamba ni kwa nini serikali inapoteza fedha kufanya jambo ambalo kiuhalisia haliwezekani? Yaani kumjengea kila Mwalimu nyumba ya kuishi hizi ni ndoto na Serikali haina huo uwezo hivyo ni kwanini kwa kuwa Mwalimu analipwa mshahara kama mwajiriwa mwingine yoyote yule wa Serikali asijitegmee kwenye makazi?
Yaani Mwalimu ataishi wapi isiwe tatizo la Serikali bali liwe tatizo binafsi la Mwalimu mwenyewe kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine kama manesi, na wengineo ambao wanalipwa mishahara na kupanga chumba!
Kwa sababu mishahara yao ni midogo na ujenzi wa nyumba unaondoa gharama za kila mwaka kwa serikali kulipa mishahara mikubwa kwenye bajeti yake. Chukulia hili kwa nini balozi wetu wananunua nyumba nchi za nje wakati wangeweza kupanga!

Hivyo badala ya kumlipa mwalimu tuseme milioni 3 kila mwezi ili kumwezesha kupanga nyumba ya Milioni 1.5, serikali itatumia milioni 1.5 kumlipa mwalimu kila mwezi kwa miaka yote wakati bado ikihodhi nyumba hiyo. Ni mpango mzuri sana kwa kuzingatia mpango wa muda mrefu ila kiukweli mishahara wanayopewa walimu na Madaktari bado haitazami market value ya pango ili kukidhi matumizi ya kawaida. Walimu na Madaktari bado wanapewa mshahara mdogo sana pamoja na kwamba hukaa nyumba za serikali wakati wabunge mawaziri na watumishi wengine wa umma wanapokea mishahara inayopitiza hata gharama za nyumba na usafiri ukijumlisha.
 
jamaa msimpuuze ana logic kama hamjui kada mbalimbali serikalini. mfano afisa anayeanza kazi kwenye halmashauru yoyote ambaye degree yake ni miaka 3 basi mshahara wake ni sawa na mwalimu mwenye degree na hana allowance zozote maana alowance ni mpaka ngazi ya kaimu mkurugenzi ndio unakuwa na sifa sasa kwa nini mazingira haya mwalimu apewe wafanyakazi wengine wasipewe?
 
jamani kazi ya walimu ni ngumu sana achilia mbali kufundisha ,kuna kupitia madaftali ya wanafuzi wote
assume mwalimu ana wanafunzi 45ktk darasa moja
ana madarasa matatu anayofundisha 3*45=
ana vpindi labda vitatu kila darasa kwa wiki 3*3*45-=
kila siku anahitaji posho au overtime
 
Barbarosa

Hujui mengi sana ndugu na unaonekana hujawahi Fanya kazi serikali ni tambua kuwa hata mawaziri wako wanaolipwa vizuri wamejengewa nyumba na serikali yaani kota za mawaziri kule msasani then watumishi wengine mfano mdogo askari wanalipwa Pesa za kodi ya nyumba hata kama watakuwa wanaishi kwenye nyumba zao mfano baba yangu mm anaishi kwenye nyumba yake ila Pesa anayolipwa tu ya nyumba ni zaidi za mshahara Wangu hapo unasemaje? Walimu nchi hii wanaonewa sawa mfano MWL anayeanza kazi ngazi ya Cheri mshahara wake haufiki 380,000/= na akiupata huo hakuna tenaa atakachokipata hadi mwezi mwingine sasa jiulize kwa mshahara huo hata akikopa Pesa bank wala hawezi kudhidi million 3
 
Last edited by a moderator:
Kwa sababu mishahara yao ni midogo na ujenzi wa nyumba unaondoa gharama za kila mwaka kwa serikali kulipa mishahara mikubwa kwenye bajeti yake. Chukulia hili kwa nini balozi wetu wananunua nyumba nchi za nje wakati wangeweza kupanga!

Hivyo badala ya kumlipa mwalimu tuseme milioni 3 kila mwezi ili kumwezesha kupanga nyumba ya Milioni 1.5, serikali itatumia milioni 1.5 kumlipa mwalimu kila mwezi kwa miaka yote wakati bado ikihodhi nyumba hiyo. Ni mpango mzuri sana kwa kuzingatia mpango wa muda mrefu ila kiukweli mishahara wanayopewa walimu na Madaktari bado haitazami market value ya pango ili kukidhi matumizi ya kawaida. Walimu na Madaktari bado wanapewa mshahara mdogo sana pamoja na kwamba hukaa nyumba za serikali wakati wabunge mawaziri na watumishi wengine wa umma wanapokea mishahara inayopitiza hata gharama za nyumba na usafiri ukijumlisha.


Lakini ni jambo ambalo haliwezekani kumjengea kila Mwalimu wa nchi nyumba ya kuishi Serikali haiwezi kufanya hilo wataongea tu kila siku lakini Kiuchumi hilo haliwezekani, chukulia tu kwa mfano kwa sasa hivi Tanzania kuna mwalimu mmoja kwa kila watoto 100 kwa hali ya kawaida inapaswa kuwa mwalimu mmoja kwa watoto 40 sasa kama kila mwalimu tutakayeongeza huko mbele ya safari ni lazima ajengewe nyumba hiyo fedha itatoka wapi? hapo hapo tunahitaji watoto wetu wale chakula cha mchana shuleni, wanahitaji madaftari, vitabu, na madawati na vitu vingine muhimu kwao sasa hiyo fedha itatoka wapi?

Na usisahau kuwa siku zote bajeti za Elimu hupangwa kiasi ambacho Serikali husika hutumia kwa kila mtoto wa shule na SIYO Mwalimu, kwa kawaida Mwalimu ni mwajiriwa na anapaswa ajitegemee na ataishi wapi haipaswi kuwa kazi ya Serikali, Serikali inapaswa imlipe fedha za kumtosha kuishi ( Na hii ni kwa Waajiriwa wote na sio walimu tu) ili ajitegemee sasa kujenga nyumba ni kuongeza gharama kwa maan ni lazima pia serikali hiyo hiyo ilipe umeme luku kwenye hizo nyumba, ilipe maji, ikarabati zikiharibika n.k sasa hiyo fedha ni kwa nini tusiwekeze kwa watoto wa shule?

Lakini kusema kwamba kila Mwalimu ajengewe nyumba ya kuishi siyo ukweli na hilo haliwezekani, kama Serikali imeshindwa kuwajengea nyumba Viongozi wakubwa ambao ni wachache itawezaje kuwajengea kila mwalimu hapa nchini?
 
Back
Top Bottom