Kwanini reli ya SGR ya Kenya imekuwa mradi uliosifiwa sana katika ujenzi wa pamoja wa Ukanda Mmoja, Njia Moja?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111336212582.jpg


Mkutano wa tatu wa kilele wa ushirikiano wa kimataifa wa Ukanda Mmoja, Njia Moja utafanyika Beijing. Ikiwa moja ya nchi 52 za Afrika ambazo zimesaini kumbukumbu ya maelewano ya ushirikiano katika ujenzi wa pamoja wa Ukanda Mmoja, Njia Moja, Kenya imetajwa na watu wengi kuwa mojawapo ya nchi zilizonufaika zaidi na Pendekezo hili, na kwamba reli ya kisasa ya SGR imekuwa mradi wa kuigwa wa ushirikiano wa China na Afrika.

Juu ya hili, Rais wa Kenya William Ruto anayehudhuria mkutano huo wa kilele hapa Beijing, alisema ‘Kenya imefaidika na ujenzi wa pamoja wa Ukanda Mmoja, Njia Moja na kupata matunda halisi kutoka kwa mradi wa Reli ya SGR.’

Ikiwa reli ya kwanza kujengwa nchini Kenya tangu nchi hiyo ijipatie uhuru, reli ya SGR imetajwa na vyombo vya habari vya Magharibi kuwa "mojawapo ya reli 13 zinazostahiki kutumiwa zaidi duniani" na kusafiri kwa reli hii kumeorodheshwa kama "moja ya mambo muhimu zaidi yanayostahiki kufanywa nchini Kenya”.

Tangu kuzinduliwa rasmi kwa reli hiyo mnamo Mei 31, 2017, imekuwa ikisafiri kwa usalama kwa zaidi ya miaka 6. Mstari wa ‘Nyumbani kwetu kunazidi kupendeza na wenzagu wanazidi kuishi kwa uchangamfu siku baada ya siku" uliomo katika wimbo wa "Reli ya SGR Inafika Nyumbani Kwetu" ulioimbwa na mwimbaji wa Kenya Sudi Boy sasa umekuwa ukweli halisi.

Katika kipindi cha miaka sita iliyopita, wakati reli hii imekuza maendeleo ya kiuchumi ya Kenya, pia imetengeneza karibu nafasi za ajira elfu 50 kwa nchi hiyo, ambapo wafanyikazi wengi wazawa wamekuwa na uzoefu mkubwa. Kwa mfano, Concilia Owire, mtu mashuhuri nchini Kenya, alianzia kuwa mfanyakazi wa kawaida hadi kuwa mmoja wa madereva wa kwanza wa kike nchini Kenya, na sasa anahudumu kama msaidizi mkuu wa kitengo cha reli, hadithi zake zimeelezea kwa uhai kiini cha Ukanda Mmoja, Njia Moja, yaani ushirikiano na maendeleo.

Hali halisi ni kwamba vyombo vya habari vya Magharibi havijaacha kukashifu kwa nia mbaya reli ya SGR. Moja ya madai yaliyotolewa mwanzoni mwa ujenzi kwamba "mradi huo utatishia maisha ya wanyama pori", na nyingine ni mtego wa madeni" ambayo bado inasikika mara kwa mara hadi leo.

Hata hivyo, ukweli ni kwamba reli ya SGR haijaharibu mazingira ya awali ya maisha ya wanyama pori wakubwa kama twiga na tembo, na imesifiwa na kutambuliwa sana na vyombo vya habari vya Kenya na wanamazingira wa huko. Kuhusu kauli isiyo ya kweli ya "mtego wa madeni", Rais Ruto amejibu tena mjini Beijing kwamba, "Tunajua tunachotaka, tunajua marafiki zetu ni akina nani, na tunajua jinsi ya kuchagua washirika."

Ukweli umethibitisha kwamba njia bora ya kujibu propaganda mbaya za nchi za Magharibi kuhusu ushirikiano kati ya China na Afrika ni kwamba China na Afrika zinazingatia nia ya awali ya kujenga kwa pamoja Ukanda Mmoja, Njia Moja na kuleta miradi ya ujenzi ya China barani Afrika na ushirikiano kati ya China na Afrika kuendelea kutoa matunda yanayoonekana kwa maendeleo ya kiuchumi ya Afrika na kuboresha maisha ya watu.

China imefanikiwa kupata maendeleo kwa mtindo wa Kichina huku ikiheshimu nchi nyingine katika kuchunguza njia zao za kisasa. Hii ni sababu muhimu kwa nini zaidi ya nchi 150 na mashirika zaidi ya 30 ya kimataifa kujiunga na familia ya Ukanda Mmoja, Njia Moja.

Dunia inatarajia kuona ukurasa mpya utakaofunguliwa na Ukanda Mmoja, Njia Moja, na inaamini kuwa mkutano wa tatu wa ushirikiano wa kimataifa wa Ukanda Mmoja, Njia Moja utafikia makubaliano zaidi na kuendelea kuwezesha Pendekezo hilo kupata sifa nzuri zaidi miongoni mwa watu wa nchi mbalimbali.
 
Back
Top Bottom