Kwanini Serikali ilituficha kuugua kwa Dkt. Magufuli?

Siishi Tz lakini nilipata taarifa za kifo chake Mzena Hospital tarehe 9 na aliyenipa taarifa pia yuko ughaibuni nchi tofauti na ninayoishi mimi, walijaribu kuficha lakini zilivuja japo at that point in time sikuziamini.
Ni kweli mkuu. Hata mimi nilipata taarifa kabla ila nikawa siamini. Hili jambo watu wote waelewa wanajua undani wake. Waliobaki kudanganyika ni wale wafuata mkumbo wasiojua mbele yao futi mbili kuna nini.
 
The 180° shift of every single policy change(good or bad) after his death only leads me to one conclusion ,he was "Epsteined" and not in a suicide sense

But on another note some part in me tells me he died suddenly + a close circle of people knew and the shock of it confused them on what to tell the public
Wanasema marais sita wapinga chanjo wamefanyiziwa na wazungu wenye dunia yao.

Mwanzoni walisema ni mkwere ndio mastermind lakini siku zilivyozidi kusogea waliofanya unyama ni watu wenye mamlaka nzito.
 
Hana jibu,hata yeye hakujua kama Magufuli anaumwa, ilikuwa SIRI KUU,watu wachache SANA ndiyo waliokuwa wanajua kama mzee anaumwa.
Kumuuliza Hilo swali huyo Vasco da Gama wa kike ni kumuonea.
Nyie jamaa vilaza sana, nyinyi si ndiyo mlikuwa mnamsema Magufuli hasafiri sababu mshamba, hajui kiingereza and mara anaogopa ndege? Leo hii huyu kaanza kusafiri ashakuwa Vasco da gama wa kike!! Jinga kweli wewe jamaa
 
Unatii sheria bila shuruti huko ulipo ukija huku unasema TZ haina serikali. Kwani hizi Tozo na kodi za luku wewe unazilipa kwa serikali ipi?
Tozo na kodi za luku ni hela ambayo naporwa na magaidi ambayo hayana kibali cha wananchi.Samia jana amekiri kuwa katika uchaguzi wa 2020 walitumia mbinu ya kujifanya kuwa upinzani wanakosea kujaza form ili wao CCM wapite.
 
Wanadai huyo mama mwenyewe hakuwa na uhakika wa maisha yake ndani ya siku zile chache.

Tumshukuru Mabeho na wasaidizi wake kwa kuweza kuiongoza nchi bila ya kuwa mbele ya macho ya watu.
 
Kifo cha ghafla hakuna uhusiano na taarifa za kuugua.

Huwezi kusema mtu kafa ghafla halafu utoe taarifa za kuugua.

Itoshe SSH alisema mzee alizidiwa ghafla na kufa ghafla kutokana na heart electric shock.

Ni kama Michael Jackson Cardiac arrest ilimuondoa ghafla,Sasa hapa huwezi tena kuhoji sickness proceedings. The same Mkapa,Sokoine, na Mchopa.
 
Kama sikosei, mpaka sasa Rais Samia keshaongea na waandishi wa habari kama mara mbili hivi.

Ni zaidi ya mwezi sasa tokea alipoongea na wahariri wa vyombo vya habari/ waandishi wa habari toka ikulu ya Dar es Salaam.

Wiki moja au mbili zilizopita, akafanya mahojiano na Salim Kikeke wa BBC.

Katika nyakati zote hizo mbili, sikusikia kabisa akiulizwa ni kwa nini serikali yake ilituficha kuhusu kuugua kwa Rais Magufuli.

Wananchi hatukupata taarifa zozote zile zilizo rasmi hadi tukaishia kutegemea habari umbea na zisizo rasmi kupitia mitandao ya kijamii.

Kimya kilipozidi kutanda, tukaanza kudokezwa dokezwa kuwa hali si nzuri, mara sijui yupo anachapa kazi, mara sijui anafanywa nini…

Haikupendeza hata kidogo. Na hata vyombo vya habari vya kimataifa viliripoti kuhusu tetesi za kutoonekana kwa Magufuli.

Kwangu hili halikubaliki kabisa!

Wananchi kama waajiri wa hawa viongozi wetu, tuna haki ya kujua kuhusu afya za viongozi wetu.

Hapa simaanishi kila kitu kuhusu afya. Namaanisha tu ile kwa ujumla wake.

Kama mtu anaumwa, kalazwa, tuna haki ya kujua.

Mambo ya kuficha/ kufichwa halafu mnakuja tu kuambiwa mtu kaaga dunia, hayafai.
Hivyo, ningependa sana kujua kwa nini wananchi hatukupewa taarifa.

Na itokeapo fursa ingine ya Rais Samia au hata waziri mkuu Majaliwa kuongea na waandishi wa habari, ningependa kuona na kusikia wakiulizwa ni kwa nini hawakutufahamisha kilichokuwa kinaendelea.

Pascal Mayalla take note and spread the word.
Move on
 
Kama sikosei, mpaka sasa Rais Samia keshaongea na waandishi wa habari kama mara mbili hivi.

Ni zaidi ya mwezi sasa tokea alipoongea na wahariri wa vyombo vya habari/ waandishi wa habari toka ikulu ya Dar es Salaam.

Wiki moja au mbili zilizopita, akafanya mahojiano na Salim Kikeke wa BBC.

Katika nyakati zote hizo mbili, sikusikia kabisa akiulizwa ni kwa nini serikali yake ilituficha kuhusu kuugua kwa Rais Magufuli.

Wananchi hatukupata taarifa zozote zile zilizo rasmi hadi tukaishia kutegemea habari umbea na zisizo rasmi kupitia mitandao ya kijamii.

Kimya kilipozidi kutanda, tukaanza kudokezwa dokezwa kuwa hali si nzuri, mara sijui yupo anachapa kazi, mara sijui anafanywa nini…

Haikupendeza hata kidogo. Na hata vyombo vya habari vya kimataifa viliripoti kuhusu tetesi za kutoonekana kwa Magufuli.

Kwangu hili halikubaliki kabisa!

Wananchi kama waajiri wa hawa viongozi wetu, tuna haki ya kujua kuhusu afya za viongozi wetu.

Hapa simaanishi kila kitu kuhusu afya. Namaanisha tu ile kwa ujumla wake.

Kama mtu anaumwa, kalazwa, tuna haki ya kujua.

Mambo ya kuficha/ kufichwa halafu mnakuja tu kuambiwa mtu kaaga dunia, hayafai.
Hivyo, ningependa sana kujua kwa nini wananchi hatukupewa taarifa.

Na itokeapo fursa ingine ya Rais Samia au hata waziri mkuu Majaliwa kuongea na waandishi wa habari, ningependa kuona na kusikia wakiulizwa ni kwa nini hawakutufahamisha kilichokuwa kinaendelea.

Pascal Mayalla take note and spread the word.
Sukuma gang bado haiamini kilichotokea,mzee baba ndo hivyo tena hayupo tena na haitatokea tena msukuma kupewa hii nchi maana imedhihirika kua HAMFAI KUPEWA DOLA!
 
Nchi imepoa sana
Imepoa sana, siku hizi hata uzinduzi hamna tena kama zamani.
Halafu ngosha kila siku alikua anatuaminisha kua tupo vitani, halafu anatusisitiza kua vita ya kiuchumi ni mbaya kwerikweri.
Mi nataka kujua hii vita tulishinda, tulishindwa au bado tuko fonti raini kwenye mapambo?
 
Wananchi wangeambiwa ukweli wa kuugua kwake wangeweza kumuombea kwa Mungu kwa uzito yamkini kwa rehema za Mwenyezi Mungu angepona labda!

Sijui Kwanini walificha!

Pamoja na tetesi kuzagaa lakini bado wakakanusha kuwa jamaa ni mzima anapiga kazi kama kawaida.
Kama Mungu angeona umuhimu wa Maugufuli kuendelea kuwepo asingesubiri maombi ya wananchi
 
Kwa mujibu wa katiba ya URT,kifungu na ibara sikumbuki wataalamu wa katiba waje hapa kusaidia,endapo raisi wa nchi hii ataugua na atakuwa Yu mahututi hajitambui kwa kipindi cha wiki mbili,inabidi makamu wa raisi aapishwe kuwa raisi, kutoka na maelezo hayo ndiyo sababu inayopelekea taarifa za kuugua kiongozi mkuu zisiwe wazi,ili angalau kukwepa hicho kifungu na kusubiri kudra za mwenyezi,mgonjwa aweze kupona.
Hili ndio jibu hebu fikiria mtu azinduke akute akute mama wa watu kakakalia kiti chake ingekuwa vita kuu ya nne
 
Tozo na kodi za luku ni hela ambayo naporwa na magaidi ambayo hayana kibali cha wananchi.Samia jana amekiri kuwa katika uchaguzi wa 2020 walitumia mbinu ya kujifanya kuwa upinzani wanakosea kujaza form ili wao CCM wapite.
Unaporwa na nani na umesema serikali hakuna? hapo ulipo unatii sheria bila shuruti za serikali isiyokuwepo? Maana upo huru, ina maana wewe ni mtiifu na mwoga wa kuvunja sheria.
 
Naporwa na majambazi wa uchaguzi.
hapo ulipo unatii sheria bila shuruti za serikali isiyokuwepo? Maana upo huru, ina maana wewe ni mtiifu kwa majambazi wa uchaguzi na mwoga wa kuvunja sheria zao hivyo huna madhara, endelea kutii sheria bila shuruti za hao majambazi ambao ndio serikali yako.

Usisahau kujiachia unyang'anywe zile tozo kama tu mwanamwali asemaye mdomoni sina mume ilihali ameolewa na analala kitandani kwa mumewe.
 
hapo ulipo unatii sheria bila shuruti za serikali isiyokuwepo? Maana upo huru, ina maana wewe ni mtiifu kwa majambazi wa uchaguzi na mwoga wa kuvunja sheria zao.
Definition ya Serikali ni group la watu waliochaguliwa na watu kwa ajili ya kutetea maslahi ya watu hao.(Government of the people, by the people, for the people)

Sasa hiki kikundi cha majambazi kinachoongoza watu hapa Tanzania kimekosa sifa zote kuu mbili:

1.Hiki kikundi cha ugaidi hakijatokana na watu.Hakina kibali cha wananchi.

2.Hakitetei maslahi ya wananchi.

Kwa sababu kikundi hiki cha ugaidi kimekosa sifa kuu mbili za kuitwa Serikali hakiwezi kuitwa ni Serikali.
 
Back
Top Bottom