Kwanini saba iwe moja kwenye masaa?

Ambe sokoro waito[emoji38]
 
Ambe sokoro waito[emoji38]
Kuhusu hii elimu yako ni ndogo kwanini ujiulizi ni kwanini kila mwaka majira yanajirudiarudia kmfano kila mwezi 4.masika mwezi 7kiangazi wa9 vuli nk. Fanya utafiti lete majibu ya utafiti wako hapa acha kulialia. Kuyajua haya kuna gharama.
 

Kabla ya huyo mtunga kalenda ulikuwa unahesabu vipi masaa?
 
Kabla ya huyo mtunga kalenda ulikuwa unahesabu vipi masaa?
Ikawa asubuhi ikawa jioni siku 1.hapakua na masaa zaidi ya hayo ya kutazama jua linapokucha na likizama tu ni siku imeisha.ikianza jioni tena na usiku wote kwenda asubuhi ni siku ya pili pia
 
Hivi kweli watu na akili zao kabisa Wanazungumza habari za 666 kwenye mambo ya haya masaa?, yaani Hiyo 666 itambulike upitia Kiswahili tu?

Hapo Mwanzo kulikuwa hakuna saa,na saa za kwanza kabisa zilikuwa zinatumia kivuli, hivyo siku inaanza jua linapotoka mpaka saa sita 6 Mchana kivuli cha kitu kinakuwa sawa na kitu chenyewe na kisha kuanzia saa saba mchana kivuli kinaanza kugeuka kuelekea upande wa pili,
Baadae zikaja saa zile za Mercury kunakuwa na tube na mercury ndani na huwa inadrop kidogokidogo kwenda upande mmoja kisha baada ya masaa sita unageuza ile tube, hapo ndip mapinduzi ya masaa 24 yalipoanza kutoka katika masaa 12 tu ya jua

Yote kwa yote iliaminika kila baada a masaa sita 6 , siku inabadirika KWA KUFUATA MFANO WA JUA NA KIVULI kwa hiyo kwenye kila saa ni lazima effect ya SITA iwepo, SITA ndio imekuwa kama factor kwa saa zote

G'taxi
 

Siku ina saa 24. Saa tunazotumia zinegawanya sehemu 12, kwa maana ya nusu siku. Hivyo basi, ili kuweza kutofautisha kati ya mchana na usiku, kunatumika am/pm.

Kwa mataifa ambayo siku uanza saa 1 asubuhi, inakamilika saa 12 alfajiri. Kwa maana hiyo mshale wa saa ukiwekwa kwenye 1 kuashiria mwanzo wa siku, inakapofika saa 7 mchana/usiku, mshale unakuwa kwenye 1.

Kwa mataifa ambayo siku uanza saa 7 usiku, huweka mshale wa saa kwenye 1, na inapofika saa 1 asubuhi/jioni, mshale wa saa unakuwa kwenye 7.
 
Umetumia saa za kiswahili kuuiliza namba za saa zinazotumiwa na wangereza. Kiswahili saa moja ni saa 1. Kingezeza hawajasema saa 1 wanasema Seven o'clock. Saa 1 ni kiswahili.

Na washawasha!
hahahaha [emoji144] [emoji144] [emoji144]
 
Siku ina masaa 24, na SAA la ishirini na nne linakamilika saa 6 usiku hivyo saa inabidi ianze kuhesabu upya ikianzia na 1 ambayo ndiyo saa 7 usiku na kuendelea na utaratibu huo hadi itakapokamilisha mzunguko waje wa saa 24
 
Umetumia saa za kiswahili kuuiliza namba za saa zinazotumiwa na wangereza. Kiswahili saa moja ni saa 1. Kingezeza hawajasema saa 1 wanasema Seven o'clock. Saa 1 ni kiswahili.

Na washawasha!
Mkuu hata Kiingereza moja ni One na seven ni saba bado hauko sawa
 
Brainwashed ideas!
 
Ila hii itafaa kwa zile saa zinazoonesha namba na sio za mishale.
Mie sàa yoyote iwe ya mshale au digits naset kikwetu.
Na nikiangalia hizi za kizungu mara nachanganya.
Nishazoea kiswahili long time now.
 
Tazama haka kamchezo ka 666

Saa 1=saa7
7-1=6

Saa 2=saa 8
8-2=6

Saa 3=saa9
9-3=6

Saa 4=saa10
10-4=6

Saa 5=saa11
11-5=6
Hvyo utaona masaa yote yanauhusiano mkubwa na no 6 Ambayo ni no ya mnyama vicarius ama papa. Ipo history yake ambayo ni ndefu sana Juu ya kwanini mpk ikawa hivi l
 
Kwanini utoe tu na usijumlishe au kuzidisha na kugawanya. Nini influence ya kutoa?
 
Ndio mambo ya freemason ama ?
 



Saa zinaonyesha idadi ya masaa baada ya saa sita usiku, huwa inaandikwa 00:00 kwa masaa 24,au 12:00 am kwa masaa 12,hapo ndio siku huwa inaanza, sasa ukienda lisaa limoja kwa saa zote(either ni masaa 24 au 12) saa huandika 01:00 kuonyesha kuwa ni lisaa limoja baada ya leo kuanza, na hiyo tutasema ni saa saba usiku, ukienda masaa mawili baada ya saa sita usiku(yani 00:00+02:000) itakuwa ni saa nane usiku, au 02:00 au 2 hours baada ya saa sita, kwahyo 1 ni saa 7 kwakuwa ni lisaa limoja baada ya siku kubadilika(saa sita)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…