Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,818
- 62,032
Ndugu zangu
Kwa mujibu wa uchunguzi na utafiti ulioendeshwa na wataalamu wetu profesa Mruma na Profesa Osoro ilibainika wazi kabisa kuwa Watanzania tulikuwa tukiibiwa na kampuni ya ACACIA katika madini yetu hususan kupitia mchanga wa makinikia.
Kwa mujibu wa Utafiti huo ilibainishwa kuwa pamoja na dhahabu walizokuwa wakikomba, walikuwa wakikombana madini mengineyo kama vile copper, chuma, cobalt na mengineyo yenye thamani.
Uchunguzi ulionyesha kuwa kwa muda mzima walio-operate nchini, ACACIA wametuibia takriban dola bilion 190 ambazo ni takriban sawa na shilingi Trilion 424.
Hizi ni pesa nyingi, nyingi, nyingi mno. Cha kushangaza ni kwamba serikali hii iliyounda tume na kubaini haya IMESAMEHE HIZI PESA!
Mtu unajiuliza kama siyo Uhujumu Uchumi hii ni kitu gani?
Tulichoambulia eti ni kupewa asilimia 16 ya hisa kwenye madini yetu wenyewe huku Mabeberu yakiendelea kukomba asilimia 84 na kutuachia vijisenti vya Dola milion 300 ambayo haifiki hata TRLION moja, Yaani Tumesamehe Trilion 424 ili Tupewe vihela ambavyo havifiki hata TRILION 1, Tumerogwa?
Katika vitu ambavyo serikali inayokuja inapaswa kufanya baada ya awamu hii kutoka madarakani ni kuwachukulia hatua wale wote waliosamehe hizi Trilion 424.
Mimi najiuliza, Bajeti yetu ya kila mwaka haifiki Trilion 40, Halafu leo hii unasamehe Trilion 424 ambayo ni bajeti ya nchi ya miaka 10 na tena hapo bila kutembeza bakuli kwa wahisani!
Serikali itupe majibu, Isijifanye kuweka Ukimya ili kutusahaulisha
KWA NINI IMUACHIE MWIZI ASEPE NA TRILION ZETU 424?
Kwa mujibu wa uchunguzi na utafiti ulioendeshwa na wataalamu wetu profesa Mruma na Profesa Osoro ilibainika wazi kabisa kuwa Watanzania tulikuwa tukiibiwa na kampuni ya ACACIA katika madini yetu hususan kupitia mchanga wa makinikia.
Kwa mujibu wa Utafiti huo ilibainishwa kuwa pamoja na dhahabu walizokuwa wakikomba, walikuwa wakikombana madini mengineyo kama vile copper, chuma, cobalt na mengineyo yenye thamani.
Uchunguzi ulionyesha kuwa kwa muda mzima walio-operate nchini, ACACIA wametuibia takriban dola bilion 190 ambazo ni takriban sawa na shilingi Trilion 424.
Hizi ni pesa nyingi, nyingi, nyingi mno. Cha kushangaza ni kwamba serikali hii iliyounda tume na kubaini haya IMESAMEHE HIZI PESA!
Mtu unajiuliza kama siyo Uhujumu Uchumi hii ni kitu gani?
Tulichoambulia eti ni kupewa asilimia 16 ya hisa kwenye madini yetu wenyewe huku Mabeberu yakiendelea kukomba asilimia 84 na kutuachia vijisenti vya Dola milion 300 ambayo haifiki hata TRLION moja, Yaani Tumesamehe Trilion 424 ili Tupewe vihela ambavyo havifiki hata TRILION 1, Tumerogwa?
Katika vitu ambavyo serikali inayokuja inapaswa kufanya baada ya awamu hii kutoka madarakani ni kuwachukulia hatua wale wote waliosamehe hizi Trilion 424.
Mimi najiuliza, Bajeti yetu ya kila mwaka haifiki Trilion 40, Halafu leo hii unasamehe Trilion 424 ambayo ni bajeti ya nchi ya miaka 10 na tena hapo bila kutembeza bakuli kwa wahisani!
Serikali itupe majibu, Isijifanye kuweka Ukimya ili kutusahaulisha
KWA NINI IMUACHIE MWIZI ASEPE NA TRILION ZETU 424?