Kwanini saba iwe moja kwenye masaa?

Kwanza tukubaliane kuwa siku maja ina masaa 24. Na siku inaanza saa sita kamili usiku. Sasa hapo ukianza kuhesabu unaanzia 00:00 lakini kwa wakati huo ni usiku ikifika saa limoja inakuwa 01:00, likifika saa la pili inakuwa 02:00 na kuendelea mpaka 23:00. Hapo inakuwa masaa 24. Sasa kupanga ni kuchagua. Saa yako bwana mleta mada iset namna hii. Ikifika saa sita kamili usiku weka saa yako idisplay 00:00 ukiwa unajua ndio siku imeanza.
 
mbwembwe za mswahili tu, akiona kumekucha ndo anasema siku imeanza anaita saa moja huku kuna masaa 7 yalishapita tangu siku ianze, ndo maana wenyewe huwa wanasema seven a.m.
kwahyo kama mpango wa 666 mnao usema basi safari hii sisi wa bongo ndo tumeutengeneza 🙂
 
Inasemekana ni mfumo wa ki freemasonic, maana inasemekana namna ya freemason ni 6 hivyo kwa usomaji wa saa 7=1, 8=2 kwa mzungumko wote wa saa basi zinabaki 6, ambayo ndio namba ya freemanic
 
Thread closed!
Labda kama ni ubishi tu utaendelea.
 
saa ilianzia libya au algeria,sikumbuki vizuri,ilikua inaenda na jua kwa kupima kivuli,likitoka alfajiri hadi saa sita,kivuli kunakua sawa na kipimo,kisha saa saba kivuli kinaanza kuangukia upande mwingine,hapo walianza kuhesabu upya,yaani moja,ndo tulipopatia mfumo wetu
 
Hapana iko hivi, kwa kiswahili waweza rekebisha saa yako isome kiswahili which mean ikiwa moja utasoma saa moja ila ukiweka kwa kizungu ndipo kwenye moja utasoma saa saba na kwenye mbili utasoma saa nane hiyo ni kwa kingereza si kiswahili, hope umenielewa samjarusha
 
7am, means, 7 hours has passed since the beginning of the day, 12.01am

Kiswahili sisi hatujagundua chochote kuhusu masaa na mwenendo wake.

Tukubali kuwa tunatumika na wazungu
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
7- 1= 6
8- 2 = 6
9- 3= 6
Hapo ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita sitini na sita. (Ufunuo 13 : 8)
 
Ndiyo maana ni muhimu sana kuzingatia kutaja eneo ulipo unapotaja saa. Kwa mfano nikiwa bongo sasa hivi ni saa 10:59 jioni kwa saa za Afrika Mashariki(EAT?) Yeyote aliye upande mwingine wa Dunia atatumia time zone yetu kujua unamaanisha saa ngapi kwa GMT. Suala la inasomekaje kwenye saa yako inategemea uelewa wako kuhusu siku/terehe mpya inaanza wakati gani. Mimi kwa mfano; huwezi kunishawishi eti nianze siku usiku wa manane kama desturi ya Warumi wa kale ilivyo! Kwa hiyo ninaanza siku na tarehe mpya saa 12:00 jioni na inaisha saa 11:59 jioni. Kwa hiyo wakati wewe unasubiri usiku wa saa sita ndiyo uingie Alhamisi, mimi nitakuwa nimeianza tangu saa kumi na mbili jioni hii.
 
BaKita wanatakiwe watufumbulie hili na ikiwezekana moja iitwe moja na saba iitwe saba..
ndio maana unaambiwa Tanzania ni magenious maana mambo yao ni complicated sana....mtoto wakati yuko nyumbani anafundishwa saa kwa kilugha ,,akienda madrasa anafundishwa kiarabu mara sijui alaasir au adhuhur au magharib...akienda english media anajazwa na oclocks na 2300hours ...akiiingia mtaa anaambiwa hii ni mida ya wanga...yaani huu mchanyato ukiweza kuumaster ni lazima uwe genious.
 
Wanageuza mambo wazungu, sio watu wazuri...............................
 
Hii ni elimu ya namba(ni pana zaidi kiroho) kwa mfano kama ni saa 7 halafu saa inaandika 1, bhasi chukua 7-1=6(namba ya uasi), kama ni saa 8 ila saa inaandika 2, chukua 8-2=6 ama kama ni saa 10 halafu saa inaandika 4 bhasi chukua 10-4=6 yaani hii inaitwa 666(ikiwakilisha uasi wa mwanadamu anayelazimisha kuabudiwa kama Mungu) =pope, unajua vitu huanzia kutokea ktk ulimwengu wa roho kisha huja ktk ulimwengu halisi, shtuka chukua hatua kwa kumsoma Pope Gregorian X111 kisha utajua jinsi alivyobadili majira, mtafute Bwana ungali hai, barikiwa.
 
Nadhani unajua kua dunia imitawaliwa na 666 so kila saa ni 6


Mfano SAA 9 ni 3 je 9-3
SAA 4 ni 10 je 10-4
Usiumize kichwa

Hata ukija masaa24 utakua hujakwepa kitu cc huwa tunasema Massa 24 ndio kiswahili

Mfano kwakiswahili SAA 7 ni 13 je 13-7

Mfano SAA 11 ni 17 je 17-11
 
Huo n mpango wa Freemasonry kutumia hayo masaa ili tuwetunazungukia ktk namba za shetani(666)ambayo n pnga Kristi. Chukua 7-1=6,8-2=6...huo n mpango wa kshetan
 
Swali zuri sana, ntakujibu kama ifuatavyo..
_Chukua hyo 7 toa 1, jibu utalipata kichwa.
Chukua hyo 8 toa 2, jibu unalijua.
_vhukua 9 toa 3, utapata jibu.
NB: jibu utakalopata katka masaa yote yatafanana.. Sasabas tutafute maana ya hyo namba.
666[emoji33]
 
Ni opposite yake kwa saa ya mshale zinaangaliana.....ilipokaa saba ukacross kwa juu unaona zinatazamana
 
Watanzania Tunaanza siku asubui. Wazungu saa 6 tukianza asubui tutakuwa nyuma masaa 6
 
Mazoea yetu ya kufanya mambo bila ya tafakari.
sisi tunafuata utaratibu wa wakoloni waliotutawala...mbona wachina wanasheherekea mwaka mpya kivyao ...sisi bado tunatawaliwa na ndio maana vitu vingi tunaiga toka kwao ila wachina majority wanabuni wenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…